Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Sasa hoja ya pili kwamba nchi imeingia kubaya, sijui unazungumzia awamu ipi ila Kama ya JPM, hapana, maana Mwamba alitaka kuifanya nchi kujitegemea, kuwa sawa na kujari masilahi ya wananchi, hebu twende kwa mifano mkuu, nchi yetu ndo Kwanza tunaawamu ya 6 yaan tunarais wa 6, tukiwa tunamiak 60 ya Uhuru,je can we compared na nchi USA?? Ambayo inarais wa 47?? Inamiaka zaidi takriban 100+ ya Uhuru?? Je democracy ya kwetu inaweza kuwa sawa na wao??

Mkuu, huwezi kuwa masikini ukacompite na tajiri, hapana[emoji15][emoji15] unachotakiwa Ni kuwa na akili ili ujikwamue kutoka hapo, na ndicho alichokuwa anakifanya Mwamba,

Sasa tatzo lilikuja wapi?? Ni kwenye mifumo, baada ya JPM kulala, kwa kuwa hatuna mpango wa maendeleo wa mda mrefu, (tuseme miaka 15-30) miladi yote ambayo iliibuliwa na miongozo yote, inawekwa kando taratb lakini kwa uhakika, Nini kinafuata, tunarudi nyuma kwa kasi ya ajabu kubwa na kwa sabab hatuna vision, and planning, for the long term, tunapiga maketime au kurud nyuma,

I
Umeongea vizuri sana na kwa utulivu, lakini na wewe naona uko gizani kama wengine. Kujitenga na dunia siyo lazima useme hadharani kwamba hutaki kushirikiana na dunia, au uamue kuvunja mahusiano ya kidiplomasia. Unaweza ukawa bado uko kwenye mahusiano na wenzako lakini hutui ushirikiano wa kutosha na unafanya mambo kinyume na utaratibu uliokubalika.

Raisi Magufuli aliliingiza taifa kwenye giza nene kwasababu zisizokuwa za msingi, KIBURI, JEHURI, HADAA, MABAVU na UJUAJI. Hivi unadhani kulikuwa na ulazima wowote wa kuzuia ndege zetu zisiruke nje ya nchi yetu ??? Moja ya sababu ya ndege kutoruka na kuogopa kukamatwa kwasababu ya madeni yalitokana na sisi kutoheshimu baadhi ya mikataba ya kimataifa ya uwekezaji (Bilateral Investment Treaties- BIT's).

Sasa kukupasha tu, kule chini maneno ya Mtwara kuna muitalia alipewa ardhi kwa ajili ya uwekezaji. Tanzania na Italy tulisaini BIT. Moja ya kanuni kubwa kabisa kwenye BIT ni Rule Against Expropriation and The Most Favoured National. Ikatokea vijana wa Magufuli wakiwa wamepewa amri kwamba wanyang'anye ardhi ambayo haijaendelezwa, kumbe kuna utaratibu wao wakanyang'anya.

Sasa jamaa akapeleka kesi kwenye mahakama za kimataifa akawa anavizia mali zetu: Lakini ukweli ni kwamba Mzee alishauriwa afuate utaratibu lakini alipuuza kwa madaha. USALAMA WA TAIFA wakamshauri sasa amualike jamaa aje Tanzania ili wakubaliane, kumbe jamaa walikuwa wanataka akifika tu wamkamate na kumtandika kesi za kutosha. Jamaa akawa mjanja akitoa masharti wakutane naye nje ya nchi.

Hebu tafuta kesi ya SUNLODGES V Tanzania (Expropriation Case) maana nimeona wewe walau una akili kuliko hawa vijana wengine ambao kazi yao ni kupiga vigelegele ilhali hawafamu kitu.....

Sasa hii ni akili ya wapi kweli, hivi idara za USALAMA WA TAIFA hali zikifahamu kwamba mikataba imesainiwa na nji na kuna utaratibu wa kujitoa. Kwanini wasaidie utekelezaji wa mambo ambayo mpaka sasa yamekuwa na madhara makubwa kwa taifa letu ???
 
