Ili nipate uteuzi ni lazima kuwa kada wa CCM au niwe Chawa wa Mama?

Ili nipate uteuzi ni lazima kuwa kada wa CCM au niwe Chawa wa Mama?

Liverpool VPN

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2020
Posts
6,958
Reaction score
16,358
INTRODUCTION
Eeh bwana ehh habari zenu

Nikiri Mimi sio shabiki kabisaa wa siasa. Yaani sina Kadi ya chama chochote na sifikirii kuwa na Kadi ya chama chochoteee kileee.

Na kifupi huwa sifatilii zile habari za siasa zaidi ya hizi ambazo zinapostiwa insta kwenye page za habari za labda msingwa, Ikulu, na Wizara.

Mimi ni mtumishi wa halmashauri, Elimu yangu ni Bachelor of Science in ..... na Masters of Science in ....., na nina miaka 10 kazini Halmashauri (experience).

SCENARIO
Juzi mama alivyoteua ma-DC Kuna jambo nikakumbuka, nimeoma niwashirikishe ili mnipe jibu.

Kipindi kile mama alivyomteua nadhani Mkuu wa Magereza nilikua Dodoma kwenye semina Morena Hotel.

Sasa tukiwa tunapiga breakfast seminani zikapita gari V8 kaliii nyeusi na ving'oro pale kwenye lami ya Morena, kwamba Mkuu wa Magereza anaenda Ikulu kuapishwa.

Mimi nikaropoka "Mimi huyo miaka 5 ijayo nitapanda hizo gari nikielekea Ikulu kuapishwa baada ya kula uteuzi wa Mama"

Sasa tukiwa pale mezani jamaa mmoja akaniuliza "Una Kadi ya Chama?" Jibu likawa hapana. Ila tulipiga story na vitu vingiii kuhusu uteuzi na CCM, ila niliondoka na hili.

PROBLEM
Ili upate uteuzi haijalisha muda wako wa Kazi (Experience/duration), Haijalishi Elimu yako, ila KINACHOTAKIWA UWE NA KADI YA CHAMA CCM.

Kwamba, hata upige Kazi vipi ofisini ila ili uonekane Basi ni lazima uwe na Kadi ya CCM. Yaani ukitaka tobo la uteuzi basi shikiria Kadi ya CCM na uitangaze kama unayo, yaani ishi ki-CCM.

QUESTION

Sasa Je, ni kweli hili jambo ni sahihi? Kwamba pamoja Nina Miaka 10 serikalini na elimu ya Masters ila bado natakiwa kuwa Kadi ili mama anione mimi mtumishi wake Bora huku Kijijini?

(Halmashauri yetu ni Chaka/vijiji hasa)

Yaani ili nilambe uD(R) C, uDED, uD(R)AS, na vyengine ni lazima nijinadi ndani ya CCM na kuwashughulika na hoja za wapinzani mpaka mama atakaponisikia na kuniona?

Kwamba nikiwa hivihivi Neutral (kama nilivyosasa sina Kadi) basi hata nipige Kazi haswa ila NISAHAU UTEUZI?

#YNWA
 
Inabidi ujitoe akili, mwenyekiti akijamba sifia sema ushuzi unanukia vzr unaweza tibu njaa ya wadanganyika, mwenyekiti akipora mali za umma sifia sema anaipiga mwingi, yaani uwe jama zezeta. Zaidi wqpinzani wawe maadui zako wa kwanza kuliko chochote hata kama ni wazazi wako watukane wakemeee wafanyie fujo ili mpaka mwenyekiti asikie kuna chawa yupo kazini.
 
Uko halmashaur gani ivo vitu n konekshen tu mda mwengine ongea na watu ka sie utapata tu teuzi one day unaweza kuwa ccm chawa haswa mwisho ukawa kunguni na usile uteuzi mpk kufa
 
Watumikie wananchi huko kijijini kwenu wapate huduma Bora na up mshahara wako wa 400k unatosha mkuu

Nani kakwambia Nina mshahara wa 400k. Kwa akili zako za kawaida miaka 10 kazini nikiwa na bachelor then napokea 400k?

Anyway ndio akili za vijana wetu wa TZ.

YANGA BINGWA.

#YNWA
 
Nani kakwambia Nina mshahara wa 400k
Kwa akili zako za kawaida miaka 10 kazini nikiwa na bachelor then napokea 400k?

Anyway ndio akili za vijana wetu wa TZ.

YANGA BINGWA.

#YNWA
Wakitoa Kodi unabaki na 300k+ Kazi mnayo Sana ndo maana hatuoi mkuu

Hata Mimi napokea 500k nipo katika sonona nimeshindwa Hadi kuoa
 
With my respect kwako mkuu nawe unaamini kuwa nchi hii itatawaliwa na ccm milele?,why kuna issue ya kuwa na kadi ya ccm?,ndio maana tunahitaji katiba mpya maana inapotokea kuna nafasi ya mkuu wa magereza inatangazwa na kama una sifa nawe unaomba,it's time to stop kuwa maisha yetu politicians ndio wanatuamulia!
 
With my respect kwako mkuu nawe unaamini kuwa nchi hii itatawaliwa na ccm milele?,why kuna issue ya kuwa na kadi ya ccm?,ndio maana tunahitaji katiba mpya maana inapotokea kuna nafasi ya mkuu wa magereza inatangazwa na kama una sifa nawe unaomba,it's time to stop kuwa maisha yetu politicians ndio wanatuamulia!

Fact.

#YNWA
 
1. Uwe na unatashi wa kupata kazi unayoitaka.
2. Uwe well connected na watu sahihi kama mapadre, mkuu wako wa kaz, chama, usalama na wizaran

3. Mlengo wa kisiasa ujulikane, umtukuze mama

4. Pesa, kwa ajiri ya nauli, kuhudumia koneksheni na kuhonga itakapobidi.
 
Back
Top Bottom