Inakuwaje graduates wa UDOM wanafaulu sana sahili za Utumishi?

Inakuwaje graduates wa UDOM wanafaulu sana sahili za Utumishi?

Graduates wa UDOM niliokutana nao kikazi wako vizuri. UDSM siku hizi kwa kweli vijana wachache ndo wanatoka wakiwa competent, wengi wanaongea vingereza kama watoto wa English medium.
 
Lakini UDSM si wanasema inachukua wanafunzi wa division one tu, inakuwaje performance yake iwe sawa na vyuo vingine?
Mambo yanabadilika mzee

Unaweza kitaa div 3 akifika Chuo anabadilika kabisa anakuwa mtabe kweli.

Wengi akili za kitoto ndio ziliwakwamisha sekondari.

So kuwa na division haisaidii kitu je performance Yako Chuo ikoje na competence Yako Ikoje.

Kuna cousin wangu mmoja alipita na division 3 o level akaenda advance nayo akapata 3 enzi za mkwere akapata Chuo Fulani kule Chuo alikuja ibuka best student tulishangaa hata sisi. GPA Kali sana.

alipomaloza tu Wala hakusota kitaa alikaa mwaka mmoja tu akapata kazi serikalini taasisi Fulani tena kupitia huko ajira portal.

So division one za udsm sio kwamba ndio wataalanu sana huko Chuo wengi wanazembea sana wanasoma kwa mazoea wanadhani Jina la Chuo kitawabeba matokeo yake wanasaga soli.

Halafu udsm alumni wako selective sana wanangoja TRA na the like ndio waombe kazi
 
Kwa taarifa yako,
Jina hili ni miongoni mwa chachu zilizoifanya UDOM ipae. Labda kwa faida yako mkuu; ukimpa mtu jina la kebehi linasababisha ajitathmini na hatimaye afanye maboresho makubwa kwenye nyanja tofauti mwishowe anakuwa mtu bora kwenye jamii.
Mbona maneno mengi kama unateseka hivi😅😅 Udom chuo cha KATA
 
UDSM ni rare products wewe, wale huwa wao hawaombi hivyo viajira. Zikitoka zile ajira za maana huwa waajiri wanaenda Chuo na kuomba majina ya wanafunzi waliomaliza halafu wanawatafuta kuwaomba wakubali kujiunga na makampuni/taasisi/mashirika yao.
vikibaki hivi vinafasi vidogo ambavyo wanafunzi wa UDSM huwa wamevikataa ndiyo wanaenda kuvitangaza na hapo ndiyo utaona akina UDOM wakivugombea😄😄.
Hauwwzi ukakuta mwanafunzi wa UDSM akiwa mtaani😀😀

Wewe unathibitisha kuwa watanzania wengi ni waongo sana.

Hii tabia ya kusifia vyuo mlivyotoka inaharibu elimu sana,tabia hii imesababisha sua na udsm kuelekea kufa kizembe.
 
Mbona maneno mengi kama unateseka hivi😅😅 Udom chuo cha KATA
Ni chuo cha kata kweli,ila ndio hivyo graduate wake wanaaminika.
Mwezi wa kwanza TAEC wamechukua 10 wote udom,na kweli wako vizuri.

Haya hao wa vyuo bora udsm na wenzenu sua wako wapi?
 
Watu mnalishwa matango pori na nyie mnayala bila kuhoji.
Mleta mada tupe data za research yako.
 
Ni kweli kabisa lakini ukweli ni kwamba Magufuli atakumbukwa sana kwa kukibadilisha hiki chuo kuondokana na kuzalisha vilaza! Udom kimeboreka sana sana…
Pia Utaratibu wa TCU kupangia wanafunzi vyuo umesaidia kubalance, vinginevyo usingekuta mwanafunzi kichwa anaenda udom, Nina case Moja ya products nyingi za CBE especially dodoma kampasi kuwa na vilaza wengi ila Kuna kijana nilimpata aliyemaliza pale ni exceptional! Kwa hiyo pamoja na inputs za chuo chenyewe, na uwezo binafsi wa mwanafunzi unachangia kwa 70%
 
Jamani kwani ufanisi wa mtu unapimwa na chuo alichosoma? Tusipende kushusha thamani ya chuo husika, unaweza ukawa umesoma udom lakini kichwani ukawa upo vizuri sana

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Jamani kwani ufanisi wa mtu unapimwa na chuo alichosoma? Tusipende kushusha thamani ya chuo husika, unaweza ukawa umesoma udom lakini kichwani ukawa upo vizuri sana

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
Mbona hakuna aliyeshusha chuo thamani. Hizo coment fedhuli baadhi ni za wanafunzi ambao bado wapo vyuoni,.kwahiyo usihangaike nazo, wakirudi mtaani adabu itakuwepo.
 
Back
Top Bottom