Inakuwaje mtu anagoma kufa mpaka amuone mtu anayemhitaji kumuona?

Inakuwaje mtu anagoma kufa mpaka amuone mtu anayemhitaji kumuona?

Asalaam!
Rejea mada tajwa hapo juu. Kuna suala moja nimejihoji kwa muda mrefu lakini sijapata jawabu kutokana na visa vikuu viwili nilivyovishuhudia mwenyewe.

Mwaka 2013 mkoani Mbeya, Baba yetu mkubwa aliugua sana. Alizungushwa hospital nyingi sana pasipo mafanikio.
Mara ya mwisho ilikuwa MNH ambapo alishauriwa kurudi nyumbani ili walau ndugu wahangaike na tiba ya upande wa pili.
Mzee yule alikuwa akisema natamani kufa lakini kabla sijafa nataka kumuona mwanangu wa mwisho Asubhisye ambaye alikuwa Tanga. Ilibidi aitwe na aliporudi nyumbani Asubhisye aliongea nae na Mzee akachangamka kweli. Cha ajabu kesho yake alifariki.

Kisa cha pili nilikishuhudia kwa baba mwenye nyumba enzi nafanya kazi Geita mwishoni Mwa mwaka 2013. Mzee yule aliitwa Kachila alikuwa Muha wa Kasulu huko. Aliugua sana na matibabu yalishindikana.

Alikuwa kila Mara akisema naombeni muende Ukerewe mkaongee na Mke wangu amlete mtoto nimuone. Miaka mitatu nyuma alitengana na mkewe ambaye alikuwa mjamzito na tangu aondoke hakuwahi kurudi hata baada ya kujifungua.

Baada ya matakwa yake kutekelezwa naye alifariki baada ya siku moja.
Sasa najiuliza...je kuna mahusiano gani kati ya kukata roho na kumuona MTU unayemhitaji?

Kwa visa tajwa hapo juu, je nawe umewahi shuhudia au ni coincidence tu niliyokutana nayo?

Karibuni tueleweshane na kubadilishana uzoefu katika hili!



Sent using Jamii Forums mobile app
In short hao wote walikua wame sell their souls to the devil.
Wanachofanya ni kuacha maagizo na Mikoba iendelee kwa kizazi kijacho walichokikabidhi kama kanuni inavyowataka kwenye ukoo na mila za matambiko.
Na Roho zao wanazikabidhi baada muda mfupi waliokaa hapa duniani wakitumikia.
Na kinachowatokea sio natural death/God's plan.

Reason:- Hakuna mwanadamu mwenye uwezo WA kuamua afaje.
Cc mshana jr

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kisa hiki changu nadhani utashi tu wa mtu ndio humfanya awe na hofu kubwa ya maisha hata kuhisi kifo kinamkabili.

Baba yangu mdogo baada ya kuugua sana kwa kipindi cha muda mfupi, alipoteza kabisa hata nguvu ya kugeuka kitandani. Siku moja akiwa na mdogo wake pale hospital, alimuagiza aje aniite kwani Ana maongezi na mimi.

Nilifika pembeni ta kitanda chake kisha akanishika mkono na kuniachia maneno ya wosia. Alipomaliza, alinitajia namba yake ya siri ya ATM ya NMB akaniomba nikamtajie mama mdogo ila kadi ya CRDB nibaki nayo. Aliongea kwa sauti ya upole na msisitizo hata kidume nikadondosha machozi.

Baada ya mimi kuondoka eneo la hospitali, hali ya mzee ikabadilika na kuwa mbaya, akapewa referral kwenda MNH, baada ya mwezi mmoja, alipona kabisa na yupo hai mpaka leo.
Ilikuwa 2012 lakini siku ile naikumbuka mpaka leo kama vile ni tukio la jana.
So sio kila mtu akihitaji kuonana na mtu basi HUFA baada ya kumuona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa hawagomi kufa... maana ukijua mtu kagoma kufa mpaka amwone flan nanyi hamtaki huyo mtu afe basi mna mwambia tu jamaa alisafiri kwenda uk ndo anadunduliza nauli aweze kurudi uje umwage so vuta vuta subira msubiri aje... au unamwambia naye jamaa hali yake ni mbaya hatukukwambia subiria apone then aje akuone.
 
Kumbuka hata yule nabii Mzee wa kwenye biblia aliyeambiwa na Roho mt. Kwamba hatakufa mpaka atakapomwona masihi ( yesu) na baada ya yesu kuzaliwa yule Mzee alipomwona, alisema hivi " sasa Bwana waweza kumchukuwa mtumishi wako apumzike kwa amani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asalaam!
Rejea mada tajwa hapo juu. Kuna suala moja nimejihoji kwa muda mrefu lakini sijapata jawabu kutokana na visa vikuu viwili nilivyovishuhudia mwenyewe.

Mwaka 2013 mkoani Mbeya, Baba yetu mkubwa aliugua sana. Alizungushwa hospital nyingi sana pasipo mafanikio.
Mara ya mwisho ilikuwa MNH ambapo alishauriwa kurudi nyumbani ili walau ndugu wahangaike na tiba ya upande wa pili.
Mzee yule alikuwa akisema natamani kufa lakini kabla sijafa nataka kumuona mwanangu wa mwisho Asubhisye ambaye alikuwa Tanga. Ilibidi aitwe na aliporudi nyumbani Asubhisye aliongea nae na Mzee akachangamka kweli. Cha ajabu kesho yake alifariki.

Kisa cha pili nilikishuhudia kwa baba mwenye nyumba enzi nafanya kazi Geita mwishoni Mwa mwaka 2013. Mzee yule aliitwa Kachila alikuwa Muha wa Kasulu huko. Aliugua sana na matibabu yalishindikana.

Alikuwa kila Mara akisema naombeni muende Ukerewe mkaongee na Mke wangu amlete mtoto nimuone. Miaka mitatu nyuma alitengana na mkewe ambaye alikuwa mjamzito na tangu aondoke hakuwahi kurudi hata baada ya kujifungua.

Baada ya matakwa yake kutekelezwa naye alifariki baada ya siku moja.
Sasa najiuliza...je kuna mahusiano gani kati ya kukata roho na kumuona MTU unayemhitaji?

Kwa visa tajwa hapo juu, je nawe umewahi shuhudia au ni coincidence tu niliyokutana nayo?

Karibuni tueleweshane na kubadilishana uzoefu katika hili!



Sent using Jamii Forums mobile app
Sio hvyo tu mkuu, wengne kabla ya umauti huwa wanaomba wapikiwe aina flan ya chakula, au hata huomba maji ya kunywa....haya mambo kina mshana jr wanaeza kufafanua zaid, wamebobea ktk hz fani ngoja tumuite aje
 
Back
Top Bottom