Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 95,871
- 116,627
Watalipana posho nono na kuziiba zingineJe watakubali tutumie kwenye miradi yenye tija kwenye uchumi?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Watalipana posho nono na kuziiba zingineJe watakubali tutumie kwenye miradi yenye tija kwenye uchumi?
Ufadhili hauwezi kuwa mkopoMkuu unatakiwa ujue by default kwamba World Bank na IMF hawafadhili kitu bure, hawatoi ruzuku(grants) wao wanakopesha.
Kwa hiyo hata ikiandikwa ufadhilii ujue ni mkopo tu huo.
Nisaidie tafsiri ya neno financing kwa kiswahili. Kwa mfano tukisema the world bank is financing the construction of 320km road from Chalinze to Kibaigwa.Ufadhili hauwezi kuwa mkopo
Ni kutoa pesa,je wanatoa kwa misingi gani,mkopo au ufadhili?!..ulishasikia aliyekua mfadhili wa yanga gulamali kaidai yanga?!..au Azim dewji kuidai Simba?Nisaidie tafsiri ya neno financing kwa kiswahili. Kwa mfano tukisema the world bank is financing the construction of 320km road from Chalinze to Kibaigwa.
Mkuu Mo anafadhili simba, anadai ama hadai?😂Ni kutoa pesa,je wanatoa kwa misingi gani,mkopo au ufadhili?!..ulishasikia aliyekua mfadhili wa yanga gulamali kaidai yanga?!..au Azim dewji kuidai Simba?
Sikumtaja mo sababu analeta utapeli,nimemtaja Azim dewji,kaka yake binam aliyefadhili Simba 1990sMkuu Mo anafadhili simba, anadai ama hadai?😂
Anyway, hiyo ndio dhana ya neno financing ama ufadhili.
Hizi ndio hela za rushwa kwa vigogo IMF hua wanatoa. Eti mamilioni kwa ajili ya mabadiliko ya hali ya hewa. Mwananchi gani ataweza kuona au kujua hizo hela zimefanya kazi ya faida yoyote kwake? Wanatoa sifa za bure tu huku wenyewe wananchi tunajua ni ulaji rushwa na ubadhilifu serikali hii imejaai. Magufuli alipokua anawaomba mikopo kwa reri au bwawa la nyerere walimnyima maana wanajua ni mambo ya maendeleo ya kweli ila hivi viinimacho wanatolea hela za kuliwa na huku wakikamilisha biashara ya kukopesha yenye faida kwao. Wanajua kuna mashirika yao yatakuja kushirikiana na vigogo kula hela zitakazobakia deni kwa nchi bila manufaa ila kuweka deni tu kwa wananchi.Bodi ya Wakurugenzi ya IMF imeidhinisha Mkopo kiasi Cha $900 Milioni sawa na karibu Shilingi Trilioni 2.4 Kwa Tanzania Ili kuisaidia kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Hali ya hewa kwenye uchumi.
Aidha ieleweke kwamba Serikali inakopo kile ambacho kimeidhinishwa kwenye Bajeti,haifangi kiholela.
Aidha ieleweke kwamba Nchi inakopeshwa Kwa sababu Ina uwezo wa kulipa kulingana na uimara wa Uchumi wake. Sio Kila Nchi inapewa Mkopo.
My Take: Katika kipindi hiki Nchi inatekeleza miradi mikubwa ya Maendeleo, Tuendelee kukopa kwani mikopo inaharakisha maendeleo hususani Miradi ya kimkakati
==============
Shirika la kimataifa la fedha (IMF) Alhamisi limesema bodi yake ya utendaji imeidhinisha ufadhili wa dola milioni 786.2 kwa Tanzania kuisaidia nchi hiyo kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.
Shirika hilo la kifedha linakamilisha pia tathmini tofauti ya kuruhusu malipo ya dola milioni 149.4 kwa ajili ya msaada wa bajeti.
Mamlaka za Tanzania zina dhamira ya kuendelea kutekeleza mageuzi ya kudhibiti uthabiti wa kifedha, kuimarisha ufufuaji wa uchumi, kukuza ukuaji endelevu na shirikishi, IMF ilisema katika taarifa.
Katika miaka mitatu iliyopita, utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan ulifanya mageuzi mbalimbali ya kiuchumi kwa lengo la kurudisha ukuaji wa uchumi katika kiwango cha ukuaji wa pato la taifa la kabla ya janga la Covid wa asilimia 6 hadi asilimia 7.
Mpango wa mageuzi ya uchumi wa Tanzania bado umeendelea kuwa imara, IMF imesema, na kuongeza kuwa ukuaji wa uchumi uliongezeka mwaka 2023 baada ya kupungua mwaka 2022.
Uchumi wa Tanzania ambao unategemea utali, madini, kilimo na viwanda, umeendelea kustahimili mabadiliko ya hali ya hewa yanayochochewa na kuongezeka kwa sekta ya huduma, kulingana na Benki ya Dunia.
Uchumi wa Tanzania unakadiriwa kukua kwa asilimia 5.4 mwaka huu, kutoka asilimia 5.1, waziri wa mipango na uwekezaji katika Ofisi ya Rais, Kitila Mkumbo alisema wiki iliyopita.
DW Kiswahili
PIA, SOMA: