Ilikuwa kosa kubwa sana Joseph Kabila kumuibia Tshisekedi ushindi wa urais Congo dhidi ya mshindi halali, Fayulu

Ilikuwa kosa kubwa sana Joseph Kabila kumuibia Tshisekedi ushindi wa urais Congo dhidi ya mshindi halali, Fayulu

Uchaguzi wa Congo DRC wa mwaka 2018 ulikuwa ni fursa ya dhahabu ya Congo kurekebisha mambo mengi sana na kuipa nchi hiyo muelekeo sahihi wa kitaifa kwa mara ya kwanza ila uroho wa madaraka wa Kabila kulinda maslahi yake na kutoheshimu matakwa ya raia ukaikosesha Congo fursa hiyo.

Katika uchaguzi wa DRC wa mwaka 2018 ni wazi kwamba Martin Fayulu alishinda uchaguzi huo kwa kura nyingi sana lakini Kabila akaingilia Tume ya Taifa ya uchaguzi(CENI) kumsimika Tshisekedi aliyemuahidi atakuwa kibaraka wake.

Martin Fayulu alikuwa ni mgombea aliyeweza kuunganisha makundi mengi tofauti ya Congo, alikuwa na ushawashi mkubwa, huenda angeweza kuipa Congo ahueni kwa mara ya kwanza tofauti na Tshisekedi aliyeingizwa kwa msaada wa Kabila kupora uchaguzi.
Kura zinaibiwa na maccm leo ndiyo ukalie kupigia kelele kura za Congo?
 
Hiyo 99.99% inawezekana kwasababu Kagame kaleta Amani ambayo haijawahi kuonekana Rwanda mimi nimeshawahi kuishi Rwanda ya Habyarimana ilikuwa hakuna Amani kama hii ya sasa.

Wanyarwanda wanajua nini maana ukosefu wa Amani ndio maana wanampenda Kiongozi wao.
Kwa hiyo Kagame akifa amani amna tena ndo maana Rwanda tunasema ina safari ndefu sana
 
Katumbi hata hakugombea 2018, mgombea wa Kabila alikuwa anaitwa Emmanuel Ramazani Shadary ambaye alipata kura kidogo sana ndio ikabidi Kabila ale dili na Tshisekedi.
Haya bhana, niliyachanganya madesa
 
Hiyo 99.99% inawezekana kwasababu Kagame kaleta Amani ambayo haijawahi kuonekana Rwanda mimi nimeshawahi kuishi Rwanda ya Habyarimana ilikuwa hakuna Amani kama hii ya sasa.

Wanyarwanda wanajua nini maana ukosefu wa Amani ndio maana wanampenda Kiongozi wao.
Mbona sasa anaua wapinzani wake kama anakubalika hivo.
 
Kati ya Fayulu na Tshekedi, Kagame hamtaki Tshekedi, bora Fayulu.
Kwani Kagame ni nani mpaka awe na mtu anayemtaka katika uchaguzi wa wakongoman.

Huyu kagame yatamshinda tu, siku zake zinahesabika. Asilimia 90 ya nchi za afrika hazimpendi na anasemekana ndio chanzo cha mgogoro nchini Kongo.
 
Uchaguzi wa Congo DRC wa mwaka 2018 ulikuwa ni fursa ya dhahabu ya Congo kurekebisha mambo mengi sana na kuipa nchi hiyo muelekeo sahihi wa kitaifa kwa mara ya kwanza ila uroho wa madaraka wa Kabila kulinda maslahi yake na kutoheshimu matakwa ya raia ukaikosesha Congo fursa hiyo.

Katika uchaguzi wa DRC wa mwaka 2018 ni wazi kwamba Martin Fayulu alishinda uchaguzi huo kwa kura nyingi sana lakini Kabila akaingilia Tume ya Taifa ya uchaguzi(CENI) kumsimika Tshisekedi aliyemuahidi atakuwa kibaraka wake.

Martin Fayulu alikuwa ni mgombea aliyeweza kuunganisha makundi mengi tofauti ya Congo, alikuwa na ushawashi mkubwa, huenda angeweza kuipa Congo ahueni kwa mara ya kwanza tofauti na Tshisekedi aliyeingizwa kwa msaada wa Kabila kupora uchaguzi.
Nasikia utaongozana na Netanyahu mpk USA..lkn nashangaa upo Goma sahv 🤣
 
Aliyeobiwa kura na kusimikwa Tschekedi ni Katumbi Gavana wa Lubumbashi na mmiliki wa TP Mazembe na sio Fayulu.

