Inakuaje!

Nimeuliza Lizzy una mume ili tuone tutachangia vipi maana unaweza ukawa unaizungumzia ndoa kinadharia zaidi. Kama umeolewa una muda gani ndani ya ndoa? Ukitaka kumlaumu mtu unatakiwa kwanza uvae viatu vyake ndo uweze kukosoa ama kusifia

hakuna cha kuvaa viatu
khaaaa ..
na sisi tulioona wazazi wetu
wanapitia hayo hivyo si viatu tosha...
saa nyingine chakula kina harufu mbaya
si lazima uonje ndo ugundue kimeoza..
Na lizzy haja kosoa wala kusifia kauliza..
 
Kumbe mpaka uwe umeoa/kuolewa ndio unaweza kuzungumzia ndoa, nilikuwa sijui kwa style hii kazi ipo

Hivyo hivyo ndo itakua mpaka uwe maskini ndo uongelee wizi..uchanganyikiwe ndo uongelee bangi...upate mimba ndo uongelee utoaji!Kazi ipo si kidogo!
 
Hilo pia ni suhisho ila kama hutakuwa makini utaoa/kuolewa na kuachana mpaka itakuwa kero sasa. Kwa ufupi kutoka nje ya ndoa haimaanishi upendo umeisha ni adventure pia saa nyingine.
 
Hilo pia ni suhisho ila kama hutakuwa makini utaoa/kuolewa na kuachana mpaka itakuwa kero sasa. Kwa ufupi kutoka nje ya ndoa haimaanishi upendo umeisha ni adventure pia saa nyingine.

Hizo adventure huwezi kuzitafuta na kujiridhisha nazo kabla hujaoa??
 
Hayo unayoyasema unaweza kuingia kwenye ndoa na usikutane nayo so it depends.
 

Lizzy mdogo wangu,

Ndoa ni kitu tofauti na haya tunayoongelea. Kuna watu wanaingia kwenye ndoa kutafuta heshima na siyo kuridhika kwa moyo. Kwa hiyo tunaweza kusema mengi ila ndo aiachwe tu ilivyo. Ni dude ambalo hata waliomo hawaliewi vizuri.

Naanza kwa kiasi fulani kukubaliana na Lord...Hapa tunaweza kuongea mengi ila aijuaye aibu ya maiti ni mwosha!
 
Kumbe mpaka uwe umeoa/kuolewa ndio unaweza kuzungumzia ndoa, nilikuwa sijui kwa style hii kazi ipo

Hypothetically siyo lazima ila realistically kuna ukweli fulani. Ni kama ambavyo sijui a.b,c za American football kwa hiyo siwezi kuiongelea ila theoretically naweza kuongelea soccer kwa sababu walau najua vitu kidogo vinavyohusiana na huo mchezo. Hata hivyo practically siwezi kuingia kwa ndani kuhusu mambo ya soccer!
 
Hilo pia ni suhisho ila kama hutakuwa makini utaoa/kuolewa na kuachana mpaka itakuwa kero sasa. Kwa ufupi kutoka nje ya ndoa haimaanishi upendo umeisha ni adventure pia saa nyingine.
Kumbe kutoka nje ya ndoa ni adventure binadamu tuna kazi sana suprises huwa haziishi na hii ndio imenishangaza haswa hivi hizo adventure hauwezi kuzifanya kabla haujaoa
 
Kumbe kutoka nje ya ndoa ni adventure binadamu tuna kazi sana suprises huwa haziishi na hii ndio imenishangaza haswa hivi hizo adventure hauwezi kuzifanya kabla haujaoa

TF, binadamu siyo static kiasi hicho kwamba ukifanya adventures ujanani baadaye unastaafu. Ndo maana mizee inaongoza kwa ufataki. Unahitaji miwani kuuona huo ukweli?
 
Na ndio maana nikasema not neccesarily hayo anayoyasema yatokee maana saa zingine yanaweza yasitokee
 
TF, binadamu siyo static kiasi hicho kwamba ukifanya adventures ujanani baadaye unastaafu. Ndo maana mizee inaongoza kwa ufataki. Unahitaji miwani kuuona huo ukweli?
Mzee DC naomba unieleweshe labda mimi sielewi kwa vile sijaoa hizo adventure unazofanya nje ya ndoa yako ni kwamba ni bora kwako kwa vile hautosheki au ni kwa vile unaamua kufanya kwa kisingizio cha kuwa ndoa yako ina matatizo?
 
umeamua kuoa = tulia
umeona ndoa haikufai =timua usimuze mtu in anyway
( physical {magonjwa}, emotional and mental)
ulielewa ndoa niku kigumu tangu mwazo hata dini zetu zina fahamu hili
"kwenye shida na raha" ... Wengi tumekulia kuona jinsi wazazi walivyokuwa
wanapurukushana wenye upendo wa hali ya juu walitulia na kuvumilia na wale
walioona hii mie siwezi walicheza mbele sioni kutoka ndani ya ndoa yako ndio Solution..
umeoa kwa sababu gani??

huu ni Uhuni mtupu...
 
