Elections 2015 Ilani ya CCM 2015-2020 - Uchaguzi Mkuu 2015

Elections 2015 Ilani ya CCM 2015-2020 - Uchaguzi Mkuu 2015

Ilani ya Magufuli imeandaliwa na CCM ileile iliyochoka na ambayo imeshindwa kutekeleza, hayo yote yaliomo kwenye ilani hata kama amekabidhiwa Magufuli ataishia kuisoma ilani jukwaani,kwenye utekelezaji ni 0.
 
Magufuli huyu huyu aliahidi bungeni ujenzi wa barabara njia nne ya arusha -moshi miaka miwili iliyopita alichofanya kila ikikaribia bajet anaweka alama za road reserve nenda toka sakina hadi mjini
 
Mkuu ujenzi wa barabara siyo kama mtu anakwenda kujenga jiko la kupikia
 
Tukiacha mipasho, vijembe na zomea zomea pamoja na minenguo ya burudani nzuri, haya ndo mambo yatakayo mpaisha Dr John Pombe Magufuli.

Issues za JP Magufuli in Summary:
1. Umoja wa Taifa
2. Kulinda Muungano wa Tanzania.
3. Ulinzi na usalama
4. Kuheshimu mihimili ya Dola.
5. Mahakama maalum ya mafisadi na majizi
5. Utawala bora
7. Ataheshimu mawazo yote ya kuleta maendeleo hata yakitoka upinzani
8. Ataimarisha vyombo vya usalama
9. Vita dhidi ya ubadhirifu
10. Kodi ilipwe na wote
11. Ataongeza ajira kwa kuimarisha viwanda
12. Sekta ya kilimo itaimarishwa
13. Sekta ya mifugo itaimarishwa ili iwe na tija kwa kujenga viwanda
14. Madini yatadhibitiwa ili yalete maendeleo
15. Maji yatapelekwa Vijijini na mijini
16. Zahanati kila kijiji, Hospitali ya rufaa kila mkoa, kuboresha maslahi ya wauguzi
17. Elimu bure hadi kidato cha nne, nyumba za walimu zitajengwa.
18. Wanafunzi wa vyuo vikuu, atahakikisha mikopo inakwenda mapema ili wasome
19. Kujenga hostel za mwana vyuo
20. Maslahi ya watumishi, kila mtu anayefanya kazi atapata haki yake.
21. Gesi itasimamiwa vyema ili isaidie nchi
22. Barabara zitaboreshwa, flyovers kujenga ya kwanza salander, tazara
23. Msongamano Dsm utashughulikiwa
24. Reli itajengwa upya
25. Bandari, anga zitaboreshwa
26. Maslahi ya maliasili yataboreshwa ili watalii wengi waje ili tupate pesa
27. Serikali itakuwa rafiki kwa wawekezaji wenye nia njema
28. Maslahi ya wafanyakazi yatalindwa
29. Walemavu watalindwa na haki zao zitalindwa
30. Uhuru wa Habari utalindwa na atakuwa na waandishi karibu
31. Wasanii na wanamichezo haki zao zitalindwa, kutakuwa na Mfuko maalum kwa ajili hiyo
32. Reli ya Dar itajengwa

UKAWA waje na mbadala tuone.


CCM ni mabingwa wa jadi wa ahadi zisizotekelezeka.

Pekuapekua ahadi za Jakaya Kikwete uone aliyoahidi na aliyotekeleza.


CCM ni rangi ile ile mkuu masopakyindi.

Shtuka!!
 
Last edited by a moderator:
UKAWA waje na mbadala tuone.
Kwani lazima ya UKAWA iwe mbadala? Haikubaliki ilani kufanana maudhui? Kama UKAWA wangeanza kutoa ilani yao kama hiyo, CCM wangeibadili hii? Hivi kuna watu bado wanaamini katika ilani? Mbona vyama vyote tu vina ilani nzuri tu? JK alitekeleza mambo yasiyomo kwenye ilani ya CCM mfano Katiba mpya, akayaacha yaliyo katika ilani ya CCM mfano Mahakama ya Kadhi. Je, alifanya vibaya?
 
safi sana mwaka huu mafisadi lazima wakae tu hata iweje.
 
Yote yaliyopo katika ILANI YA CCM yanayoweza kutekelezeka hayo ya itifaki, mishahara ya viongozi, posho, magari ya kifahari na nk.

Kwa sababu serikali chini ya ccm haijawahi kumpa mlipa kodi kipaumbele ndio maana daima maslahi yao mbele. Moja ya kielelezo kuwa tunalipa kodi kwa ajili ya maslahi kwanza viongozi jinsi wanarukiana vichwa kama mbuzi, rushwa na hujuma kupata nafasi za ubunge.