Hivi Nyakubonga kuna Raisi ambaye alifanikiwa kukuza uchumi wa Tanzania kwa kupitia Diplomasia kama Mzee Mkapa ??? Japo alikuwa na makosa yake mengi tu, lakini alitumia vizuri mtaji ulioachwa na Mzee Nyerere. Unakumbuka baada kwenda G8 nini kilitokea: Hivi unakumbuka uwekezaji ulivyokuwa nchini na madeni mengi ya nje kufutwa ???

Tena naona mnasahau kuhusu changamoto za kiusalama zilizokuwepo huu ukanda wetu mnamo miaka ya 1995-2003, nchi nyingi ziliingia kwenye matatizo makubwa lakini unafahamu kwanini Tanzania ilitoka salama ??? Tanzania ilikuwa inaangaliwa katika jicho la kipekee sana linapokuja suala zima la siasa za Afrika. Leo hii nini kimetokea ??? Binafis siamini kabisa kama Tanzania ina msuli ule iliyokuwa nao miaka hiyo......

Halafu leo Raisi Magufuli alitaka kutuaminisha kwamba hawa watangulizi wake hawakufanya chochote wala lolote kwa nchi hii: Ilhali mifumo yote ambayo ilimfanikisha hata yeye kuvuruga nchi yetu ameikuta imejengwa na wao. Sisi kama nchi bado tuna safari ndefu sana, lakini njia na mbinu za watu kama Magufuli ni hatari mno na zimeturudisha nyuma miaka 25. Kurudi kwenye ile nafasi yetu, inawezekana lakini itachukua muda sana na nguvu ya ziada.

NB: Mimi ninachouliza iliwezekanaje nchi ikawa ikavurugwa hivi, ilhali kuna taasisi nyeti zenye wasomi na wataalamu ambao walikuwa wanafahamu fika nchi ilikotoka. Kwanini washiriki utekelezaji wa mauti ya taifa letu halafu leo hii wanaachwa bila hata kupigwa kitanzi au kunyongwa kwa uhaini ili wapuuzi wengine wasidiriki kabisa kurudia jambo kama hili ???
Mkapa alikuza uchumi na kusamehewa madeni lakini kumbuka acacia wameingia kipindi chake hakukua na mgodi mkubwa tofauti Williamson diamond mine
 
Unajua ni kwa nini Nyerere alikuwa reluctant kufungulia uchimbaji holela wa madini?
Alikuwa ana akilizi za ziada kuliko maraisa wote wa Tanzania, lakini pia Tanzania lilikuwa ni taifa changa bado.

Alikataa kuruhusu madini yachimbwe hili linakubalika, lakini alifuata kanuni na taratibu za dunia na sheria za kimataifa: Tena alifanya kabisa majadiliano na ushirikiano hata na watu ambao alikuwa hakubaliani nao. Ndiyo Tanzania ilifanikiwa sana kwenye nyanja nzima ya Kidiplomasia......
 
Nakubaliana kabisa na wewe, lakini mkakati wa kujikwamua kutoka kwenye hiyo mifumo ya kibeberu ni ipi ???
Unaufahamu mchezo wa CHESS ??? Siku zote anayemshinda ni yule mwenye kusoma vizuri na kutabiri hatua za adui.
Niliipata point yako mkuu. Tunatakiwa kujikwamua kwa akili na tahadhari ya hali ya juu. Si kwa makelele na vurugu kama walivyokuwa wanafanya watu tuliowaamini kuwa wana uelewa mkubwa wa mambo.
 
Hakuna ambae hakutaka kushirikiana na nchi nyingine ila kushirikiana kwa kutunyonya hilo ndo tulikataa awamu ya tano na inatakiwa iwe hivo kwa nchi zote za Africa gasa kusini mwa jangwa la sahara! Ile mikata ya kusaini mi nakuletea kandamili ww nipe Tanzanite hatuitaki

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwendazake ameifilisi Tibisii na kundi lake
 
I believe 'diplomacy is an art of compromise'
My maan, my maaan! You have made my day.
Tungekuwa jirani ningekununulia hata kawaha ndugu yangu, umezungumza nilichokuwa nakitafuta humu ndani.

