Inatumika nguvu kubwa sana kuishusha Simba

Inatumika nguvu kubwa sana kuishusha Simba

Unalialia nini tena? Haya usilie tutawakataza kusifia Yanga sawa eeh...
Unaposema simba inashushwa na Yanga inapandishwa una maana gani?
Yanga ni timu kubwa, iko juu haina haja ya mtu kuipandisha popote.
Yanga tunacheza uwanjani, matokeo yanajieleza. Mmezoea kucheza mdomoni, ndiyo maana mnajiona mnashushwa.
 
Unalialia nini tena? Haya usilie tutawakataza kusifia Yanga sawa eeh...
Unaposema simba inashushwa na Yanga inapandishwa una maana gani?
Yanga ni timu kubwa, iko juu haina haja ya mtu kuipandisha popote.
Yanga tunacheza uwanjani, matokeo yanajieleza. Mmezoea kucheza mdomoni, ndiyo maana mnajiona mnashushwa.
Hatujakataa yanga kusifiwa, ila ni uzwazwa kuisifia yanga at the same time kuiponda simba ambazo hata ukiziweka kwenye mzani mmoja kimataifa simba ni heavy weight kwa yanga na timu nyingi under the saharan desert.
 
Duuh mbona unajitesa namna hii bure? Haujui mpira wa miguu unabadirika?

Kuna aliyebisha Simba haikuwa Bora hiyo miaka minne ya nyuma?

Huioni Yanga Kwa Sasa ndio timu Bora hapa nchini Tanzania??
Mtoke huko shirikisho mje cl
 
Kama hawawezi ku-recognize yanayo fanywa na simba ni bora wakakaa tu kimya sio kulazimisha Simba ionekane mbovu na Yanga kuwa bora hali ya kuwa uhalisia haupo hivyo
So wewe kila ukiona mtu kwenye TV anaongealea mpira unajua ni mchambuzi
 
Hatujakataa yanga kusifiwa, ila ni uzwazwa kuisifia yanga at the same time kuiponda simba ambazo hata ukiziweka kwenye mzani mmoja kimataifa simba ni heavy weight kwa yanga na timu nyingi under the saharan desert.
Pole unaonekana unauchungu sana
 
Kuna mchambuzi mmoja wa redio kwa mihemko yake akauliza eti kwani hao simba walishindwa nini kushiriki cafcc kama kule cafcl wanaona ni kugumu? Nilipigwaa na butwaa ajabi.
 
Ndugu mbumbumbu jiulize maswali ya Msingi kabla huja sukumwa na hisia.
Jiulize msimu uliopita na msimu huu timu gani zilizokua zikitarajiwa kumpa changamoto Yanga na Matokeo yalikuaje?

Jiulize una misimu mingapi hujapata matokeo Kwa Yanga.
Jiweke Neutral angalia kikosi na bench laufundi la Yanga vinafanana na timu Yako?
Kama Yanga anabebwa na Marefa ndio Sababu ya kufanya vizuri, je! Kimataifa ambapo anafanya vizuri bado anabebwa na Marefa?
Kwa aina hii ya ushabiki nikopamoja na wadau wanao taka Lage ajengewe mnara [emoji3][emoji3]
Hahaaaa uto bhana umeelewa uzi? Viwango vinavoongelewa ni vya ukanda wa cecafa na afrika kwa ujumla.
 
Kuna mchambuzi mmoja wa redio kwa mihemko yake akauliza eti kwani hao simba walishindwa nini kushiriki cafcc kama kule cafcl wanaona ni kugumu? Nilipigwaa na butwaa ajabi.
Kuanza sasa ntakua naangalia mechi tu, naachana na uchambuzi
 
Kwani shida iko wapi wakisema Yanga ni bora kuliko simba, halafu ukweli ukawa simba ni bora zaidi kuliko Yanga?

Acha kuutesa moyo wako kwa mambo madogo madogo.
Shida ni kwamba kuna watu wanabeti huko kwa kuwasikiliza wachambuzi ambao kwa kiasi kikubwa wanapotosha
 
Malalamiko yameanza tena! Sijui ni homa tu ya tarehe 16 ya Mwezi huu wa 4!! Maana siku zinakimbia kweli kweli.

