IMF yaidhinisha ufadhili wa Dola Milioni 900 kwa Tanzania kwa ajili ya Bajeti na kukabiliana na Mabadiliko ya hali ya Hewa

IMF yaidhinisha ufadhili wa Dola Milioni 900 kwa Tanzania kwa ajili ya Bajeti na kukabiliana na Mabadiliko ya hali ya Hewa

Hahaha hahahaha 🤣 umelala usingizi mzito wewe
Usingizi upi?
20240621_071126.jpg
 
Kila siku mikopo lakini nafuu ya maisha kitaa hakuna, ina faida kwa nani sasa?!.
 
Ndio Nchi kupigwa Mnada?
Haipigwi mnada ila utaona sehemu muhimu kuchukuliwa na mabeberu tukishindwa kulipa mikop. Maana kuna nchi zimewahi chukulia viwanja vyao vya ndege kisa mikopo isiyolipika na masharti lukuki.

Lakini pia mkuu kwenye hali ya kawaida hebu angalia tunavyokopa hovyo mfano SGR ni mikopo mingapi umesikia imekopwa kwa mradu huo tu ,viongozi wanapiga sana hela kwa jambo linaloitwa mikopo na sisi tunaona sawa
 
Kila siku mikopo lakini nafuu ya maisha kutaa hakuna, ina faida kwa nani sasa?!.
Toka lini mikopo lukuki inayotumiwa vibaya ikaleta nafuu ya maisha mkuu...hebu nenda kakope hela halafu kanywee pombe kisha utaona maisha yako yatakavyokua mabaya jama ya digi digi ndo kinachotokea kwetu serikali ina matumizi mabaya ya hela halafu tunaumia sisi kwa kodi za ajabu.
 
Kama mabio alihusika kuleta chura kwa wapigakura basi na alaaniwe yeye na vizazi vyake
 
Hizi habari za kukopa tutaacha lini ndugu zangu wapendwa Watanzania?
 
Huyo chura ndio nani?
Yupo kwenye taasisi ya urais ameshasema yanayofanyika yote kwenye urais wake sio yeye ni taasisi ndio inaamua kwa hio msijemkaanza kumlaumu yeye ilaumuni taasisi sio yeye yeye hausiki
 
Chadema watadhani wamepewa ruhusa ya kula mayai ya kuchemsha na maharage ili waanze kupitisha upepo, kwa kuwa wameona kuna hela za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa
 
Bodi ya Wakurugenzi ya IMF imeidhinisha Mkopo kiasi Cha $900 Milioni sawa na karibu Shilingi Trilioni 2.4 Kwa Tanzania Ili kuisaidia kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Hali ya hewa kwenye uchumi.

Aidha ieleweke kwamba Serikali inakopo kile ambacho kimeidhinishwa kwenye Bajeti,haifangi kiholela.

Aidha ieleweke kwamba Nchi inakopeshwa Kwa sababu Ina uwezo wa kulipa kulingana na uimara wa Uchumi wake. Sio Kila Nchi inapewa Mkopo.

My Take: Katika kipindi hiki Nchi inatekeleza miradi mikubwa ya Maendeleo, Tuendelee kukopa kwani mikopo inaharakisha maendeleo hususani Miradi ya kimkakati

==============


Shirika la kimataifa la fedha (IMF) Alhamisi limesema bodi yake ya utendaji imeidhinisha ufadhili wa dola milioni 786.2 kwa Tanzania kuisaidia nchi hiyo kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Shirika hilo la kifedha linakamilisha pia tathmini tofauti ya kuruhusu malipo ya dola milioni 149.4 kwa ajili ya msaada wa bajeti.

Mamlaka za Tanzania zina dhamira ya kuendelea kutekeleza mageuzi ya kudhibiti uthabiti wa kifedha, kuimarisha ufufuaji wa uchumi, kukuza ukuaji endelevu na shirikishi, IMF ilisema katika taarifa.

Katika miaka mitatu iliyopita, utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan ulifanya mageuzi mbalimbali ya kiuchumi kwa lengo la kurudisha ukuaji wa uchumi katika kiwango cha ukuaji wa pato la taifa la kabla ya janga la Covid wa asilimia 6 hadi asilimia 7.

Mpango wa mageuzi ya uchumi wa Tanzania bado umeendelea kuwa imara, IMF imesema, na kuongeza kuwa ukuaji wa uchumi uliongezeka mwaka 2023 baada ya kupungua mwaka 2022.

Uchumi wa Tanzania ambao unategemea utali, madini, kilimo na viwanda, umeendelea kustahimili mabadiliko ya hali ya hewa yanayochochewa na kuongezeka kwa sekta ya huduma, kulingana na Benki ya Dunia.

Uchumi wa Tanzania unakadiriwa kukua kwa asilimia 5.4 mwaka huu, kutoka asilimia 5.1, waziri wa mipango na uwekezaji katika Ofisi ya Rais, Kitila Mkumbo alisema wiki iliyopita.

DW Kiswahili

PIA, SOMA:
Nazihurumia hizo hela
 
Ngoja wakope ili wataalam wa kutumbua nchi waendelee na projects zao, its nonstop hadi maza aachie madaraka as nchi iko autopilot. Sidhani kama kuna eneo halina upigaji kipindi hiki.

It's a real shame kuwa na utawala wa namna hii.
 
Back
Top Bottom