DIPLOMACY is an art of maintaining communication and relations among nations. It also includes virtues like compromise, reciprocity, consensus, consent and good-faith. Babu Nyerere was a master of this, that's why he left us a hefty fortune of diplomatic clout.

Raisi Magufuli and his cronies were unstable, dangerous and volatile, ameacha madhara makubwa mno kwa nchi, lakini kuna watu bado hawataki kukubali ukweli ambao uko wazi.....
 
Jakaya Kikwete naye alikosea na tukamsema, uzuri alikuwa ni mtu ambaye anapenda kusikiliza ushauri wa kitaalamu, kufuata kanuni taratibu na aliheshimu sheria za kimataifa: Ndiyo maana hata aliposhindana na baadhi ya mataifa alikuwa kwenye upande salama kwasababu alifahamu fika kwamba hakuna nchi inayoweza kuendelea duniani bila diplomasia.

Sasa Raisi Magufuli tukisema kwamba alikuwa haheshimu kanuni na taratibu, na alikuwa ni mtu ambaye hataki ushauri hata kwenye mambo nyeti mbona mnakasirika wakati ushahidi uko mwingi tu. Mimi ninayezungumza na wewe nakwambia ukweli kwa yake ambaye nimeyaona kama mwanasheria. Nimekaa na watu ambao ni walikuwa washahuri wa karibu wa Raisi Magufuli, na wanasema kweli alivurunda. Mengine hatuwezi kuyaweka wazi tu,....

Nikuulize labda hivi unafahamu kwanini tulikuwa tunawinda sana na mabeberi hadi wakakamata ndege zetu, ambazo tukawa tunaogopa hata zisiruke nje ??? Tanzania tuna Bilateral Investment Agreements (BIT's) na nchi zisizopungua 30. Sasa Raisi Magufuli hali akifahamu kwamba kuna utaratibu maalumu wa kufuata unapotaka kuwashughulikia mabeberu, yeye akaamua kufanya kama anavyoshughulika na BAVICHA.

Nchi ikawa inaingia kwenye taharuki zisizo na msingi kisa tabia yake ya kutopenda kusikiliza na kujifanya anajua kila kitu. AU haya nayo umeyasahau mkuu ???
Ni kama nakuelewa brother, lakini tukimjudge Magufuli kwa kuangalia angle moja tutakuta hakuna alichokifanya

Kitu ambacho kwa maoni yangu, si kweli.
 
Umeegemea kwenye point ya mwisho kabisa, na hayo mawazo yako ni yakimaskini na kutokujiamini. Baadala ya kuchakata kichwa tunafanyaje na rasilimali zetu. Unakimbilia kujihusisha na dunia ndo wewe utakuja kutusainisha Hadi ushoga ili upate misaada
Mkuu, mbona tumejadiliana vizuri tu tokea mwanzo na sijakutuhumu wala kukukashifu kwa chochote kile mkuu. Kwanini uanze kunitolee kashfa mbaya kama hizi ilhali mimi sijakutenda chochote ???
 
Huwa nawaza sana tulifikaje hapa tulipo leo,

Hivi ilikuwaje taifa lenye wasomi wazuri kabisa likaamua kufanya maamuzi ya kipumbavu ambayo hata Waroma wa kale walioishi miaka 2000 iliyopita wasingeyafanya. Hivi katika maksudi kabisa, taasisi nyeti za Tanzania ziliamini kabisa kwamba wao wangeweza kuifanya Tanzania nchi tajiri bila kushirikiana na dunia : Hivi ilikuwaje kabisa wataalamu wetu ambao wameenda shule, wanafahamu mifumo ya dunia ya kiuchumi, kiulinzi na kisiasa na wako kule USALAMA, BENKI KUU na MAMBO YA NJE wakakubaliana na huu upumbavu na kuanza kuutekeleza kabisa?