Fayulu alikuwa mgombea wa chama cha Kabila, ila alishika nafasi ya 3 ikabidi hesabu zifanyike kwa Tschekedi na Katumbi ndio ikawa hivyo
Tume ya uchaguzi ilokuwa chini ya Nangaa ilimtangaza Tshisekedi kuwa ndiye mshindi kwa asilimia 38.56 na Martin Fayulu akishika nafasi ya pili kwa kupata asilimia 34 na wa tatu alikuwa Emmanuel Ramazani Shadary ambae alipata asilimia 23.

Fayulu alipinga matokeo hayo akisema Tshisekedi alikula njama na Kabila kuchakachua kura na akaenda kwenye mahakama ya Katiba ambako mapingamizi yake yalitupiliwa mbali.

Kanisa katoliki nalo lilitoa kauli kuonyesha mashaka yake juu ya uchaguzi huo.

Uchaguzi wenyewe ulipangwa ufanyike 2016 lakini Kabila akaanza kupiga danadana na ni shinikizo kutoka jumuiya ya kimataifa ndilo lilomfanya Kabila apange uchaguzi ufanyike mwaka 2017 na ukazogezwa tena hadi 2018 na hapo pia machine za kupigia zipatazo 8000 ziliungua moto ulotokea kwenye bohari za tume ya uchaguzi. Machine hizo ilikuwa ni mara ya kwanza zingetumika kweye uchaguzi nchini Congo DRC.

Makubaliano yalikuwa chama cha Kabila kimuunge mkono Chadary awe mgombea wao lakini Katumbi na Jean-Pierre Bemba wakapinga wakimtaka Martin Fayulu ndie awe mgombea.

Lakini hapohapo kuna mtu akaja na majina mfukoni na majina hayo yakawa Tshisekedi na Vital Kamerhe ambae angekuwa Waziri mkuu wa Tshisekedi.

Hivyo kulifanyika kitu chaitwa "double knock effect" kwanza majina yametoka mfukoni na pili, uchaguzi ukachakachuliwa.
 
Mtaongea Yote Ila Shida za Wakongomani zinaletwa na west wakubwa wa dunia wananjaa na madini (resources) Njia inayotumika (Divide & Rule). Unafikiri Rwanda anapata wapi kiburi yote hiyo kufadhili M-23? Anaback up kubwa ya mabepari PK anakuambia Usiponikaribisha NitajikaribishaMwenyewe.
Huo ni uongo mtupu, kwani aliyeko madarakani amekataa kuwauzia hayo madini? Labda uniambie alikiuka mikataba yao ndio maana ikawa hivyo, mnakiuka miiko ya uongozi, uchaguzi baadae mnadingizia hewa.
 
Tume ya uchaguzi ilokuwa chini ya Nangaa ilimtangaza Tshisekedi kuwa ndiye mshindi kwa asilimia 38.56 na Martin Fayulu akishika nafasi ya pili kwa kupata asilimia 34 na wa tatu alikuwa Emmanuel Ramazani Shadary ambae alipata asilimia 23.

Fayulu alipinga matokeo hayo akisema Tshisekedi alikula njama na Kabila kuchakachua kura na akaenda kwenye mahakama ya Katiba ambako mapingamizi yake yalitupiliwa mbali.

Kanisa katoliki nalo lilitoa kauli kuonyesha mashaka yake juu ya uchaguzi huo.

Uchaguzi wenyewe ulipangwa ufanyike 2016 lakini Kabila akaanza kupiga danadana na ni shinikizo kutoka jumuiya ya kimataifa ndilo lilomfanya Kabila apange uchaguzi ufanyike mwaka 2017 na ukazogezwa tena hadi 2018 na hapo pia machine za kupigia zipatazo 8000 ziliungua moto ulotokea kwenye bohari za tume ya uchaguzi. Machine hizo ilikuwa ni mara ya kwanza zingetumika kweye uchaguzi nchini Congo DRC.

Makubaliano yalikuwa chama cha Kabila kimuunge mkono Chadary awe mgombea wao lakini Katumbi na Jean-Pierre Bemba wakapinga wakimtaka Martin Fayulu ndie awe mgombea.

Lakini hapohapo kuna mtu akaja na majina mfukoni na majina hayo yakawa Tshisekedi na Vital Kamerhe ambae angekuwa Waziri mkuu wa Tshisekedi.

Hivyo kulifanyika kitu chaitwa "double knock effect" kwanza majina yametoka mfukoni na pili, uchaguzi ukachakachuliwa.
Ilikuaje Nanga akubali kumtangaza mshindi, halafu leo aseme hakushinda aliiba kura?.
 
Tishekedi anaonekana mbaya na wezi wa Rwanda kwakuwa hatekelezi matakwa ya Rwanda na washirika wake
 
Back
Top Bottom