Mtu anakuja kuwekeza unamuita beberuMkuu hii thread kuanzia kichwa tu umeandika upuuz. Hakuna sehemu Magufuli hakutaka kushirikiana na dunia. Swala ni maslai ya Tz mbele.Kuanza kufumua mikataba ya ovyo tayari ni kukataa kushirikiana na dunia?Kukataa Lockdown au Chanjo tayari hataki kushirikiana na dunia?
Hivi Rwanda ni duniaMmmmmh! Tulijitenga na dunia lini? Mbona tuliongea na Rwanda na Uganda kuhusu kuonganisha nchi zetu na (SGR). Mbona mkutano wa sadac ulifanyika Tanzania. Mbona balozi zetu hazikufungwa nchi jirani na duniani.Mbona wageni/watalii walifika nchini.Mbona viwanda vya wageni hususani ni waChina vimeongezeka.
Au kuwa karibu na dunia nikujenga bandari ya bagamoyo kwa masharti ya kipumbavu na kubinafsisha Tanesco. Au kusaini bogus treaty
Je umesema kuhusu leagal of nation je kwanini ujerumani aliona ni uboya akawageuka. Nakusuhu UN kwanini Patrice lumumba aliomba jeshi kutoka UN ili kuwaondoa wabelgiji wezi wa shaba congo baadala yake wanajeshi wa UN wakaanza kuwasupport wabelgiji. Huuu ndio uhusiano na dunia? jihusishe na dunia lakini chunga chako kwasababu hakuna wakutupa zaidi ya mungu lazima tuheshimu zawadi hii.
Nasikitika Sana mtoa maada umekuja na kapoint uchwara sijui ka diplomasia sijui naahisi ndo hicho ukijuacho kwenye maendeleo foreign policy hayo ni mambo ya mwisho maendeleo yanaanza ndani tengeneza mazingira ya ndani kwanza. Hizo nchi China na wenzake zimewin sio kwasababu ya blabla unazosema wewe ni kwa kufanya kazi kwa bidii na kutengeneza mazingira ya uwekazaji.
Hawezi kukujibu tena ongezea awataje ata watatu then atueleze walifanya yapi ao watatu?Yawezekana hujamwelewa Lumumba, yeye amejikita zaidi katika awamu ya tano...
Ndio maana naamini kabla na baada ya awamu ya tano, nyinyi wataalamu mlipewa nafasi na makafanya kazi
Swali langu, kabla na baada ya Magufuli mmeisaidiaje Tanzania katika vipengele alivyotaja Malcom?
Asante.
Hapa ndio kaulizaWatu hawakuwa wanaamini ule utapeli, bali ilikuwa ni shuruti. Na ilikuwa ukionyesha kwenda kinyume na ule utapeli unatekwa, kuuwawa au kubambikiwa kesi. Yaani tulipata kiongozi muovu, hisia zake akawa anatulazimisha tuziamini!
Tanzania itaendeleaje hata hatuna Uwekezaji kwenye technology..?Naamini Tanzania inaweza kuendelea bila kutegemea misaada bali ikabaki tu kuheshimiana na kushirikiana kwenye maendeleo...
Wakubwa wa dunia wanaamini kwenye umafia kwa kuendelea kufanya wengine masikini kwa kutumia baadhibya tools zai kila mahala..Wakubwa wadunia wakigundua una mtazamo tofauti wakuwatoa watu kwenye utumwa wa kiuchumi basi hutumia tools zao na vibaraka waliopandikizwa kila mahala kukumaliza..... WaAfrica tujaribu kuwa real na Uafrica wetu tusishupaze shingo na kubabaika sana na hawa pua ndefu....
Ben mkapa alifanya nchi yetu first class diplomacyHawezi kukujibu tena ongezea awataje ata watatu then atueleze walifanya yapi ao watatu?
Ayo majina hutokosa la January, Membe na Nape hapo ndo utajua kweli hatuna watu nchii hii
Sent using Jamii Forums mobile app
Nchi kama Singapore na Korea-Kaskazini ambazo ni ndogo kuliko Tanzania ziliwezake kuwa tajiri huku zikiendelea kushirikiana na mabeberu kama Marekani, Uingereza na Uchina ??? Lakini pia, ni lazima ufahamu kwamba kushambuliwa Muhammar Qhadaffy kuna historia ndefu sana. Hivi mnaikumbuka michezo yake lakini :Kuna njia ipi mbadala ambazo nchi za Afrika zitatumia kulinda masilahi yake? Huoni aliyoyapa Gadaffi? Labda utasaidie hata kidogo, nchi kama Tanzania itawezaje kulinda rasilimali zake kwa njia ya urafiki na mabeberu?