Mpangilio wa dunia yetu ya sasa uliwekewa msingi mwaka 1814 kule Vienna baada ya miaka 25 ya vita za mfalme Napoleon Bonaparte. Mwanamfalme Von Matternich alifahamu kabisa ili dunia isirudie kuingia kwenye songombingo la vita au kadhia yoyote ile, basi ni lazima watengeneze mfumo ambao uko kama utandu wa bui-bui: Kwamba maamuzi ya nchi moja yakifanyika lazima yaathiri nchi zote, hivyo nchi lazima zikubaliane kwenye baadhi ya mambo muhimu yanayowagusa wote. Ndiyo nadharia ya MZANI WA NGUVU (Balance of Power) ikazaliwa.

Mfumo wa dunia ya yetu hii tunayoishi leo hii umejengwa na matukio yaliyotokea miaka ya 1913, 1914, 1918, 1920, 1927, 1928, 1933, 1935, 1939, 1941, 1944, 1945, 1947, 1948, 1971 na 2001 . Kiufupi mlolongo wa matukio haya yafuatayo ndiyo yanatoa mwelekeo mzima wa mwenendo wa dunia yetu ya leo : Nashauri tufanya utafiti wa ndani kuhusu hili.

Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.

Mtaalamu yoyote yule wa Uchumi, Diplomasia, Ulinzi na Sheria ni lazima afahamu fika kuhusu haya ninayoyasema hapa. Kwamba dunia nzima tuko ndani ya utandu moja wa bui-bui. Huwezi kufanya jambo lolote lile ukiwa nje ya hapo. Ndani ya huu utandu wa bui-bui kuna kila aina ya watu: Wema na wabaya, Huru na watumwa, Masikini na tajiri, Wenye matumaini na wasio na matumaini, Wababe na dhaifu na Waamini Mungu na Maadui wa Mungu.

Huu ndiyo mfumo wa dunia (The World Order), huwezi kufanya maajabu yoyote yale ukiwa nje: Hata mataifa makubwa yenye nguvu duniani yanaheshimu huu mfumo kwasababu yanafahamu siku mfumo huu unaharibika basi ndiyo utakuwa mwisho wao. Hivyo kuna baadhi ya sheria hata yenyewe yatazifuata tu kwasababu zina manufaa kwao. Mwandishi George Orwell kwenye The ANIMAL FARM aliwahi kusema "All animals are equal, but some are more equal than others" hivyo hata kama tunataka usawa kuna wale waliotutangulia watakuwa mbele yetu kwenye baadhi ya mambo tu.

Sasa kinachoumiza wasomi wa Tanzania wenye PhD za sheria, uchumi na diplomasia. Huku wengine wakiwa na shahada kwenye masomo ya ulinzi, usalama na sayansi za vita wakiwa na akili timamu kabisa, wakaamua kuwa wapumbavu. Wakatundika elimu zao nyuma ya milango na kuanza kutekeleza jambo ambalo hata watu wa kale walioishi miaka 2000 hawakuwahi kuliwaza. Tanzania ina matatizo mengi, lakini ilikuwa inarekebishika vizuri tu kwasababu waliofikisha nchi yetu hapa wanafahamika na tunakula na kunywa nao kila siku.

Kuanza kulaumu mabeberu peke yake haisaidii kwasababu kuna wenzetu ambao wamefanikiwa kutumia mifumo hii-hii ya mabeberu kuwashinda mabeberu kiuchumi, kiulinzi na kisiasa. Ukweli ni kwamba huu mfumo umejengwa na mabeberu lakini hata walioujenga hawaundeshi wanavyotaka wao. Mataifa ya Magharibi ndiyo waanzilishi wa World Trade Organization (WTO) lakini leo hii, WTO imemnufaisha Uchina kuliko tangu alivyojiunga nao mwaka 2001 na mpaka sasa wanajutia kumkaribisha.

