Inasemekana alipotekwa Nondo kuna CCTV Camera, pia simu ya moja ya watekaji ilianguka na imekabidhiwa polisi. Je, watakamatwa?

Inasemekana alipotekwa Nondo kuna CCTV Camera, pia simu ya moja ya watekaji ilianguka na imekabidhiwa polisi. Je, watakamatwa?

Serikali inataka kuhalisha mjadala wa rafu za uchagizi wa serikali za mitaa hakuna jipya hapo
 
Wakuu,

Inasemekena eneo alilotekewa Nondo kuna CCTV Camera inayorekodi matukio eneo hilo, lakini pia katika purukushani za patashika nguo kuchanika simu ya moja ya watekaji ilianguka chini, na hivyo vyote amepewa Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Magufuli.

Wakuu hii ina maana wasiyojulikana kwa mara nyingine watajulikana, na ni suala la muda tu kama kuna hata mmoja alifanikiwa kurekodi tukio hilo video zitaanza kusambaa.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Swali la muhimu ni kwamba tutaona watu hawa wakifikishwa kwenye mikono ya sheria, au Jeshi la Polisi litatulia bati kama ilivyokuwa kwenye utekaji wa bonge ambako wameshindwa hata kutoa majina tu ya wale watekaji wakati picha zao zinaonekana!

Au ndio ataambiwa tena kuwa alijiteka, walikuja ndugu zake wakafanya igizo! Ila polisi wa TZ mna sehemu yenu mbinguni kwa sir God!
Unaanzaje kukabidhi simu ya watekaji kwa polisi ambao in fact ndio watekaji wenyewe ?
 
Unaanzaje kukabidhi simu ya watekaji kwa polisi ambao in fact ndio watekaji wenyewe ?

..yaani natamani kusikia habari hii.

..kupitia simu hiyo mambo mengi sana yangeweza kujulikana kuhusu genge hilo.

..Polisi au wasiojulikana wakikuteka jambo la kwanza wanataka simu yako, sasa sisi tumepata simu yao halafu hatujiongezi.

..THIS IS A VERY STUPID MISTAKE, AND A GOLDEN CHANCE HAS BEEN WASTED.
 
Alipopigiwa risasi Lisu pana CCTV camera masaa 24.

Pia pale Kibo Complex alipotekwa mzee Ali Kibao pana CCTV camera masaa 24.
 
Hata alipopigiwa risasi Lisu palikuwa na CCTV camera masaa 24.

..muhimu zaidi ni nani ana access na CCTV zilizoko eneo la tukio.

..kama ni SERIKALI basi itakuwa vigumu sana kupata ushahidi huo.

..ACT wanatakiwa wapige kelele ili ushahidi wa CCTV utolewe hadharani.
 
..CCTV za tukio la Lissu hazikuangukia mikononi mwa Chadema, au wananchi.

..Chadema wangepata CCTV hizo tungekuwa tunazungumza habari nyingine.
Yeah wangefahamika sura zao lakini wasingefanywa lolote, unadhani wanapoteka live wanavaa masks? Si wanaonekana sura zao? Picha za watekaji wa yule bonge si zimejaa mitandaoni lakini umesikia lolote kutoka kwa polisi kuhusu upelelezi wa issue hiyo?
Hao watekaji labda wauawe kwenye scene ndiyo suluhisho pekee lakini hilo likifanyika ghadhabu ya vyombo vya dola pamoja na UVCCM ndiyo itaonekana dhahiri shahiri.
 
Wakuu,

Inasemekena eneo alilotekewa Nondo kuna CCTV Camera inayorekodi matukio eneo hilo, lakini pia katika purukushani za patashika nguo kuchanika simu ya moja ya watekaji ilianguka chini, na hivyo vyote amepewa Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Magufuli.

Wakuu hii ina maana wasiyojulikana kwa mara nyingine watajulikana, na ni suala la muda tu kama kuna hata mmoja alifanikiwa kurekodi tukio hilo video zitaanza kusambaa.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Swali la muhimu ni kwamba tutaona watu hawa wakifikishwa kwenye mikono ya sheria, au Jeshi la Polisi litatulia bati kama ilivyokuwa kwenye utekaji wa bonge ambako wameshindwa hata kutoa majina tu ya wale watekaji wakati picha zao zinaonekana!

Au ndio ataambiwa tena kuwa alijiteka, walikuja ndugu zake wakafanya igizo! Ila polisi wa TZ mna sehemu yenu mbinguni kwa sir God!
simu ya polisi inakabidhiwa polisi hii nchi raha sana
 
Back
Top Bottom