Hivi Nyakubonga kuna Raisi ambaye alifanikiwa kukuza uchumi wa Tanzania kwa kupitia Diplomasia kama Mzee Mkapa ??? Japo alikuwa na makosa yake mengi tu, lakini alitumia vizuri mtaji ulioachwa na Mzee Nyerere. Unakumbuka baada kwenda G8 nini kilitokea: Hivi unakumbuka uwekezaji ulivyokuwa nchini na madeni mengi ya nje kufutwa ???Malcom Lumumba naamini wewe ni mtaalamu mzuri wa diplomasia
Na mwana diplomasia kama wewe ni lazima utakua unawafahamu wajuvi wenzako wa diplomasia ndani ya nchi hii
Swali langu...
Tuambieni watanzania, utaalamu wenu wa diplomasia ulitusaidiaje kama nchi kujikomboa na janga la umasikini?(before&after magu, maana kwa mujibu wako huyu ni sufuri kwenye diplomacy)
Mpinge kwa hoja ndoo tutakuona mwanaume
Nakubaliana kabisa na wewe, lakini mkakati wa kujikwamua kutoka kwenye hiyo mifumo ya kibeberu ni ipi ???Ushirikiano ni muhimu sana. Lakini ushirikiano kwa namna ulivyo sasa hatutakuja kuendelea kamwe, tutabaki maskini siku zote. WTO wanahimiza soko huria, vikampuni toka nchi maskini vikashindane kwa usawa sokoni na makampuni makubwa ya matajiri. Hao IMF na WB wanalazimisha nchi zifuate sera za kichumi ambazo zinadumaza maendeleo ya nchi maskini. Sera ambazo nchi tajiri hazikuzitumia kujipatia maendeleo.
Hata nchi tajiri zenyewe mambo yakiziendea kombo zinaachana na makubaliano ya kimataifa. US kuipiga pin Huawei ni mfano mmoja wapo. Ushirikiano ni muhimu lakini kwa namna uliopo hautufai.
mkuu inawezekana jamaa kiukweli hakuwavizuri nyanja zote. Lakini isiwe sababu ya kuondoa sifa kubwa alizokua nazo kwa kuanza kumtukana na kuonesha jamaa alikuwa hatendi mazuri. Na pia tusitupilie macho yetu yote kwenye kitu kimoja Kama wewe unavyouweka uhusiano na dunia Kama ndio chanzo cha maendeleo ambacho jpm hufanya nakuona yale aliyo yafanya ni zero. Na pia umesema unatakiwa ujenge ndani na nje ni sahihi lakini sidhani Kama unaweza ukaanza na nje hafu ukafwata ya ndani ni wapuzi tu Hawa wa Sasa ndio mawazo yao. Lakini njia sahihi ni kuimalisha kwanza ya ndani ya nje huja yenyewe sio lazima uzunguke. hebu niambie Kama nyerere dam ambalo lilikuwa ndoto ya mda mrefu likikamilika litavutia wawekezaji wangapi? Naona umeitaja China na marekani kuwa ni maadui na pia Zinafanya biashara nikweli lakini uhusiano alionao China kwa mmarekani sio wakujipendekeza Kama wakwetu ambao mwisho ni unyonyaji mchina aliweka nchi yake Katika mazingira ya uwekazaji mmarekani akavutiwa kwa uwekeza japo walikuwa ni maadui na mbaka Sasa ni maadui lakini wanafanya biashara kutokana na uhitaji. Pia hata hapa kwetu Katika EAC hatukuwa vizuri na Kenya but Kenya wamenunua kwetu mazao kwasababu wanauhitaji. Kwa hiyo hii point yako ya kuangalia Sana uhusiano na dunia huku tukiwa mikono mitupu mm nadhani haiko sawa.Anhaa, kwahiyo mkuu unataka kusema kwamba sera ya mambo ya nje ya Tanzania ilitekelezwa ipasavyo kwasababu ya SGR, mkutano wa SADC, kuongezeka kwa viwanda vya wachina na watalii SI NDIYO ??? Lakini, vipi kuhusu utekelezaji wa International Commitments at Regional and International Levels ambazo tuliziweka kisiasa na zile ambazo ziko kisheria ???