Hakuna litalowezekana isipokuwa kupitia kodi tutazolipa sisi wenyewe, hivyo maendeleo ni haki yetu sio zawadi au hisani.

Kwa maana mikopo yote tutalipa kwa kodi zetu watanzania wanyonge, si mnajua mwalimu unalipa kodi kupitia mshahara wako mdogo lakini wabunge, mawaziri, rais halipi kodi japo mishahara yao kwa mwezi ni mshahara wa mwalimu miaka miwili na nusu.
 
Nilishangaa kusikia kuna div 5, na nlisikitika kuona waziri wa elimu hajui kusoma wala haijui nchi yake!!! Nlihuzunika kuona twiga wanapandishwa ndege...bila kusahau uharamia wa pembe za ndovu!!! Wizi wa fedha za serikali...utumiaji wa mabavu na vyombo vya ulinzi!!

Kwa kuongezea tu, 1usd=2000+ tsh!!!
HII YOTE NI BAADA YA MIAKA ZAIDI YA 50 YA UHURU!!! WE NEED UKAWA NOTHING ELSE.
Cc baro The Tomorrow People na wooote ambao wanajidanganya ccm ndio jibu la shida za wa tz.

yeye kama kiongozi mkuu wa awamu ya tano, inatakiwa umhukumu kwa aliyoysema pia muangalie usoni na anachokisema je kinaendana , dr maghufuli atatuvusha ni kiongozi mwenye muono wa miaka 100 ijayo, naamini Tanzania tutakuwa na kupaa kiuchumi kuliko utawala wowote

TM 2015( Twende na Maghufuli 2015)

Hapa kazi tu
 
CCM HAINA TENA WABUNIFU NA ILANI YAKE IMEDHIHIRISHA KUCHOKA KWA CCM.


TUIPUMZISHE.

katika taasisi yoyote lazima kuwepo na magwiji wa ubunifu,mikakati mizito na stadi. hawa kwa kimombo wanaitwa THINK TANKS.

kwa mara ya kwanza kabisa nimeshuhudia CCM ikifeli kwa kila kitu.

kuanzia kauli mbiu ya CCM mwaka huu. nimeona Magufuli akisema wao ni KAZI TU.


ilani ya CCM kwa kadri ilivyoelezwa.

ELIMU:
Itakuwa bure kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne.

hakuna matumaini ya kuifanyia mapinduzi elimu yetu iliyodorora kabisa huku ikikumbwa na matatizo lukuki kama ukosefu wa mazingira stahiki ya kujifunzia na kujisomea, ukosefu wa mabweni mashuleni, ukosefu wa maji mashuleni, ukosefu wa vifaa vya kujifunzia ikiwemo vitabu na vifaa vya maabara,ukosefu wa umeme mashuleni.

eti CCM imeishia kuahidi elimu bure mpaka kidato cha nne katika mazingira hayahaya ya shule za kata ambazo hazina umeme,hazina mabweni,hazina vitabu, hazina maji, hazina nyumba za walimu nk.

CCM haina tena magwiji wenye uwezo wa kulisaidia taifa hili.

elimu nchini Tanzania ipo katika mdororo usioelezeka na kunahitajika mipango madhubuti ya kuifanyia mapinduzi elimu yetu ili iwe ya kisasa zaidi na yenye kuakisi ubora wa juu kabisa ndani ya miaka kumi ijayo. CCM imefeli kabisa na kudhihirisha kuwa imechoka sana kwa ilani hii ninayodiriki kuiita kuwa ni ilani isiyostahili kupelekwa kwa wananchi.

UCHUMI.

nchi kwa sasa inahitaji mipango na mikakati makini ya kulifanya taifa lipige hatua kubwa katika maswala ya TEKNOLOJIA NA VIWANDA ili kulifikisha taifa katika mapinduzi ya viwanda katika miaka isiyopungua 30 ijayo. naona hapa ccm haina kabisa mpango wala mkakati wowote wa kueleweka.

