IMF: Kasi ya Ukuaji wa Uchumi wa Uganda Kufikia 11% Kuanzia Mwaka 2025 Baada ya Pesa za Mafuta Kuanza Kumiminika

Si ulitaka kujua kipi wako mbele yetu? Nakuongezea hata kiwanda Cha Magari ya umeme,Agri sector Yao Iko vizuri kushinda Tanzania na hata sekta ya viwanda mfano Sukari.
Na mimi ndio nimekwambia nilete hali ya huduma za kijamii ya Uganda!?
Yani social development ikoje!?
Ukanikataza na kudai kuwa unazungumzia yajayo.
Huo uwekezaji wote mbona hauakisi maisha ya raia kwa Uganda??
 
Na mimi ndio nimekwambia nilete hali ya huduma za kijamii ya Uganda!?
Yani social development ikoje!?
Ukanikataza na kudai kuwa unazungumzia yajayo.
Huo uwekezaji wote mbona hauakisi maisha ya raia kwa Uganda??
Wewe kabishabe kwenye nyuzi ya kuliwa kimasihara ila humu unaonyesha unaupeo mdogo sana wa kutoa mada
 
Je ni kwamba sisi hatuna mradi mwingine ambao utaiboost Tanzania kuelekea kwe double digit. Kiwanda Cha kusafisha mafuta kitakuwa Tanga. Kwahiyo tutegemea kupata Kodi na mambo mengine kuzunguka kiwanda yataboost uchumi wa tanzania.
Badooo Kuna nickel kabanga, kiuhalisia Kuna vitu tukikomaa navyoo Bado tunaweza kuendeleza kukua.
Kwa mfano kilimo tu Kuna mazao kama ufuta yanazid kupanda na miongoni mazao yaliyoongoza kwa kuingiza pesa kati ya mazao yote. Hata waanzishe irrigation scheme kivip Dunia Bado itaendelea kuhitaji chakula kuliko uzalishaji wake na hapo ndo Europe au marekani ilipopiga gap.
Kwa mfano kiwango Cha ngani kinachozalishwa ufaransa hakifikii hata robo ya kinachozalishwa afrika na Bado wanakuja kutuuzia sisi
 
Tanga hakuna kiwanda chochote Cha Mafuta hapo ila Kuna matenki tuu ya kuhifadhia Mafuta,kiwanda linajengwa Uganda.

Miradi ipo ila sasa kama kutakuwa na muendelezo wa sera na utekelezaji.

Ugumu unakuja kwamba tunatakiwa hizo sekta zikue Kwa Kasi zaidi ya ongezeko la watu.

Sekta ya Kilimo inatakiwa ikue kwa walau asilimia 6% ndipo walau tunaweza kutafuta hiyo 10% .Kwa Sasa Kilimo kinakua Kwa asilimia 4% kutoka 2% so tunasogea ila Bado safari ni ndefu.
 
Yaishe Abdul mtoto wa mama kizimkazi.
πŸ™πŸ™πŸ™πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Tukienda na mama hadi 2035 atalivusha Taifa hili.

Sasa Kilimo kinakua Kwa 4% kutoka 2% na lengo ni zaidi ya 6% by 2025 na 10% ya GDP itoke kwenye Kilimo ,hii ndio njia mama is doing.

Sekta zingine Wala Hazina shida zinaendelea vizuri but inatakiwa Kasi iongezeke hususani Manufacturing na Biashara.

Utalii Kwa Sasa uko sawa but is very fragile industry πŸ‘‡πŸ‘‡

View: https://www.instagram.com/p/C_2N3MCo7ee/?igsh=Y3B6MjF0cjhzZWZz
 
Takwimu wa IMF na World Bank sio za kuzitilia maanani sana japo ni muhimu kuzingatia

Mara kadhaa washawahi ku-project mafanikio kadhaa lakini baadae ikawa ndivyo sivyo


Kiuhalisia, baada ya kusoma kitabu cha THE CONFESSIONS OF AN ECONOMIC HITMAN ndio nikaja kuelewa kuwa sio kila takwimu huwa sahihi, baadhi hupikwa ili kupush agenda zao


Mojawapo ya matokeo chanya sana tuliambiwa WaTanzania tutapata ni kuhusu ubinafsishaji wa bandari takwimu zilitolewa nyingi sana

Nasubiria impact yake niione, maana muda ni rafiki wa kweli na ni mapema sana kusema lolote juu ya hilo
 
Naungana na wewe,Kilimo Cha Kimkakati Cha mazao ndio iwe kipaombele chetu.

Rais eameanza ila tunataka kuweka na consistency sio akija mwingine anaacha anahamia kwingine,hili limekuwa tatizo kubwa sana kutoelewa vipaombele vya kuondoa umaskini.

Na watawala dhaifu wanakwepa Kilimo Kwa sababu wanaona kinaweza kuwaumbua ila wenye akili wanapambania Kilimo.

Kazi kubwa inaendelea kwenye Kilimo πŸ‘‡πŸ‘‡

View: https://x.com/tzthinker/status/1835414016719532398?t=DNvoNwcDMM5GnjfUrx9I6Q&s=19
View: https://youtu.be/WgKpR1zGPus?si=LoVRSitO1Hw3ZiP2
 
Ushaanza Abdul bin Kizimkazi.
πŸƒπŸƒπŸƒπŸƒπŸƒπŸƒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ
 
Wamekuja na wazo jipya Kila Wilaya inaandaa maeneo Kwa Ajili ya Kilimo huko huko Wilayani kwao.

Ile ya Dom ilikuwa pilot project
 
Affordable living cost for every Tanzanian ndilo la msingi kwanza, hao wengine mnaowaita wana uchumi mkubwa lakini kila siku mbio mbio tu, Nchi zao hazikaliki, maisha magumu ajabu, hii ndiyo nini sasa!
 
Hili wala sio suala viongozi waliopita wlikua wanakwepa. Trend ya Tanzania kuwa top 5 kuzalisha mchele ni muda mrefu tu, uzuri tumeendelea kuishikilia hapo
 
Ethiopia walishasustain mbona kwenye ukuaji wa average ya 10% kwa miaka zaidi ya 10. Au unazungumzia ethiopia ipi?
 
Lazima baada ya muda USA atawapelekea demokrasia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…