Kuna matatizo mangapi ambayo nchi iliingizwa kwasababu za kutokuwa makini katika kuheshimu hizi international Commitments ??? Kuhusu mambo ya Bilateral Investment Treaties (BIT's) ni mara ngapi tulijiingiza kwenye shida zisizokuwa na ulazima kisa tu kiburi cha mtu mmoja ??? Haya ni baadhi ya mambo ambayo inabidi tuyazungumzie, lakini sioni mtu hata mmoja akiyaleta hapa.
Hakuna nchi inayolazimishwa kusaini mikataba endapo inahisi mikataba hiyo haina manufaa kwa taifa lake. Kila taifa ni Sovereign na Signin of Treaties falls within a scope of sovereign prerogatives. Pia hata kujitoa kwenye mikataba nayo ni Sovereign Prerogative, nchi inaweza kuamua kujitoa. Sisi tunachokataa ni kujitoa bila kuwa na mkakati, kudanganya umma au kutaka umaarufu.
Katika kusoma kwangu kote hata nchi kama Serikali za nchi kama Uingereza huwa hazishindi kesi dhidi ya wawekezaji endapo pale serikali imeamua kujitoa bila kufuata mkakati maalumu. Kama tunaikataa hii mikataba basi lazima tuje na mkakati na siyo kukurupuka hapa, mwishowe tunakuja kupata madhara kama yale yaliyotukuja kisa tulivunja baadha ya BIT kwa kukurupuka.
Daaah, hili swali huwa nilikuwa nakutana nalo kila nilipokuwa nafundisha International Law kwa wanafunzi wa mwaka wa pili. Ntakujibu kwa kufupi kabisa: International Relations cross-cuts many issues other than peace and security, it touches investment issues, health issues, international monetary systems, markets, culture etc.
Kilichotokea kwa Lumumba siyo kitu kuzuri hata kidogo, na kilidhihirisha udhaifu wa mfumo wetu wa dunia ambao uko mpaka leo hii. Lakini busara ni ipi, tuendelee kujitenga na kujificha au sisi kama bara la nchi masikini tuungane ili kusaidiana kubadilisha mifumo ya dunia ambayo inatukandamiza ??? Tanzania ilipoteza pesa nyingi sana katika kusaidia nchi za Afrika kupata Uhuru, lakini unafahamu faida za kiusalama ambazo nchi ilizipata kutokana na ule uwekezaji ???
Swali la msingi kijiuliza: Kikwete na Mkapa walifanikiwa sana kuendeleza hii tunu tulioachiwa na Baba wa Taifa. Je Raisi Magufuli alifanikiwa kufanya hivyo au alishindwa ???
Kaa chini fikiri.....
Dunia hii ya leo huwezi kutengeneza ya ndani bila kutengeneza ya nje pia, maana kila kitu ambacho kinakuja ndani ya nchi hutoka nje. Kiasilia, taifa ambalo huwa tajiri ni lile ambalo linafanikiwa sana kuuza bidhaa zake nje ya nchi kwa kiwango kikubwa, na lile ambalo linafanikiwa kuvutia mitaji ya nje kwa kupitia uwekezaji. Sasa ili ufanikiwe katika hili ni lazima uwe unafahamu fika mfumo mzima wa masoko ya dunia na michezo michafu ambayo mabeparu hucheza.
Nikikuuliza Sera ya uwekezaji na viwanda ya Tanzania kwa miaka mitano iliyopita ilikuwa ni ipi hutanijibu kabisa. Mkakati ambao ulitekelezwa vizuri ni ujenzi wa miundo mbinu, katika hili lazima tukubali kwamba Raisi Magufuli alijitahidi sana , lakini huko kwingineko hebu mnifundishe zaidi
Mkuu Asante kwa andiko lako, Kwanza nikupongeze kwa kutumia lugha halisi kwenye mazingira ya kiutafiti(ulioufanya)Huwa nawaza sana tulifikaje hapa tulipo leo,
Hivi ilikuwaje taifa lenye wasomi wazuri kabisa likaamua kufanya maamuzi ya kipumbavu ambayo hata Waroma wa kale walioishi miaka 2000 iliyopita wasingeyafanya. Hivi katika maksudi kabisa, taasisi nyeti za Tanzania ziliamini kabisa kwamba wao wangeweza kuifanya Tanzania nchi tajiri bila kushirikiana na dunia : Hivi ilikuwaje kabisa wataalamu wetu ambao wameenda shule, wanafahamu mifumo ya dunia ya kiuchumi, kiulinzi na kisiasa na wako kule USALAMA, BENKI KUU na MAMBO YA NJE wakakubaliana na huu upumbavu na kuanza kuutekeleza kabisa?