Nchi kama Singapore, India, Korea-Kusini na Brazil wamewezaje kucheza vizuri kwenye huu mfumo wa mabeberu hadi kufikia kuwango cha kuwashinda mabeberu kwenye baadhi ya mambo ??? Inahitaji akili ya ziada kutoka kwa Mungu ili kuweza kucheza kwenye huu mfumo. Raisi Donald Trump alijaribu kuitoa Marekani kwenye huu mfumo wa Vienna, lakini pamoja na maguvu yote ya Marekani alifanikiwa ???

Lakini leo hii kuna watu wako ndani ya IDARA ZA USALAMA ZA TANZANIA waliamini kabisa kwamba Tanzania inaweza kujitenga na dunia bila kupata madhara. Yaani waliamini kabisa na wengine bado wanaamini kabisa. Kuna wengine bado wanaamini kwamba mfumo wa Kileninisti na Kimaksisti (Marxist-Leninism) unaweza kutumika kuikomboa Tanzania. Sawa, lakini hata walioutuletea huu mfumo Warusi na Wachina, wamebadilisha sana baadhi ya hizi falsafa.

Dunia ya nchi moja kutawala wengine (Uni-Polar World) au nchi mbili kuamulia dunia nini kifanyike (Bi-Polar World) unakufa taratibu, ndiyo maana Marekani na Urusi wanapata shida kukubaliana na huu ukweli. Wao kama mataifa hawaanguki na bado wana nguvu, ila tu ni kwamba mataifa yale madogo na masikini kama Vietnam, Poland, Mexico yamekuwa makubwa yenye uchumi unaokua kwa kasi sana.

Tanzania tuliachiwa mtaji mkubwa sana kidiplomasia, ambao ulitujengea SOFT-POWER na INFLUENCE ambayo ilifanikisha ulinzi na usalama wa Tanzania kikanda na kidunia kwa kiwango kikubwa sana. Tuliingia sehemu ambazo hata nchi kubwa hazikuweza kuingia, tulipata taarifa nyeti kabla hata baadhi ya mataifa makubwa hayajazipata, tulipewa heshima ya kipekee (Special Treatment) ambayo mataifa mengine yenye uchumi mkubwa kuliko sisi barani Afrika hayakupewa.

Tuliogelea bwawa moja na mababeru, wakomunisti, wajahidina na wazayuni lakini tulitoka salama, kesho tena tukarudi kuogelea. We were a Shrimp among Whales, lakini bado tuliheshimika mno. Lakini leo hii hebu angalia, ile nguvu yote ambayo Mzee Nyerere na Raisi Mkapa walitutengenezea, imemomonyoka kisa kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uelewa mpana wa mahitaji ya nchi yetu na nafasi yetu hapa ulimwenguni.

Binafsi naamini ili tuweze kutoka hapa tulipo ni lazima NYUMBA ISAFISHWE aidha mbele ya majirani au kisiri. Mambo ya UHAINI, KUHODHI MADARAKA, KUPANGA KUUA MARAISI WASTAAFU,KUSHIRIKIANA NA MAADUI WA TAIFA na KUWINDANA KWA KUTUMIA MAKUNDI NDANI YA TASISI ZA KIUSALAMA (Cloack and Dagger Diplomacy) tulikuwa tunayasikia nchi jirani tu: Kwetu sisi yalikuwa ni MWIKO KABISA. Vitendo vya kihaini tulishaachana navyo awamu ya kwanza. Lakini leo kuna kakundi kalifikiri kabisa kangeweza kutupangia sisi Watanzania nani awe Mkuu wa nchi kweli?

Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).

Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....
Mwendazake tu acha kusingizia watanzania wote
 
Jakaya Kikwete naye alikosea na tukamsema, uzuri alikuwa ni mtu ambaye anapenda kusikiliza ushauri wa kitaalamu, kufuata kanuni taratibu na aliheshimu sheria za kimataifa: Ndiyo maana hata aliposhindana na baadhi ya mataifa alikuwa kwenye upande salama kwasababu alifahamu fika kwamba hakuna nchi inayoweza kuendelea duniani bila diplomasia.

