Inashangaza: Watu wanamuomba ruhusa Rais Magufuli, badala ya kupewa wanatumbuliwa

Inashangaza: Watu wanamuomba ruhusa Rais Magufuli, badala ya kupewa wanatumbuliwa

Victoire

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2008
Posts
24,386
Reaction score
57,588


Nimejiuliza, Rais wetu mpendwa alipokuwa Mwalimu pale Sengerema Secondary School, alipoomba Ruhusa ya kwenda kugombea Ubunge kule Biharamulo. Je, aliachishwa kazi? Watu wanaomba ruhusa ili wakajaribu bahati zao, badala ya kupewa ruhusa wanatumbuliwa. Hii mnaionaje raia?

Binafsi naona sio sawa jamani au kwa vile ni nafasi za kuteuliwa? Najiuliza wale wa kwenye Sector zisizo za kuteuliwa i.e Watumishi wengine mfano walimu n.k wakiomba ruhusa nao wataachishwa kazi badala ya kupewa ruhusa. It means ukishindwa imekula kwako.

Hii ndo Tanzania ya Magufuli.
 
Miaka ya 2000 mwanzoni ilitoka sera sijui sheria, ukiwa mwajiriwa ukaamua kuonesha nia kazi unaondolewa.

Namkumbuka dada roz pale mbeya aliingia kugombea kupitia cuf kazi ikaishia na ubunge kakosa.

Labda wamepunguza makali
 
Miaka ya 2000 mwanzoni ilitoka sera sijui sheria, ukiwa mwajiriwa ukaamua kuonesha nia kazi unaondolewa.

Namkumbuka dada roz pale mbeya aliingia kugombea kupitia cuf kazi ikaishia na ubunge kakosa.

Labda wamepunguza makali
Ilikuwaje Magufuli alipoenda Biharamulo akashindwa kura za maoni then akarudi kushika chalk? What about Dr Mwele mwaka 2015 aliomba ruhusa kwenda kugombea Urais aliposhindwa akarudi kwenye ukurugenzi wake?
 
Bashite alivyo mwoga , nawaza jinsi anavyo kosa usingizi
Nimejiuliza,Rais wetu mpendwa,alipokuwa mwalimu pale Sengerema secondary school,alipoomba Ruhusa ya kwenda kugombea Ubunge kule Biharamulo je aliachishwa kazi ?Watu wanaomba ruhusa ili wakajaribu bahati zao,badala ya kupewa ruhusa wanatumbuliwa. Hii mnaionaje raia?
Binafsi naona sio sawa jamani au kwa vile ni nafasi za kuteuliwa...
 
Kama ni kwa wale wanafasi za kuteuliwa na mimi namuunga mkono Magufuli, kwenda kuomba nafasi ya ubunge wakati wewe unajua kuwa Rais alikuteua kuwa RC, DC, IGP na nafasi zingine za kuteuliwa ni kumkosoa na kumdharau Rais kuwa alifanya makosa kukuteua katika nafasi ulionayo.

Nafasi yako ulitakiwa uwe mbunge au nafasi nyingine, kama sivyo basi walitakiwa wakatae mapema nafasi za kuteuliwa wabaki kwenye nafasi zao za awali au wasubiri kazi wanazoona zinawafaa wao.
 
Back
Top Bottom