Mpangilio wa dunia yetu ya sasa uliwekewa msingi mwaka 1814 kule Vienna baada ya miaka 25 ya vita za mfalme Napoleon Bonaparte. Mwanamfalme Von Matternich alifahamu kabisa ili dunia isirudie kuingia kwenye songombingo la vita au kadhia yoyote ile, basi ni lazima watengeneze mfumo ambao uko kama utandu wa bui-bui: Kwamba maamuzi ya nchi moja yakifanyika lazima yaathiri nchi zote, hivyo nchi lazima zikubaliane kwenye baadhi ya mambo muhimu yanayowagusa wote. Ndiyo nadharia ya MZANI WA NGUVU (Balance of Power) ikazaliwa.
Mfumo wa dunia ya yetu hii tunayoishi leo hii umejengwa na matukio yaliyotokea miaka ya 1913, 1914, 1918, 1920, 1927, 1928, 1933, 1935, 1939, 1941, 1944, 1945, 1947, 1948, 1971 na 2001 . Kiufupi mlolongo wa matukio haya yafuatayo ndiyo yanatoa mwelekeo mzima wa mwenendo wa dunia yetu ya leo : Nashauri tufanya utafiti wa ndani kuhusu hili.
Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.
Mtaalamu yoyote yule wa Uchumi, Diplomasia, Ulinzi na Sheria ni lazima afahamu fika kuhusu haya ninayoyasema hapa. Kwamba dunia nzima tuko ndani ya utandu moja wa bui-bui. Huwezi kufanya jambo lolote lile ukiwa nje ya hapo. Ndani ya huu utandu wa bui-bui kuna kila aina ya watu: Wema na wabaya, Huru na watumwa, Masikini na tajiri, Wenye matumaini na wasio na matumaini, Wababe na dhaifu na Waamini Mungu na Maadui wa Mungu.
Huu ndiyo mfumo wa dunia (The World Order), huwezi kufanya maajabu yoyote yale ukiwa nje: Hata mataifa makubwa yenye nguvu duniani yanaheshimu huu mfumo kwasababu yanafahamu siku mfumo huu unaharibika basi ndiyo utakuwa mwisho wao. Hivyo kuna baadhi ya sheria hata yenyewe yatazifuata tu kwasababu zina manufaa kwao. Mwandishi George Orwell kwenye The ANIMAL FARM aliwahi kusema "All animals are equal, but some are more equal than others" hivyo hata kama tunataka usawa kuna wale waliotutangulia watakuwa mbele yetu kwenye baadhi ya mambo tu.
Sasa kinachoumiza wasomi wa Tanzania wenye PhD za sheria, uchumi na diplomasia. Huku wengine wakiwa na shahada kwenye masomo ya ulinzi, usalama na sayansi za vita wakiwa na akili timamu kabisa, wakaamua kuwa wapumbavu. Wakatundika elimu zao nyuma ya milango na kuanza kutekeleza jambo ambalo hata watu wa kale walioishi miaka 2000 hawakuwahi kuliwaza. Tanzania ina matatizo mengi, lakini ilikuwa inarekebishika vizuri tu kwasababu waliofikisha nchi yetu hapa wanafahamika na tunakula na kunywa nao kila siku.
Kuanza kulaumu mabeberu peke yake haisaidii kwasababu kuna wenzetu ambao wamefanikiwa kutumia mifumo hii-hii ya mabeberu kuwashinda mabeberu kiuchumi, kiulinzi na kisiasa. Ukweli ni kwamba huu mfumo umejengwa na mabeberu lakini hata walioujenga hawaundeshi wanavyotaka wao. Mataifa ya Magharibi ndiyo waanzilishi wa World Trade Organization (WTO) lakini leo hii, WTO imemnufaisha Uchina kuliko tangu alivyojiunga nao mwaka 2001 na mpaka sasa wanajutia kumkaribisha.