Sasa Raisi Magufuli tukisema kwamba alikuwa haheshimu kanuni na taratibu, na alikuwa ni mtu ambaye hataki ushauri hata kwenye mambo nyeti mbona mnakasirika wakati ushahidi uko mwingi tu. Mimi ninayezungumza na wewe nakwambia ukweli kwa yake ambaye nimeyaona kama mwanasheria. Nimekaa na watu ambao ni walikuwa washahuri wa karibu wa Raisi Magufuli, na wanasema kweli alivurunda. Mengine hatuwezi kuyaweka wazi tu,....

Nikuulize labda hivi unafahamu kwanini tulikuwa tunawinda sana na mabeberi hadi wakakamata ndege zetu, ambazo tukawa tunaogopa hata zisiruke nje ??? Tanzania tuna Bilateral Investment Agreements (BIT's) na nchi zisizopungua 30. Sasa Raisi Magufuli hali akifahamu kwamba kuna utaratibu maalumu wa kufuata unapotaka kuwashughulikia mabeberu, yeye akaamua kufanya kama anavyoshughulika na BAVICHA.

Nchi ikawa inaingia kwenye taharuki zisizo na msingi kisa tabia yake ya kutopenda kusikiliza na kujifanya anajua kila kitu. AU haya nayo umeyasahau mkuu ???
Sasa Kama kikwete naye kakosea, magu kakosea tuchukue kipi Sasa. Kama kikwete aliweka diplomasia na uhusiano ikawa hola haya magu kajisolate kajipigapiga tumefika hapa tulipo hafu unasema tumerudi 25 years nyuma Tena.
 
Ndugu yangu Malcom, in all honesty, taja machache (notable) kati ya hayo mengi sana Magufuli aliyofanya vizuri.
  • Ujenzi wa miondombinu mikubwa ya kimkakati.
  • Uandishi mkubwa wa marudio ya sheria za nchi.
  • Kurudisha nidhamu ya kazi kwenye utumishi wa umma.
  • Kuwapa nafasi za uongozi vijana na wanawake.
  • Kuimarisha (Syncronization) mfumo wa ukusanyaji mapato ya serikali (GEPG)
Sasa njia zilizotumika kufanikisha haya ni suala jingine ambalo linahitaji mada yake, lakini katika haya nasema mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni. Japo ukweli utabaki kwamba alivurunda kwenye mambo mengi tu nyeti na ya msingi, kiasi ambacho kilihatarisha na kufunika haya mafanikio yake.
 
Ni kama nakuelewa brother, lakini tukimjudge Magufuli kwa kuangalia angle moja tutakuta hakuna alichokifanya

Kitu ambacho kwa maoni yangu, si kweli.
Nakubaliana kabisa na wewe, hatutakiwi kumhukumu mwanadamu katika upande mmoja. Kuna mambo mazuri sana Raisi Magufuli ameifanyia nchi: Japo lengo la huu uzi ni kutaka kufahamu kwanini wale wataalamu kutoka TISS, JWTZ, Foreign Affairs, BoT na Ministry of Finance waliamua kuunga mkono na kufanikisha mambo ya hovyo yaliyokuwa yanafanywa na Raisi Magufuli ilhali wao wanafahamu fika mfumo wa dunia ulivyo na mahitaji ya nchi yetu ???

Ilikuwaje watu wataalamu wa Uchumi, Sheria, Diplomasia na Ulinzi wakaamua kuicha nchi itumbukie kwenye korongo refu ambalo tunahangaika kutoka mpaka sasa ??? Kwanini hawakuchuliwa hatua pale walipotaka kufanya vitendo vya kihaini baada ya Raisi kufariki ??? Kwanini bado wanaendelea kulelewa huku wakizidi kulihadaa taifa ???
 
Mfano mlijitoa mahakama ya haki za binadamu Africa, mlijitoa Open Governance Initiative ambayo ina advocate uwazi na uwajibikaji serikalini n.k. let alone influence yetu kidiplomasia AU,SADC, na EAC ilishuka sana hatukua power brokers/Regional Kingpins kama enzi zile za 70s-90s.

