Imetimia sasa, Yanga kuanza Ujenzi wa Uwanja wa Kisasa Jangwani

Hadi nitakapoona msingi wa uwanja ndipo nitaamini..
Watajenga..rejea mpango wa kuinuia bara bara ya Magomeni - Jangwani..mradi wa mto msimbazi ...na huo mradi wa Yanga kujenga uwanja
 
Mdhamini na Mfadhili wa Klabu yetu, Ghalib Salim Muhammed, ameridhia kwa dhati kushiriki kwenye kufanikisha ujenzi wa uwanja

Kuridhia kushiriki kufanikisha ....What the Sam Hill does that mean??? Maana yake nini ?????

Mtu akijiunga maandamano ya fund raiser ya ujenzi wa bweni la wasichana tayari anakuwa ametimiza ahadi ya kushiriki kufanikisha ujenzi wa bweni la wasichana.... lijengwe, lisijengwe hayamhusu!

Mjanja mwingine huyu anawaingiza chaka Watanzania wajinga wasiojali kusoma makaratasi.....

Halafu mdhamini wa Yanga ni Ghalib mtu au Ghalim kampuni ???? Akijenga kama Ghalib mtu akashindwa kukamilisha au kutimiza vigezo au viwango wakati mshampa nusu ya haki za umiliki au umiliki 100% mkienda mahakamani kumbukeni hamuwezi kugusa mali za Ghalib kampuni.

Kingine, baada ya miaka 10 msije mkalia uwanja hauingiliki, sijui viunga vya uwanja vinajaa maji... Anaweza kupandisha juu uwanja proper, huku nje kwenye parking lot na barabara hawezi kufanya yaliyo mshinda UDART, serikali au KAJIMA. Kwa watoto wadogo, KAJIMA ni Mjapan aliyekuwa anajenga maeneo magumu in the 80s, ndio alijenga Morogoro Road kwenye mkondo wa maji Jangwani. Pameshindikana.
 
Gharama ya mradi wa yanga ni billioni ngapi?
 
hela ya bure ?

Ghalib atatoa mfukoni bilions of money kushindana na maji ya Jangwani ?

Bure bure tu?

hahahahahaaaaa
Si na yeye atawekeza?
Kuna maduka na ofisi zitajengwa.
 
Reporting yako haiko sawa, MISLEADING. Habari ni kuwa GSM itashiriki ujenzi (itatoa fedha za ujenzi)-ahadi au commitment. Na si kwamba Ujenzi unaanza kama ulivyoreport.

Ingawa ni Habari njema, na ni step ahead. Maana changamoto kuu ilikua ni Source of fund.
 
Reporting yako haiko sawa, MISLEADING. Habari ni kuwa GSM itashiriki ujenzi (itatoa fedha za ujenzi)-ahadi au commitment. Na si kwamba Ujenzi unaanza kama ulivyoreport.

sasa kama wanatoa hela kwa nini ujenzi usianze ????

na kushiriki ujenzi maana yake nini, wanatoa hela yote au kamchango kama sunah???


na sio GSM itashariki. Ni Ghalib atashiriki. Kama mtu! Kwa mujibu wa andiko la Yanga wenyewe! Anaweza kushiriki kwenye matembezi ya fund raising! Manake hawajasema atatoa hela!

Usimhukumu mleta mada ambae amebandika tangazo kama lilivyo! Soma tangazo la Yanga! Msituingize mikenge kama ilivyo kawaida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…