Inadaiwa kuanzia Jumatatu hatakiwi kuonekana machinga yeyote mjini Mwanza

Maneno matupu tu haya,mwaka jana kwenye uchaguzi kilichotokea mlijua wanaoadhibiwa ni wapinzani tu na nyie hayawahusu?

Sasa mtatoka na hamna kitu mtafanya na mkianza kuwa vibaka mitaani matairi yapo tutawakaanga.
Na ndiyo walikuwa wa kwanza kuimba... "hatujinyongiiii, hatunywi sumuuu [emoji126][emoji126][emoji1739][emoji12][emoji12][emoji12]"
 
Maeneo gani mkuu wametii amri bila shurti hapa daslamu?
Nenda Mombasa Stendi kama utaona kibanda Cha machinga,wametii sheria Bila shuruti.Buguruni pale kwa Bakhresa wameanza kubomoa wenyewe,Banana wameanza kubomoa wenyewe
 
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Hamkujua maana ya kusoma namba ni nini??? Hamkujua nini maana ya unyonge??? Hamkujua kwanini mliandikishwa vile vitambulisho vya ujasiriamali... !!???
 
Mkuu!!,

Mbona kimya!?

Hujatupa mrejesho.
 
6 Oct 2021
Mwanza, Tanzania

Machinga Mwanza waanza kuhama, Jiji laanza kupangika

Wakati Mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Selemani Sekiete akitoa tangazo la kuwataka wamachinga kuondoa biashara zao kwenye barabara zao kwenye maeneo ya waenda kwa miguu na mbele taasisi za Umma na binafsi hivi karibuni, wafanyabiashara hao sasa wameanza kuondoka katika maeneo hayo na kuingia katika soko maalum waliopangiwa.
Source : Mwananchi Digital
 
2025 watarudi mjini kati maana thamani yao itakuwa imerejea.... Kura!
 
Wamachinga wajue tu kuwa CCM haijawahi kuwa chama cha kuwatetea
Tatizo mnataka huruma wakati mnaharibu utaratibu wamachinga walitumika kisiasa na magufuli akiamini anatunza wapiga kura wake matokeo yake alipo kwama kwenye kukusanya kodi akaanza kutumia mtutu wa bunduki na kuwatumia kina sabaya kufanya uny'ang'anyi wa mali na fedha
 
21 October 2021
Mwanza, Tanzania

"MACHINGA WOTE MWISHO LEO, KESHO MUONDOKE HAPA KAMA TULIVYOKUBALIANA" - RC Eng. Robert Gabriel wa MWANZA

Wamachinga mtaa wa Makoroboi jijini Mwanza, wakubali kuondoka na kwenda maeneo waliyopangwa

Zoezi la kuwapanga kwa, kutenga na kuandaa maeneo ya mbalimbali ya wafanyabiashara wadogo maarufu machinga limekamilika katika mkoa wa Mwanza ambapo Mkuu wa mkoa huo mhandisi Robert Gabriel amefanya ziara ya kukagua na kuona wafanyabiashara walioondoka katika eneo la Makoroboni na kwenda katika maeneo waliyopangiwa.

Maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya machinga ni Dampo la Buhongwa, uwanja wa Chafukoga ulipo Igogo, Igoma na maeneo mengine yaliyotengwa katika jiji la Mwanza.

Wakati zoezi la kuhama likiendelea baadhi ya wafanyabiashara wameanza kuondoa vibanda vyao huku wengine wakisalia kufanya biashara katika eneo hilo la makoroboi.

Aidha mkuu wa mkoa mhandisi Robert Gabriel ameagiza ifikapo kesho Ijumaa octoba 22.2021 wamachinga wote kuondoka katika eneo la Makoroboi na kwenda katika maeneo yaliyotegwa.

Source : Global TV online
 
Acha ujinga wewe,kila machinga kaishapewa eneo la kufanyia biashara

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Wazungu hawakukosea....

Never argue with a fool - They will drag you down to their level, Then beat you with experience!!
Fool ni wewe unayetetea ujinga,hao machinga wanalindwa na sheria ipi?

Usiishi kwa mazoea kenge wewe fuata sheria,kanuni na taratibu pimbi kabisa
 
Fool ni wewe unayetetea ujinga,hao machinga wanalindwa na sheria ipi?

Usiishi kwa mazoea kenge wewe fuata sheria,kanuni na taratibu pimbi kabisa
Never argue with an idiot. You’ll never convince the idiot that you’re correct, and bystanders won’t be able to tell who’s who.

Nilifunzwa na Mama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…