Mkuu tetea hoja yako kwa kuanisha facts and proofs za hayo maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi na Taifa hili katika kipindi chake.
Matusi na propaganda uchwara haibadilishi ukweli kuwa alikuwa Rais wa hovyo kuwahi kutokea nchi hii.
Nataja facts na wewe utaje facts za Magufuli kufirisi nchi.
Magufuli aliiendeleza hii nchi kwa yafuatayo;
1)Aliweka nidhamu katika utumishi wa umma,hii ilisaidia well provision of social services na unyanyasaji ukapungua.
2)Aliongeza wimbi la wasomi/percentage of literacy rate kwa kuweka elimu bure mpaka kidato cha nne na ada nafuu kidato cha 5 na 6.
3)Alifufua baadhi ya vitu ambavyo kama vingesimamiwa vyema ni vya kuongeza pato la taifa,mathalan ufufuaji wa njia ya reli ielekayo Arusha/Moshi na ufufuaji wa kusafirisha mizigo kuelekea Uganda kwa njia ya reli kupitia Lake Victoria.
Hii iliongeza fursa za ajira na kipato TRC.
3)Utekelezaji wa miundombinu muhimu ambayo ipo iliyoboreshwa na ipo iliyoanzishwa mipya ambayo imeongeza ufanisi wa uzalishaji katika sekta husika,mathalan ubadilishaji wa reli ya zamani ya TRC kuwa continous welded,kuliongeza ufanisi wa treni kutembea katika reli kwa mwendo kasi,ujengaji madaraja yaliyosaidia usafiri kuwa rahisi mathalan Tanzanite bridge,Nyerere bridge na Kigogo-Busisi bridge,kijazi interchange na flyover nyingine ikiwemo ya uhasibu,kumefanya raia tuokoke sana na foleni na kuwahi sehemu za uzalishaji.
4)Ufufuaji wa vitu ama mashirika ya serikali,japo nguvu haikutosha ila hatua ilikua nzuri mathalan ATCL na TTCL,la TTCL lilifanikiwa zaidi japo baada ya yeye kufariki TTCL ikazorota tena.
5)Uanzishaji wa miradi yenye tija kama ingesimamiwa vizuri katika uzalishaji na urahisishaji baadhi ya huduma za kijamii mathalan unazishwaji wa mwendokasi na JNHPP power utakaozalisha umeme kwa wingi.
6)Ideology ya Tanzania kujitahidi kujitegemea wenyewe na kupunguza utegemezi wa mataifa ya kibepari.
7)Uimarishaji wizara ya madini kwa kuleta gold refinery na kuwasaidia wachimbaji wadogo wadogo kiuzalishaji.
Hili lime boost uuzaji wa dhahabu safi yenye kiwango kutoka Tanzania ambayo ni 99.99% na matunda yake mpaka sasa yanaonekana.
Hatua zote hizi ziliifanya Tanzania itoke katika nchi zenye umasikini komavu(poorest country with intensive poverty)na kuwa katika nchi zenye umasikini wa kawaida(Low middle income country).
Ila cha ajabu kuingia 2022 Tanzania imerudi katika nchi yenye umasikini komavu na kuwa miongoni mwa mataifa 35 masikini duniani.
Aya lete wewe facts za kusema MAGUFULI KAIFILISI NCHI.
Ukileta hizo nitakuletea hatua alizozifanya Samia ambazo zikaifelisha Tanzania.