mimi Joseph Mshinga sipo tayari na sitakuwa tayari kuunga mkono ilani yoyote katika kipengele cha UCHUMI ikiwa hakuna mpango wenye matumaini ya kulifanyia mapinduzi ya viwanda taifa letu. Hatuwezi kuwa taifa la kuombaomba miaka yote. CCM katika kipengele hiki wanaomba wapewe kuiongoza nchi kwa staili ileile ya kuombaomba na kukopa. Kibaya zaidi wanaendeleza mazingira ya kulifanya taifa letu liendelee kuwa la kuombaomba,kukopa na tegemezi ili tuendelee kuuza madini na kila aina ya utajiri wetu kwa mikataba ya bei ya pelemende kwa kuwa hatuna teknolojia. CCM mpaka sasa ni chama cha ujamaa lakini katika ilani yao hakuna ujamaa uliowekwa na wala hakuna ile kauli maarufu ya ujamaa na kujitegemea lakini naona hapa ccm inatuhakikishia kuendelea kulifanya taifa letu kuwa tegemezi badala ya kujitegemea. #HILI HALIKUBARIKI# kwa manufaa ya taifa na vizazi vijavyo tuikatae katakata CCM isiendelee kutuharibia taifa letu.

sisi tunahitaji taifa ambalo ifike muda madini yetu tuchimbe wenyewe kwa teknolojia yetu wenyewe, tutengeneze bidhaa zetu wenyewe kutokana na raslimali asili zetu kwa teknolojia yetu na kwa viwanda vyetu. CCM haina kabisa think tank kwa sasa. Ilikuwa miaka ya 70(1970s) wakati ambapo viongozi wa wakati ule waliamua kuanzisha viwanda vya kila aina katika kila kona ya nchi ili kuuishi uchumi halisi. leo ccm haina tena uwezo huo na wala historia hawaikumbuki tena.


CCM THINK TANK HAS BROUGHT THIS VERY POOR MANIFESTO EVER SEEN IN TANZANIA GENERAL ELECTION.

hotuba ya Magufuli imejikita katika kuongelea matatizo madogomadogo ambayo ni ya kiutendaji na majibu ya kutaka na kutatua matatizo ya watanzania hayamo katika ilani ya CCM. TUIKATAE CCM.

tunahitaji uchumi imara utakaofanya yafuatayo.

1.uchumi utakaoruhusu darasa la saba kuwa na ajira zinazoendana na elimu yao kwa kuwa siyo kila mtanzania atasoma zaidi ya darasa la saba.

2.uchumi utakaoruhusu na kuwahakikishia wenye elimu ya kidato cha nne nao kupata ajira kulingana na elimu yao maana si kila mtanzania ana ndoto za kusoma zaidi ya kidato cha nne. Wengine elimu ya form four inawatosha kwa matakwa yao lakini lazima tuwe na uchumi unaowahakikishia kundi hili ajira ili waweze kuendelea na maisha yao.

3.uchumi utakaowahikishia kidato cha sita kupata ajira zinazolingana na elimu yao na ujira unaolingana na elimu yao. siyo lazima kila mtanzania afike chuo kikuu lakini tuna wajibu kama taifa kuhakikisha kila kiwango cha elimu kinaingia kwenye mfumo wa ajira kwa kulihakikishia kundi husika kupata kazi/ajira ili kila mtu aishi kwa kazi yake.

4. uchumi utakao wahakikishia wenye elimu ya chuo kikuu kupata ajira na ujira unaolingana na elimu yao.Kwa mazingira ya sasa hata wenye degree hawana uhakika wa kupata ajira. kwa mantiki hiyo hata wenye elimu ya chini wengi wanalazimika kujitahidi wafike chuo kikuu ili kwa kiasi fulani waweze kupata jira lakini bado hata degree haimhakikishii mtanzania kupata ajira hata ile ya kinyonyaji. Tunahitaji uchumi wa kutoa ajira kwa kila kundi.

5.tunahitaji uchumi wa kulifanyia mapinduzi taifa katika sekta ya elimu,afya, miundombinu nk.

uchumi ukiwa imara watanzania watafanya mambo mengine wao wenyewe kupitia vipato vyao halali.


mfano.
#mtu mwenye kazi na mshahara hahitaji kusomeshewa mtoto wake bure. kwa hiyo wazazi wengi wakiwa na kazi zao wanaweza kuwapeleka watoto wao shule kwa gharama zao. Umasikini ndio unawafanya watanzania wahitaji usaidizi kutoka serikalini katika kusomesha watoto wao lakini kama wakiwa na kazi kila mtu ataweza kumsomesha mtoto wake na kumudu gharama zinazohitajika.