Nchi kama Singapore, India, Korea-Kusini na Brazil wamewezaje kucheza vizuri kwenye huu mfumo wa mabeberu hadi kufikia kuwango cha kuwashinda mabeberu kwenye baadhi ya mambo ??? Inahitaji akili ya ziada kutoka kwa Mungu ili kuweza kucheza kwenye huu mfumo. Raisi Donald Trump alijaribu kuitoa Marekani kwenye huu mfumo wa Vienna, lakini pamoja na maguvu yote ya Marekani alifanikiwa ???
Lakini leo hii kuna watu wako ndani ya IDARA ZA USALAMA ZA TANZANIA waliamini kabisa kwamba Tanzania inaweza kujitenga na dunia bila kupata madhara. Yaani waliamini kabisa na wengine bado wanaamini kabisa. Kuna wengine bado wanaamini kwamba mfumo wa Kileninisti na Kimaksisti (Marxist-Leninism) unaweza kutumika kuikomboa Tanzania. Sawa, lakini hata walioutuletea huu mfumo Warusi na Wachina, wamebadilisha sana baadhi ya hizi falsafa.
Dunia ya nchi moja kutawala wengine (Uni-Polar World) au nchi mbili kuamulia dunia nini kifanyike (Bi-Polar World) unakufa taratibu, ndiyo maana Marekani na Urusi wanapata shida kukubaliana na huu ukweli. Wao kama mataifa hawaanguki na bado wana nguvu, ila tu ni kwamba mataifa yale madogo na masikini kama Vietnam, Poland, Mexico yamekuwa makubwa yenye uchumi unaokua kwa kasi sana.
Tanzania tuliachiwa mtaji mkubwa sana kidiplomasia, ambao ulitujengea SOFT-POWER na INFLUENCE ambayo ilifanikisha ulinzi na usalama wa Tanzania kikanda na kidunia kwa kiwango kikubwa sana. Tuliingia sehemu ambazo hata nchi kubwa hazikuweza kuingia, tulipata taarifa nyeti kabla hata baadhi ya mataifa makubwa hayajazipata, tulipewa heshima ya kipekee (Special Treatment) ambayo mataifa mengine yenye uchumi mkubwa kuliko sisi barani Afrika hayakupewa.
Tuliogelea bwawa moja na mababeru, wakomunisti, wajahidina na wazayuni lakini tulitoka salama, kesho tena tukarudi kuogelea. We were a Shrimp among Whales, lakini bado tuliheshimika mno. Lakini leo hii hebu angalia, ile nguvu yote ambayo Mzee Nyerere na Raisi Mkapa walitutengenezea, imemomonyoka kisa kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uelewa mpana wa mahitaji ya nchi yetu na nafasi yetu hapa ulimwenguni.
Binafsi naamini ili tuweze kutoka hapa tulipo ni lazima NYUMBA ISAFISHWE aidha mbele ya majirani au kisiri. Mambo ya UHAINI, KUHODHI MADARAKA, KUPANGA KUUA MARAISI WASTAAFU,KUSHIRIKIANA NA MAADUI WA TAIFA na KUWINDANA KWA KUTUMIA MAKUNDI NDANI YA TASISI ZA KIUSALAMA (Cloack and Dagger Diplomacy) tulikuwa tunayasikia nchi jirani tu: Kwetu sisi yalikuwa ni MWIKO KABISA. Vitendo vya kihaini tulishaachana navyo awamu ya kwanza. Lakini leo kuna kakundi kalifikiri kabisa kangeweza kutupangia sisi Watanzania nani awe Mkuu wa nchi kweli?
Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).
Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....
Sijawahi kubadilisha msimamo wangu kuhusu Raisi Magufuli kwasababu naamini katika kweli, lakini pia nina miiko yangu ya maisha ambayo ndiyo mwongozo wangu. Lakini kikubwa ni kwamba nilianza kuwa adui wa watu wengi humu ndani baada ya kuanza kukosoa aina ya utawala wa Magufuli: Hivyo bila hata kufanya rejea kama bwana Mayalla I'M AN OUTCAST and I MUST ADMIT I LOVE THIS MONIKER,........Mimi hasa ningependa kufahamu mtazamo wako binafsi kuhusu utawala wa Magufuli ulikuwaje na ukoje hivi sasa? Unaweza kurejea michango yako hapa JF kama afanyavyo Pascal Mayalla.
