hippocratessocrates
JF-Expert Member
- Jul 1, 2012
- 3,598
- 1,544
Vipaumbele:
1. Elimu
2. Afya
3. Kilimo
4. Miundombinu
5. Utawala bora
6. Mawasiliano
Swali: Je, kwa takribani miaka 54 ya kuwa madarakani wametekeleza hayo kwa kiwango gani cha kuridhisha wananchi?!
Je, kwa sasa kuna miujiza gani watakayotumia kutekeleza ilani hiyo?
Kama kwa zaidi ya nusu karne wameshindwa kutekeleza haya, badi pengine hawatufai kabisa(Hawakutufaa toka mwanzo).
1.ELIMU:
Nchi hii watu wanasomea chini ya mti(Kongwa Dodoma), Bunge liko Dodoma.
Nchi hii kule Geita wanafunzi wanasoma katika madarasa ambayo hayajaezekwa(Geita atokako Mh. Magufuli).
Elimu hii inayochezewa kwa wanafunzi kujihangaikia masomoni(kwa shida) na kushindwa kuajiriwa na wakimaliza wanashindwa hata kuajiriwa.
Elimu hii yenye kubadilishwa mitaala karibu kila baada ya mwaka hadi miaka miwili na kufanya wanafunzi kutokujielewa.
2. AFYA.
Sehemu ambapo hata Hospitali ya Taifa wataalamu wako tele lakini wenye kutoleana macho tu mgonjwa anapofika kwasababu ya kutokuwa na vifaa tiba, dawa.
Sehemu ambapo Serikali inahadaa wananchi huduma bure, lakini hakuna hospitali yenye kutoa huduma bure hata kwa makundi maalum(wazee, wajawazito, watoto wadogo wenye umri chini ya miaka mitano).
Nchi ambayo mwananchi asiye mtumishi wa Serikali hapati fursa/kuhimizwa kutumia BIMA, na yule aliye mtumishi ingawa anapata huduma za kitabibu bado huduma ya dawa ni changamoto.
Nchi ambayo Wananchi wanalala chini...chini katika/kwenye sakafu wakiwa hospitalini kwa uhaba wa vitanda lakini viongozi wa nchi wakitibiwa nje kila leo, in the name of ' ni pesa yake, kama anamudu kwanini asiemde'
3. KILIMO:
Migogoro kushindwa kutatuliwa kati ya wafugaji na wakulima.
Kushindwa kumjali mkulima mdogo(small scale) katika uuzaji, kuwapangia bei watakazo katika masoko.
4. MIUNDOMBINU.
Hivi si Nchi hii yenye kukumbwa na Mafuriko kila mwaka, anticipation kushindwa kufanyika kila mwaka?
Nchi ambayo baada ya mafuriko tunalia tunakosa maji tukishindwa ku_harvest haya maji kwa matumizi ya baadae.
Nchi ambayo Umeme unakosekana despite vyanzo kadhaa vya umeme(Maporomoko, Makaa ya mawe, Vyura wa Kihansi, Mabwawa, Nishati ya jua, Gesi) sehemu ambapo tu hata kwa Nishati ya jua kila kijiji kina uwezo wa kuwa na Solar (Wananchi wakichangia na Serikali ikiwawezesha).
Nchi ambayo barabara zake zahitaji ukarabati kila mwaka( na sehemu nyingine utanuzi).
UTAWALA BORA:
Nchi ambayo Serikali(Mhimili mmoja wa dola una nguvu na kandamizi kushinda mwingine, lakini pamoja na jitihada za kuboresha hili kupitia Katiba mpya Serikali hiyo hiyo(Kupitia watu wale wale waliodanganya umma kywa watahakikisha Katiba inapatikana kabla ya kumaliza hatamu ya uongozi kuhafifisha suala hili.
Nchi ambayo Watawala ni watu wenye kuwaweka ndugu na jamaa zao katika ngazi za juu(na chini pia) hata kama hawana uwezo/vigezo vya kuwepo huko na wenye kufanya maamuzi yasiyo na tija kwa Taifa.
6. MAWASILIANO.
Mawasiliano kutunza nyaraka za Serikali. Hili ni jambo zuri, lakini hebu tujiulize kama katika kipindi cha miaka kumi iliyopita Siri na nyaraka kupitia njia nyingi za mawasiliano ya Setikali vimefichuliwa hivi na bado Serikali haioni haya/aibu kwa uozo ulio ndani yake wala hakuna jitihada kurekebisha, itakuwaje pale ambapo tutazuiliwa na sheria kandamizi kupata hata hicho kidogo(uozo) Serikalini.
Kama wameshindwa haya kwa zaidi ya nusu Karne hawataweza hata kama tukiwapatia Nchi kwa Karne nzima. Failure has been proved by CCM.