#wakiwa na kazi kila mtu anaweza kumudu kujenga nyumba yake ya kawaida na kuishi maisha anayoyataka.


nk nk nk nk.

kwa sasa ni sahihi kuwa baadhi ya mambo yanahitaji usaidizi wa serikali kabla uchumi haujasimama na kumuwezesha mtanzania kugharamia mwenyewe gharama hizo kupitia ajira yake. Mambo hayo ni pamoja na kuifanya elimu kuwa ya bure mpaka chuo kikuu ili kila mtanzania mwenye uwezo na nia ya kuifikia elimu ya juu asome na kufika huko bila kujali kama ni watoto wa matajiri ama wa masikini. kwa mantiki hii elimu ya bure bado ina umuhimu mkubwa katika mazingira ya sasa.

TUIKATAE CCM ILI KULIOKOA TAIFA.

NA:
JOSEPH NGIKILI MSHINGA
@(visioned to industrial revolution)@
 
Yote yaliyopo katika ILANI YA CCM yanayoweza kutekelezeka hayo ya itifaki, mishahara ya viongozi, posho, magari ya kifahari na nk.

Kwa sababu serikali chini ya ccm haijawahi kumpa mlipa kodi kipaumbele ndio maana daima maslahi yao mbele. Moja ya kielelezo kuwa tunalipa kodi kwa ajili ya maslahi kwanza viongozi jinsi wanarukiana vichwa kama mbuzi, rushwa na hujuma kupata nafasi za ubunge.

Hakuna litalowezekana isipokuwa kupitia kodi tutazolipa sisi wenyewe, hivyo maendeleo ni haki yetu sio zawadi au hisani.

Kwa maana mikopo yote tutalipa kwa kodi zetu watanzania wanyonge, si mnajua mwalimu unalipa kodi kupitia mshahara wako mdogo lakini wabunge, mawaziri, rais halipi kodi japo mishahara yao kwa mwezi ni mshahara wa mwalimu miaka miwili na nusu.
Vizuri sana tena sana!
Sasa tupigie kura ya (V) kwenye kiboksi cha kura tuendelee kuwaletea maendeleo .
 
Tunatakiwa tuweke thread ya Sera za CCM Tangu Mfumo wa vyama Vingi kuanza.Wale wenye kumbukumbu watusaidie.Mimi binafsi naona marudio,hizo zimeendelea kuwa fimbo za kumchapa mpumbavu na Lofa.Wameanza Goli la mkono,wakaenda na kusema ni makapi waliohama CCM,hawakuishia hapo wanaendelea kusema Oil chafu na msumari wa kwanza wa aliyewahi kuwa mkuu wa kaya anaongea kwa nguvu kubwa tena ya kujiamini!!! Wapumbavu na Malofa!! Tumewavumilia sanaa,this is too much.
 
tumeitwa wapumbavu na malofa je?watahitaji kura za malofa na wapumbavu?
 
Ni Tanzania pekee nimeona wanasiasa wana vipaumbele zaidi ya 100 wakiingia madarakani.

Kwanini mwanasiasa asiwe na kipaumbele kimoja tu, kwa mfano Elimu au afya au kilimo au usafiri au viwanda na biashara.

Ccm ni wale wale, wanaahidi vitu vile vile ambavyo havitekelezeki,
 
Kusema ukweli Magufuli anaweza maana siyo mwanasiasa. Naamini atafanyakazi kurudisha heshima ya ccm
Angekuwa mjanja angeainisha vyanzo vya mapato vya kutekelezea ahadi hizo, kama hana basi amfuate January Makamba !
 
Tingatinga lazima awahenyeshe safari hii

Kwa ahadi hewa kama za mtanguliz wake. Tangu lini uliona ahadi 100 zikatekelezeka? Mwenzio hizo 67 zimekuwa mwiba mchungu,sembuse hizo100
 
Tunatakiwa tuweke thread ya Sera za CCM Tangu Mfumo wa vyama Vingi kuanza.Wale wenye kumbukumbu watusaidie.Mimi binafsi naona marudio,hizo zimeendelea kuwa fimbo za kumchapa mpumbavu na Lofa.Wameanza Goli la mkono,wakaenda na kusema ni makapi waliohama CCM,hawakuishia hapo wanaendelea kusema Oil chafu na msumari wa kwanza wa aliyewahi kuwa mkuu wa kaya anaongea kwa nguvu kubwa tena ya kujiamini!!! Wapumbavu na Malofa!! Tumewavumilia sanaa,this is too much.
Ulizaliwa enzi za chai maharage, huoni mbadiliko?
 
Kwa nondo hizi lazima UKAWA wakae

Wacha mihemko we ndugu mimi ni gamba lakini ebu angalia hii santuri si ni ya miaka yote? Tangulini sisi na utekelezaji ? Tukomeni kuwadanganya masikini wa taifa hili .
 
Back
Top Bottom