Nakumbuka hadi Kuna sheria iliundwa ikitaka arbitration eti zisikiliswe humu humu nchini kwa mahakama za ndani?? Kuna mindset mbovu ilijengeka kwamba tunaweza fika mbali bila input ya dunia.

Weird!
Umekosea sana kuwaambia haya, ungeacha wahangaike kuyatafuta wenyewe.
Bwana Yesu alisema "Usimwage lulu kwa nguruwe"
 
MALCOLM LUMUMBA: mada yako ni nzuri Sana vipi lakini unajua kwamba nchi yetu Sasa hivi ipo gizani?Umeeleza vema yaliyotekea ni mabaya lakini haya mambo hayana budi kutokea ili unabii utimie,baada ya gizi hili kipita mwanga utakuja .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakubaliana kabisa na wewe, hatutakiwi kumhukumu mwanadamu katika upande mmoja. Kuna mambo mazuri sana Raisi Magufuli ameifanyia nchi: Japo lengo la huu uzi ni kutaka kufahamu kwanini wale wataalamu kutoka TISS, JWTZ, Foreign Affairs, BoT na Ministry of Finance waliamua kuunga mkono na kufanikisha mambo ya hovyo yaliyokuwa yanafanywa na Raisi Magufuli ilhali wao wanafahamu fika mfumo wa dunia ulivyo na mahitaji ya nchi yetu ???

Ilikuwaje watu wataalamu wa Uchumi, Sheria, Diplomasia na Ulinzi wakaamua kuicha nchi itumbukie kwenye korongo refu ambalo tunahangaika kutoka mpaka sasa ??? Kwanini hawakuchuliwa hatua pale walipotaka kufanya vitendo vya kihaini baada ya Raisi kufariki ??? Kwanini bado wanaendelea kulelewa huku wakizidi kulihadaa taifa ???
Mkuu Malcom naomba utuonyeshe hivyo vyombo ingebidi vifanye nini kwa ukaidi ule wa JIWE..
 
Ninavyosema mahusiano baina ya nchi (International Relations) nazungumzia vitu zaidi ya uwekezaji wa 50/50, zaidi ya sayansi na teknolojia, zaidi ya misaada. Hapa sasa kwenye mahusiano ya kimataifa (International Relations) ndiyo kinakuja kitu muhumu kabisa kiitwacho Diplomasia (Diplomacy): Mahusiano ya kimataifa (International Relations) na Diplomasia (Diplomacy) ni dhana mbili tofauti kabisa, japo huwezi kuzitenga.

Sasa ili ufanikishe mahusiano ya kimataifa (International Relations) ili uweze kupata hizo 50/50, teknolojia, ulinzi au hata misaada ni lazima uwe na chombo kiitwacho Diplomasia (Diplomacy). Lakini ili hichi chombo kiitwacho diplomasia kiweze kufanya kazi vizuri katika kujenga, kufanikisha na kuimarisha mahusiano ya kimataifa (International Relations) ni lazima nchi husika itengeneze kitu kiitwacho Sera ya Mambo ya Nje (Foreign Policy).

Sasa basi ili kuelewa nini kilifanyika hapa Tanzania ni lazima ufahamu mambo niliyoyataja hapo juu:
1. Mahusiano ya kimataifa (A State of International Relations).
2. Dhana ya neno diplomasia (A Concept of Diplomacy).
3. Sera ya mambo ya nje ya Tanzania (Tanzania's Foreign Policy).

Sisi ili kupima mafanikio ya mtu huwa tunaangalia haya mambo matatu ambayo huingiliana. Ulinzi, Rasilimali, Uwekezaji, haki za binadam, soko ya kimataifa, na Misaada ni sehemu ndogo sana ambazo zinaingia kwenye haya mambo makuu matatu. Bahati mbaya sana sasa, vijana wengi wa kitanzania ambao kazi yao ni kusifia na kuunga mkono kila kitu hawana uelewa wowote ule katika hili.

