#COVID19 Inasemekana kirusi cha COVID-19 aina ya Delta kimeingia Mwanza

#COVID19 Inasemekana kirusi cha COVID-19 aina ya Delta kimeingia Mwanza

Mars 12

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2021
Posts
221
Reaction score
349
Niliandika kama mara 4 hivi kuhusu COVID-19 sasa wanaiita Delta Variant. Nikaandika kiufupi tu kuwa hatuishi kwenye dunia ya peke yetu, nikaendelea kuhusu ugonjwa huu kuingia nchini kutoka Uganda, hakuna aliyejali.

Sasa leo ITV wametangaza upungufu wa oxygen Bugando. Niliomba Serikali yetu tukufu ipige marufuku mikusanyiko yote mipirani, mikutanoni na hata kwenye mazishi, misiba, harusini, mikutano ya hadhara ya kisiasa na kidini n.k. Nikaandika hilo gonjwa la COVID-19 au Delta Variant linateketeza wenzetu Uganda, bado watu hawaamini.

Sasa hayawi hayawi yamekuwa. Nilishangaa sana na hata kupigiwa simu na marafiki zangu waliopo nje ya nchi wakishangaa sana kuona mechi ya Simba na Yanga kujaza watu wote wale elfu 55 sio maskhara. Narudia tena kutoa wito kwa wahusika kupiga marufuku mikusanyiko ya watu. Jamani jamani tunaishi dunia hiyo hiyo ya wenzetu tena waafrika wanaoathirika na kuteketea.

Tulete chanjo ya Pfizer kupitia mahospitali binafsi na ya serikali. Anayetaka achanje asiyetaka shauri lake ila tutashindwa hata kwenda sokoni na hizo jezi za Yanga na Simba zitageuka sanda.

EEH ALLAH TUNUSURU NA WANUSURU WAJA WAKO WOTE AFRIKA NA DUNIANI.SISI TUNAKIRI MBELE YAKO KUWA TUNAISHI KATIKA DUNIA HIYO HIYO WANAOISHI WENZETU ULIYOIUMBA WEWE MTUKUFU PEKEE. AMEEN.
 
Ila Tanzania masihara ni kubwa mno kuhusu Corona. Omba Tu Mungu isikupitie au kupitia wa karibu yako au ndugu ndiyo utajua machungu yake. Sitaki kukumbuka madhara ya hii Corona kwenye ukoo wetu na majirani kadhaa. Rest in Peace my people.
 
Hakuna cha DELTA VARIANT wala .DELTA FORCE 3

Mtuache jamani nyie kama mnanufaika na corona hamieni huko ilipo mkapige pesa.

1. Wimbi la kwanza China
2 . Wimbi la Pili South Africa
3 . Wimbi la tatu India
4. Wimbi la nne.........

TUACHENI JAMANI DAH !!
 
Watambue wanaoturudisha nyuma kwenye kujihadhari na ugonjwa huu:


IMG_20210706_211331_804.jpg
 
Hali imeshakuwa mbaya tena, tunarudi kule tulikotoka, hii hali ingekuwa inachukuliwa hatua mapema tungekuwa tunaiepuka, tatizo letu tumekuwa watu wa kuzubaa kama nchi hata kama tukisikia tatizo liko kwa jirani, matokeo yake tunaanza kuhangaika dakika za mwisho.
 
Ila Tanzania masihara ni kubwa mno kuhusu Corona. Omba Tu Mungu isikupitie au kupitia wa karibu yako au ndugu ndiyo utajua machungu yake. Sitaki kukumbuka madhara ya hii Corona kwenye ukoo wetu na majirani kadhaa. Rest in Peace my people.
Yaani Kuna majinga ya magufuli wanaichukulia simply sana Covid19, me ilimpata ndugu yetu, Ni hatari kabisa,
 
Aliyekwambia covid imetua mwanza leo nani? tangu wiki tatu zilizopita kuna cases za watu wanaopata mafua na kupoteza uwezo wa kuhisi harufu, labda kama wewe ndo umeona jambo geni. Karibu mwezi mzima wizara imeshatoa tahadhari za watu kujikinga na covid, au unataka waje wakufunge pingu za miguu. Aliyekwambia chanjo ya mabeberu ya Pfizer ndo itakulinda na kifo ni nani........yaani ulivyokurupuka kuleta hii taarifa ni kana kwamba kuna jambo geni...
 
Back
Top Bottom