Ilikuwaje Nyerere akamshinda Sykes?

Ilikuwaje Nyerere akamshinda Sykes?

Ndugu huu ni ushauri pengine ni nje ya mada. Mgalatia mchukulie kama ndugu yako. Safari yetu ni moja tunamtafuta Mungu, tufike kwake tukiwa wakamilifu. Labda tumetofautiana usafiri tunaotumia lakini dhamira yetu ni moja.

Tunaamini katika Mungu, basi mtangulize yeye kwanza kwenye kila jambo. Dini isiwe sababu ya kumuona John ni kafiri, Jesca ni wa motoni. Kama dini fulani ingekua ndio tiketi ya kuiona pepo bila kuangalia uhalali wa matendo basi maisha yetu ya kiimani yangekuwa mepesi sana.

Sio lazima unijibu hili swali ila fanya hivi, Jirani yako hana dini na hajawahi kumkufuru Mungu kwa namna yoyote ile amekuwa akiishi katika matendo ya kupendeza, kusaidia maskini, haibi, hadhulumu, hasemi uongo nk..lakini ni hana dini.

Wewe unaamini dini yako ni ya haki na kweli unaswali swala tano sawa, lakini wewe ni mwizi, jambazi, mzinzi, unadhulumu yatima na Wajane nk lakini una dini na unaswali fresh tu.

Narudia tena sio lazima unijibu ila jiulize ni yupi ana nafasi mbele za Mungu? Kwamba atamchoma moto Jirani kwa kuwa hakuwa wa dini fulani na atakuchagua wewe kwa kuwa wa dini fulani?

Mwenyezi Mungu ameweka kitu ndani yetu, uwe una dini usiwe na dini, uwe unaamini Mungu uwe haumini ila unapotenda jambo jema unajua na unapotenda jambo baya unajua. Labda ndio tunda la mti wa mema na mabaya.

Unaweza kukutana na comments zangu kwenye mijadala mbalimbali hapa Jf hasa ya kidini ila sijawahi kumchukia mtu asiye wa imani yangu kwa namna yoyote ile. Nikimchukia Muislamu ni sawa na nimemchukia rafiki yangu wa toka utotoni, ni sawa nimewachukia Mama zangu wadogo, Dada zangu na wadogo zangu.

Nikiona kuna mtu anatumia dini kuhubiri chuki, anatumia dini kugawa watu huwa lazima nimjibu, japo sipendagi muendelezo naamini jibu langu moja au swali langu linatosha umeshindwa kubadilika basi Mungu awe pamoja nasi.

Leo unamuita Mgalatia, Kesho kafiri, kesho wanaajiri wao tu, wiki ijayo serikali inawapendelea yanaanza machafuko.
Mungu wetu ni wa wote, tujitahidi kupendana. Kukinzana mawazo kupotu lakini kusizae chuki. Kama wote wote tunatoa damu nyekundu, haijalishi rangi zetu, dini zetu. Basi sisi ni wa baba mmoja.
Wewe na huyo unaemjibu mnatofautiana katika tafsiri ya maana ya dini! ... dini kwako wewe ni kukiri imani sahihi ni ipi wakati huyo unayejadiliana nae kwake tafsiri ya dini ni mfumo wa maisha ya mwanadamu. So ukiangalia kimaana mnajadali vitu viwili tofauti kabisa katika jina moja, kamwe hamuwezi kufikia muafaka isipokuwa mtakwazana tu wakati kila mmoja yupo sahihi kulingana na mafundiso ya dini yake.

What you guys are missing (na hii ni mostly upande wa Christians) ni kuto-acknowledge na kutambua hoja za Waislamu dhidi ya mfumo kandamizi dhidi ya Uislamu uliotengenezwa kipindi cha awamu ya kwanza (nasema hivo kulingana na hoja zinazotajwa kuwa na uzito wa kustahili kusikilizwa). Hapa ni lazima mambo yajadiliwe kwa hoja na sio ushabiki.

Kufumbia macho manung'uniko ya upande mmoja ni kulea tatizo linalokuwa siku hadi siku.
 
Kulingana na mahojiano ya Tundu Lissu na mtangazaji wa ITV , Lissu alidai mara ya Mwisho CCM kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti kwa ushindani ilikuwa mwaka 1954 kati ya Julius Nyerere na Abdulwahid Sykes. Ambapo Nyerere alimbwaga Abdulwahid Sykes. Uchaguzi huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Anatoglou.