Mzee DC naomba unieleweshe labda mimi sielewi kwa vile sijaoa hizo adventure unazofanya nje ya ndoa yako ni kwamba ni bora kwako kwa vile hautosheki au ni kwa vile unaamua kufanya kwa kisingizio cha kuwa ndoa yako ina matatizo?

TF, bahati mbaya sijawahi kujaribu hiyo biashara ya kutoka nje ya ndoa kwa hiyo sina uzoefu unaonihusu mimi binafsi. Ila ukweli ni kwamba watu wengi wanatoka nje ya ndoa. Siyo kwa sababu ya kutotosheka wala kwa sababu ya kisingizio cha kukerwa na wenzi wao. Bali wanajikuta katika tamaa ya kubadili mboga tu hata kama main menu ni ile ile!
 

AD,

Hakuna anayekataa kwamba kutoka nje ni uhuni. Ila asilimia kubwa ya wanandoa (may be zaidi ya 80%) wanatoka nje ya ndoa. Hapo ndipo kizungumkuti kinapoanzia. Amini usiamini hakuna mwenye immunity dhidi ya hii kitu. Ukiweza kuwa miongoni mwa wachache waliomudu kuishi kwenye ndoa kwa staili ya useja basi gold medal itakuwa halali yako.

Binafsi sina hakika kama nitafikia umri wa kuzima kibatali nikiwa nimeumudu huo useja. Ni kazi ngumu sana!
 
AD kweli inasikitisha!Anayokushauri usifanye yeye anafanya zaidi...kama mtu ameamua kua mtu wa ajabu awe tayari kuonekana wa ajabu na sio kupofua watu wengine kwa ngozi zisizo zao!Tamaa inaua wadau...
Lizzy.....hope you had a wonderful easter

Maisha ni kitu kigumu sana kukielewa hasa katika nyanja ya mapenzi Dada yangu. Kutokana na post yako ni wazi kuwa unawafahamu fika whoever unayemzungumzia BUT sidhani kama unawafahamu kwa kiasi hicho cha kujua wenzi wao ni wema, wazuri n.k kwa sababu aliyeko ndani ya chungu kile ndiye ajuaye ukali wa moto unaopikia. So kusema kuwa mume wa mwanamke mtokaji ni mzuri, mwema n.k. we need to be cautioned kidogo.

Pili kuna mtu alishasema kuwa kuolewa/oa si mwisho wa kupenda. Ni utashi wa binadamu na utaendelea tu kuwa hivyo so kuridhika na uliye naye ni azi kidogo. Na si kweli kuwa waliooa/olewa hawapendi tena bali tunakuwa restricted na taratibu za ndoa kuwa ukishaoa/olewa huruhusiwi kupenda tena japo ni against human nature. So watu tunalazimika kuabide and wherever there is this condition inategemea na uwezo wa mtu wa kujicontrol kuzuia kupenda nje so tegemea kuna wanaoweza na wale wasioweza.....ni maumbio yetu.

Lakini pia sikatai kuwa kuna mmomonyoko wa maadili kuwa tamaa zinatuzidi na tunajikuta tunashindwa abstain. ila panapohusika na tamaa si rahisi ukawakuta hawa wawili wakadumu kwa muda mrefu as watatamani tena sehemu nyingine na safari ikaendelea. Maisha ya mahusiano ni magumu kwa kweli.

Mwisho kwenye suala la kuwa role models na wanaowapreachia kuwa wema wakati wao ni waovu............tunahubiriwa kila siku kuwa kutende kwa kadri ya mafundisho yao na si kwa matendo yao.......na hii haiko katika mahusiano tu, hata kidini ni mara ngapi tunakuwa na wahubiri au viongozi wa dini wenye mambo ya kidunia but tunashauriwa kutenda yale wanayotuhubiria na si yale wanayoyatenda.
Happy Easter bi dada
 
Nashukuru DC kwa majibu yako
 


MJ1,

Habari yako binafsi mjukuu wangu? Naamini easter imeenda vizuri na ikakuacha mzima kabisa.

Kwa ufupi na bila kuchakachua post yako ni kwamba UNAFIKI NDiO UNATUTAWALA SISI BINADAMU. Uhalisia unapatikana kwa nadra sana!

Mubarikiwe nyote bandugu bapendwa!

DC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…