Nakubaliana kabisa na wewe, lazima Afrika tujifunze kujitegemea na naamini kabisa hili tunaliweza.Naamini Tanzania inaweza kuendelea bila kutegemea misaada bali ikabaki tu kuheshimiana na kushirikiana kwenye maendeleo...
Wakubwa wa dunia wanaamini kwenye umafia kwa kuendelea kufanya wengine masikini kwa kutumia baadhibya tools zai kila mahala..Wakubwa wadunia wakigundua una mtazamo tofauti wakuwatoa watu kwenye utumwa wa kiuchumi basi hutumia tools zao na vibaraka waliopandikizwa kila mahala kukumaliza..... WaAfrica tujaribu kuwa real na Uafrica wetu tusishupaze shingo na kubabaika sana na hawa pua ndefu....
Mimi Malcom Lumumba nitasema ukweli daima, fitna kwangu mwiko. Raisi Magufuli kuna mambo mengi sana aliyafanya vizuri lakini mambo ya nje na diplomasia haviko kwenye hiyo orodha. Dunia yetu ya leo siyo ile ya karne ya 18 na 19 ambayo ulikuwa unaweza kujifungia tu (Isolationism) halafu mambo yakawa yanaenda tu. Tunaishi kwenye ulimwengu wa utandawazi, hivyo ni lazima tunavyojenga ndani na nje tujenge: Lazima kuwe na uwiano mzuri......mkuu inawezekana jamaa kiukweli hakuwavizuri nyanja zote. Lakini isiwe sababu ya kuondoa sifa kubwa alizokua nazo kwa kuanza kumtukana na kuonesha jamaa alikuwa hatendi mazuri. Na pia tusitupilie macho yetu yote kwenye kitu kimoja Kama wewe unavyouweka uhusiano na dunia Kama ndio chanzo cha maendeleo ambacho jpm hufanya nakuona yale aliyo yafanya ni zero. Na pia umesema unatakiwa ujenge ndani na nje ni sahihi lakini sidhani Kama unaweza ukaanza na nje hafu ukafwata ya ndani ni wapuzi tu Hawa wa Sasa ndio mawazo yao. Lakini njia sahihi ni kuimalisha kwanza ya ndani ya nje huja yenyewe sio lazima uzunguke. hebu niambie Kama nyerere dam ambalo lilikuwa ndoto ya mda mrefu likikamilika litavutia wawekezaji wangapi? Naona umeitaja China na marekani kuwa ni maadui na pia Zinafanya biashara nikweli lakini uhusiano alionao China kwa mmarekani sio wakujipendekeza Kama wakwetu ambao mwisho ni unyonyaji mchina aliweka nchi yake Katika mazingira ya uwekazaji mmarekani akavutiwa kwa uwekeza japo walikuwa ni maadui na mbaka Sasa ni maadui lakini wanafanya biashara kutokana na uhitaji. Pia hata hapa kwetu Katika EAC hatukuwa vizuri na Kenya but Kenya wamenunua kwetu mazao kwasababu wanauhitaji. Kwa hiyo hii point yako ya kuangalia Sana uhusiano na dunia huku tukiwa mikono mitupu mm nadhani haiko sawa.
Nakubaliana kabisa na wewe, lazima tulinde rasilimali zetu kwa WIVU MKUBWA, lakini siyo kutumia ile njia ambayo kipenzi chenu alikuwa anaitumia. Amevuruga mambo na itifikati katika kiwango kikubwa sana,.....
Anhaa bwana Grinch upo,......???amevuruga kitu gani!!!
mtu mpumbavu akikusoma anawezasema uko timamu kumbe unaumwa kichwa.
unalalamika watu kuchukia mama kusafiri,tukuulize ushirikiano ni kusafiri peke yake!!mtu yuko hewani akirudi makamu karuka lakini umeme na maji hakuna huku.
Unajua ni kwa nini Nyerere alikuwa reluctant kufungulia uchimbaji holela wa madini?Yaani huu unyonyaji dhidi ya Tanzania uanze tu awamu ya tano ???
Mjamaa Nyerere mbona alishirikiana sana na dunia ???
Alikuwa haogopi kunyonywa ???