Ndiyo maana huishia kusema tunachuki na marehemu lakini ukweli wenyewe ndiyo huu ambao wengi wao hawataki kuukubali
Madini uliyotema hapa na unayoendelea kutema kwenye huu Uzi nakunyooshea mikono juu! Wewe kwangu ni bingwa! Ni mwalimu!

Heshima yako Mkuu!
 
To be honest i admire your reasoning. Umeandika vyema.

I believe 'diplomacy is an art of compromise'

Sasa kwa magufuli hili lisingewezekana hawezi 'kucompromise' maana deep down kiasili yeye ni mtu wa kuamini anachokiamini yeye tu, hashauriki na hili amelisema mara kadhaa ata hadharani kwamba 'mimi ni jiwe' , 'siyumbishwi' , 'sishauriki' , 'tena mkijaribu kunishauri ndo mnakua mnaharibu kabisa' . Vitu vingi katika international scale kaviharibu kabisa na it will take time kuvirepair, kaua soko la korosho, kavunja mikataba mingi kiholela, ndege zimekamatwa nje, nchi imefunguliwa kesi nyingi za madai kwenye mahakama na wawekezaji waliofukuzwa au kuvunjiwa mikataba yao bila kufuata utaratibu, wakati dunia ikijitahid kupambana na janga la korona ye anakwambia korona haipo hiyo ni michezo tu ya wazungu, n.k. n.k

Mtu yeyote yule anayekataa au anayebisha kwamba Magufuli hajairudisha nyuma Nchi katika nyanja na sera za uhusiano wa kimataifa basi huyo atakua tu naye ni mbishi wa kiasili kama magufuli na hatuna budi bali inabidi tumpuuze

Sasa turudi kwenye hoja yako ya msingi ambayo ningependa pia wachangiaji wanaofuta wajikite nayo ni kwamba 'vichwa vyetu au think tanks wa nchi hii kwenye vyombo vyetu nyeti vya ulinzi na usalama vilikua wapi wakati haya yote yanatendeka???'
Hapa ndipo kuna hoja ya msingi inayohitaji majibu ya kina. Na kama walikaa kimya na mpaka leo wapo kwenye nafasi zao hata kama Uongozi wa juu umebadilika tutawaamini vipi kama wataweza kutuvusha salama sisi kama taifa.
Ni swali zito na fikirishi kwa mustakabali wa Taifa letu.

Tuseme bila kumung'unya maneno! Hao watu ni wahaini. Hao watu inabidi wanyongwe mpaka kufa hadharani.
 
Alikuwa ana akilizi za ziada kuliko maraisa wote wa Tanzania, lakini pia Tanzania lilikuwa ni taifa changa bado.

Alikataa kuruhusu madini yachimbwe hili linakubalika, lakini alifuata kanuni na taratibu za dunia na sheria za kimataifa: Tena alifanya kabisa majadiliano na ushirikiano hata na watu ambao alikuwa hakubaliani nao. Ndiyo Tanzania ilifanikiwa sana kwenye nyanja nzima ya Kidiplomasia......
Exactly, alikuwa anaprotect natural resources za nchi ili nchi inufaike nazo baadae. Wakaja marais wasioona mbali wakafungulia uchimbaji bila kujali kwa kusaini mamikataba ya ovyo yasiyoinufaisha nchi ilimradi tu wamekidhi mahitaji ya ulafi wao. Shame on them!
 
Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.

Bandiko bora kabisa lililogusia history, Geopolitics na diplomasia .
 
Bandiko bora kabisa lililogusia history, Geopolitics na diplomasia .
Sisi ni sehemu ya ulimwengu huu tuna haki pia ya kuweka mustakabali mpya wa mwenendo mpya wa mtazamo wa uendeshaji wa masuala ya ulimwengu. Kukwepa kutumia haki hii kisa tuna tetea status quo ya set up ya sasa ambayo haitunufaishi wote bali baadhi yetu hasa wale tulio wakabidhi dhamana ya uongozi ni kukiri udhaifu ambao hatupaswi kuwa nao!
 
Back
Top Bottom