Inakuwaje sarafu za milioni 200 zinafichwa mamlaka zisishtuke mapema?

Inakuwaje sarafu za milioni 200 zinafichwa mamlaka zisishtuke mapema?

MAKULUGA

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2011
Posts
7,828
Reaction score
10,527
Salama JF?

Kutokana na jinsi Mambo yanavyoenda nchini siku hizi siangalii wala kusikiliza taarifa za habari za ndani.

Nimewapa jukumu watoto wangu kuangalia taarifa ya habari ili baadaye waniambie wamepata habari gani. Mimi nimebaki kuingia JF, Instagram,Twitter na kwingine ambako napata habari za ukweli, umbeya, majungu, tetesi na uchambuzi. Jukumu langu ni kutumia akili yangu na kaelimu kangu kadogo kuzichuja!

Jana watoto walipoona habari ya Wachina kukamatwa na magunia ya Sarafu za Tanzania walilazimika kuniita nishuhudie mubashara!

Kwa wale ambao hawakubahatika kuona ni kuwa Wachina wachezesha kamari walikamatwa na sarafu za Tsh.200 na 500 zenye thamani ya Sh.Milioni 200.

Nimejiuliza lengo la hao ndugu wa Nyerere nini au ni kukwepa kodi? Swali gumu zaidi, inakuwaje kwa Mji mdogo kama Morogoro sarafu za Milioni 200 zitolewe kwenye mzunguko mamlaka husika zisigundue hadi wakusanye viroba vya fedha kiasi kile!?

Kwa akili yangu, inakataa na kuuita huu ni uzembe uliovuka mipaka! Hata Kama sio Mtaalamu wa fedha au mchumi lakini mhhhh!
 
Hayo mamichezo yafutwe yanaharibu sana watoto, na hii bodi ya michezo ya kubahatisha imelala inatoa tu leseni kiholela.

Jamani zile mashine ni programmed, programmer anaweza weka conditions katika watu kumi wanaocheza washinde wanne kwa interval fulani sasa hiyo utaita ni bahati nasibu.

Bodi kabla haijatoa leseni ya hayo madude ilitakiwa ichukue hata madude 10 wakae nayo wiki nzima waone ila hata isingesaidia sana maana mwiaho wa siku yanabadilishwa setting kirahisi, wito wangu hayo mamashine yafutwe kabisa hawa wachina wanatuchuna ngozi bila ganzi.

Wanaingiza pesa nyingi kwa kazi zisizoeleweka.

Hayo madude wameyasambaza hadi maeneo ya vijijini kukamua maskini, ni kama kuku wao wa mayai wamewasambaza mwisho wa siku wanaend kuokota mayai.

Bodi ya michezo ya kubahatisha haya madude tuondoleeni tafadhali watoto wanaiba pesa wanapeleka huko.

Mwisho.
 
Sioni tatizo hapo kwani wabongo wenyewe ndo wanawapelekea hizo sarafu kwenye zile mashine za bonanza sasa shida iko wapi??

Wao wameona fursa ya wabongo kupenda kamari na fedha za mdebwedo na wakaamua kutumia fursa. Hizo sarafu ndo commodity kwenye biashara yao,kuwakamata wakati ww ndo umewapa leseni ya biashara sio busara. Mara mia wawafungie tu hizo mashine zao za bonanza
 
Sioni tatizo hapo kwani wabongo wenyewe ndo wanawapelekea hizo sarafu kwenye zile mashine za bonanza sasa shida iko wapi??

Wao wameona fursa ya wabongo kupenda kamari na fedha za mdebwedo na wakaamua kutumia fursa. Hizo sarafu ndo commodity kwenye biashara yao,kuwakamata wakati ww ndo umewapa leseni ya biashara sio busara. Mara mia wawafungie tu hizo mashine zao za bonanza
Mkuu hiyo biashara ni halali...Mimi nashangaa kuweka ndani Kiasi kikubwa cha Fedha ...Mimi kwa uelewa wangu Fedha ni Mali ya Serikali, sisi tunamiliki thamani ya fedha,!

Ndio maana ukifanya kazi unalipwa kwa kuthaminisha na Fedha... Sasa ukizitoa kwenye mzunguko huoni kuwa Ni hatari!
Hata ule mchezo wa Dar kuuziana change' Nafikiri kiuchumi SIO SAWA!
 
Tatizo siouhakali,kwa Nini wazifungie ndani ...Sarafu M200!
Mkuu hizo sarafu ndio kama commodity zao, ni kama wewe uwe na duka na bidhaa za kuuza. Kwao bidhaa ni hizo sarafu. Na sehemu kama Morogoro wanakua wameweka vituo vingi sana hadi vijijini na huwa hawaajiri mtu mweusi ashike hela zao so utakuta sarafu zote kwenye hivyo vituo zinakusanywa sehemu moja na zitasambazwa tena baadae zikihitajika.

Naamini wakiwakagua hata mikoa mingine kama Dar na mwanza watakuza hata zaidi ya mil 400 za sarafu
 
Mkuu hiyo biashara Ni halali...Mimi nashangaa kuweka ndani Kiasi kikubwa Cha Fedha ...Mimi kwa uelewa wangu Fedha ni Mali ya Serikali,sisi tunamiliki thamani ya fedha,!
Ndio maana ukifanya kazi unalipwa kwa kuthaminisha na Fedha...Sasa ukizitoakwenye mzunguko huoni kuwa Ni hatari!
Hata ule mchezo wa Dar kuuziana change' Nafikiri kiuchumi SIO SAWA!
Mkuu unachosema ni kweli lkn na wao wanachofanya kwao ni sawa kabisa kutokana na nature ya biashara yao. Tatizo ni kwamba serikali haikuifanyia uchunguzi mzr hii biashara kabla ya kuwapa leseni na haya ndio madhara yake
 
Ninavyoelewa Mimi hayo makokoro yanautumia coins 200 na 500. Na mashine moja inaweza kuweka mpaka coin 1000.

Sasa kila siku lazima wapitie mashine zote kuongeza pesa ama kuchukua pesa.

Sasa lazima wawe na float (working capital).

Ukiangalia 200million gawanya kwa Mia mbili unapata coin 1,000,000 za Tsh 200 ama 500,000 za Tsh500.

Kama Wana mashine 200 maana yake kila mashine imekuwa allocated 5000 coins za Tsh 200 au 2500 za Tsh 500.

Hivyo kuwa na hizo coin Wala sioni Kama ni shida.

Mbona Kuna watu ulienda nyumbani kwao watakuwa na zaidi ya billion 3 ndani kwao.

Tujipange na mambo ya maana.

Covid inaua, stay safe stay home
 
Back
Top Bottom