Swali la msingi ilikuwa ni kwamba ilikuwaje Nyerere amshinde Sykes ambaye alikuwa ni mtoto wa hapa Dar na baba yake alikuwa kiongozi wa TAA hapo kabla. Yani Nyerere kutoka Musoma aliwezaje kuwashawishi wajumbe wamchague yeye wamuache Sykes wa Dar.

Tusaidiane mbinu alizotumia Nyerere kushinda uchaguzi huo maana haikuwa rahisi.
Inawezekana Sykes alikuwa kilaza
 
Hilo haliwezekani,labda kwa watoto ambao hawajazaliwa bado ndiyo tuwaandalie mapito yasiyo na udini
Mapito haya ya udini yana chimbuko hayajatokea tu, na ukiangalia wenye malalamiko hawadai kufanyiwa favor bali wanalalamikia uonevu. So ni busara ku-address malalamiko yao katika kipimo cha sawasawa. Ikiwa kweli kuna makosa yalifanyika nyuma turekebishe coz sote hapa sio tuliofanya hayo makosa, na ikiwa malalamiko ni miss understanding tu basi tujadiliane kwa hekima mpaka wenye malalamiko wauone ukweli na waridhike.

Tukishindwa sisi tutegemee watoto wetu wawe katika hali mbaya zaidi. Sisi tuliozaliwa miaka ya 80s tumekuwa na kucheza pamoja bila kujali dini kwa kuwa wakati ule hatukujadili sana haya mambo, ni rahisi kabisa kukuta katika sisi mabest friends zetu ni wa dini tofauti sisi, lakini kwa sasa haya mambo yanavyojadiliwa na kuchukua hisia za watu kuna hatari watoto zetu ama wajukuu zetu wasiamiliane na wale wa imani tofauti na zao, na hapo tutakuwa pabaya sana kama taifa.
 
Kwa hivyo wale wazee wa Anatoglou waliokuwa wanapambana dhidi ya mwingereza walimchagua Nyerere kwa maelekezo ya mwingereza?. Nadhani umetoka nje ya mada.
Wasingepata uhuru ng'o bila ya kibaraka Nyerere
 
Kulingana na mahojiano ya Tundu Lissu na mtangazaji wa ITV , Lissu alidai mara ya Mwisho CCM kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti kwa ushindani ilikuwa mwaka 1954 kati ya Julius Nyerere na Abdulwahid Sykes. Ambapo Nyerere alimbwaga Abdulwahid Sykes. Uchaguzi huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Anatoglou.

Swali la msingi ilikuwa ni kwamba ilikuwaje Nyerere amshinde Sykes ambaye alikuwa ni mtoto wa hapa Dar na baba yake alikuwa kiongozi wa TAA hapo kabla. Yani Nyerere kutoka Musoma aliwezaje kuwashawishi wajumbe wamchague yeye wamuache Sykes wa Dar.

Tusaidiane mbinu alizotumia Nyerere kushinda uchaguzi huo maana haikuwa rahisi.

Hii ilikuwa kabla ya Ukabila, Udini na Ukanda .... Kushamiri.
 
Kura hazikupigwa nchi nzima kwa kuwa chama ndio kilikuwa kinaanza waliopiga kura ni wale waanzilishi 17 kuwa nani miongoni mwao awe rais wa TANU.Nyerere alikuwa msomi ndiye mtanganyika wa kwanza kuwa na Master degree hivyo waliona kwa usomi wake, ujengaji hoja ndiye angeweza kuwavusha.

Kingine ingawa wapiga kura wengi walikuwq waislamu lakini wakati ule hakukuwa na udini huu tunaouona leo. Ingekuwa leo hii na kama wapiga kura wengi wangekuwa waislamu asingepata. Ni kama Senegal nchi yenye waislamu asilimia 80 lakini rais wao wa kwanza alikuwa mkristo aliitwa Leopald Senghor lakini waliofuatia wote ni waislamu na haitatokea tena Senegal iwe na rais mkristo kwa sababu siku hizi Jamii imekuwa polarised.

Funzo hapa ni kuwa viongozi wanapohubiri ubaguzi iwe wa kidini, kijinsia, rika su ukabila wanapolarise Jamii hivyo lile kundi dogo kamwe haliwezi kutoa kiongozi.
Uchaguzi unaojadiliwa hapa ni wa TAA na siyo TANU.
 
Back
Top Bottom