Ina maana hizi Bodaboda wanazigawa bure kama peremende?

Ina maana hizi Bodaboda wanazigawa bure kama peremende?

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2021
Posts
1,242
Reaction score
4,813
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekabidhi pikipiki 100 zenye thamani ya sh. milioni 260 kwa vijana wa wilaya ya Ruangwa ili wazitumie kufanya biashara ya usafirishaji.

Akizungumza na vijana wa Ruangwa kwenye hafla ya kukabidhi pikipiki hizo iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya CWT, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi, Waziri Mkuu alisema utoaji wa pikipiki hizo ni muendelezo wa mpango wa ofisi ya Mbunge wa kuwawezesha vijana, wanaume, wanawake na wazee.

"Mwaka 2016/2017 tulichukua pikipiki 235 na kuzigawa kwenye wilaya yote hii. Na jambo zuri kwa sasa, kwenye Serikali ya awamu ya sita, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Tanzania na yeye ameamua kuwa na kada ya wasafirishaji wa wadogo, wa kati na wakubwa.”

IMG_6579.jpeg

Chanzo: Mwanahabari
 
Mnaolalamika mnataka vijana wafanyiwe nn kama elimu zao chenga , kulima hawataki , na kuajiri wote kwa mkupuo serikali haiwezi na kuwaondoa wwfanyakazi waliopo ili iingize wapya haiwezi pia ,mnatukana CCM mnataka chama gani kiingie , au huu utopolo wa akina Mbowe na zitto ??? Mtakuwa na makamasi kwenye ubongo
 
Mnaolalamika mnataka vijana wafanyiwe nn kama elimu zao chenga , kulima hawataki , na kuajiri wote kwa mkupuo serikali haiwezi na kuwaondoa wwfanyakazi waliopo ili iingize wapya haiwezi pia ,mnatukana CCM mnataka chama gani kiingie , au huu utopolo wa akina Mbowe na zitto ??? Mtakuwa na makamasi kwenye ubongo
Hatujalalamika. Tunajiuliza tu kama wanagawiwa bure
 
Si ameshasikia hakuna kupita bila kupingwa. Kwanza ameshatumikia miaka 10 ya Uwaziri Mkuu , angepumzika awaachie wengine

Yeye ni nani mpaka we Waziri Mkuu miaka kwa zaidi ya miaka 10?

Kwangu mimi katika Mawaziri Wakuu waliowahi kuongoza Tanzania huyu ni wa mwisho.
 
Mnaolalamika mnataka vijana wafanyiwe nn kama elimu zao chenga , kulima hawataki , na kuajiri wote kwa mkupuo serikali haiwezi na kuwaondoa wwfanyakazi waliopo ili iingize wapya haiwezi pia ,mnatukana CCM mnataka chama gani kiingie , au huu utopolo wa akina Mbowe na zitto ??? Mtakuwa na makamasi kwenye ubongo
Kwaiyo ni kuwaandalia mauaji tu? Ccm uwezo wa kufikiri uligota sasa ivi wanatembelea uzoefu.
 
Badala afungue mashamba na akabidhi matrekta eti anatoa toyo... mawazo machache sana kutoka kwa kiongozi mkubwa kabisa nchini. Bora angekabidhi kimyakimya
 
Back
Top Bottom