Au ndiyo ameanza kutafutwa mchawi? Ili siku hiyo baada ya timu fulani kushushiwa kipigo cha mbwa mwizi, ionekane ni hiyo project fake ndiyo imesababisha!!
Ngoja mtembee na matokeo mfukoni. Mtafumliwa hadi mtapike mihogo , ugali na sukari ya Heris
 
😂😂 aisee maisha ni magumu sana ukiangalia vile jirani anapata riziki yake wewe una changamoto unaanza kisirani

Rizki haiwezi kukunyookea muda wote usipate changamoto, na wengine wanahitaji hicho unachokipata wakipata usione umetengwa (kwanini yeye apate mi nikose) subra kitu Cha msingi.

Kuna siku Azam nae atakuja vizuri. Makosa ya uwanjani Kila sehemu yapo ila mkuu unaangalia ya sehemu Moja

Upande wa wachambuzi wapo ndio wanachangamoto hiyo ya kuonesha ushabiki mf. Wachambuzi wa efm (wawili) Hawa nao Kuna muda wanasema ukweli ila Kuna muda wanaegemea zaidi upande mmoja
Sasa aliye na riziki nzuri nani hapa.Yani tufananishe jeans na pajama?wakati mwenye pajama aliipata pajama baada ya jeans kumchana mapajani.Hebu kueni makini.
 
Habari wakuu

Jana asubuhi niliangalia kipindi cha Viwanjani kinachorushwa kwenye chaneli ya Azam sports 1HD na binafsi nimesikitishwa sana kwa niliyo yaona.

Sijui kama nitakuwa sahihi nikisema kwamba kuna project imeandaliwa ya kuishusha Simba ili ipandishwe Yanga, sina uhakika ila ndicho ninachokiona.

Kampeni hii inaonekana ni endelevu na ni long term project ambayo ilianza msimu uliopita na inaendelea msimu huu, kwanini nasema hivyo;

Msimu uliopita wakati ndugu zetu wakiwa na miaka 4 bila ubingwa, tulishuhudia one of the most dramatic seasons of all, Yanga ilibidi awe bingwa kwa hali na mali wenyewe wanasema iwe jua iwe mvua, na ndipo ikazaliwa Unbeaten ya mechi 49 lakini cha kustaajabisha kama sio kuhuzunisha kwenye hiyo unbeaten yao walifungiwa marefa wasiopungua wanne.

Labda ndugu zangu wana simba niwakumbushe mechi ya Yanga na Namungo ilipigwa kwenye uwanja wa Ilulu pale mkoani Lindi, mechi iliyozua malalamiko chungu nzima, ilikuwa ni baada ya Yanga kupewa penati ya uongo dk za mwishoni ambapo Namungo alikuwa mbele kwa goli 2-1 penati iliyopigwa na Saido Ntibazonkiza na kuisawazishia Yanga na mchezo kumalizika kwa draw ya goli 2-2.

Haiku ishia hapo iliendea kwenye michezo mingine mingi iliyofuatia, kila ambapo Yanga akitanguliwa kipindi cha kwanza basi kipindi cha pili inazuka penati yenye utata na Red card kwa mpinzani, sijazungumzia makosa ya kibinadamu ya kujirudia rudia kwa makipa wa timu pinzani wanapo kutana na Yanga.

Pia tuachilie mbali ahadi ya fedha kwa kigezo cha hamasa kwa wapinzani wa Simba hali iliyo pelekea kuchezewa rafu mbaya na kupata majeruhi wengi na kudhoofisha timu, mfano mzuri ni ile mechi na Dodoma jiji ambayo ilitoa majeruhi wengi kwa upande wa Simba wakiwemo Pape Ousmane Sakho, Thadeo Lwanga na Kennedy juma ndani ya mechi moja.

That was a by the way, turudi kwenye mada husika, katika kile kipindi cha viwanjani yali jadiliwa mafanikio ya Yanga msimu huu kwenye Kombe la Shirikisho barani Africa na alimwagiwa sana maua, pongezi zikaenda kila mahali hususani kwa viongozi ambao ni GSM.

Tatizo likaja walipoanza kuizungumzia Simba, mmoja wa wachambuzi nisingependa kumtaja jina alionesha chuki za wazi, hoja hana yaani aligeuka shabiki ghafla anabisha mpaka wenzie aliyekuwa nao wanamcheka.

Anadai Simba mbovu, kutinga robo fainali ya CAFCL ni bahati tu amekutana na mpinzani dhaifu akamfunga nje ndani, kumbuka ni huyo huyo amemsifu sana Yanga kwa kumfunga Tp mazembe nje ndani akasahau sababu ya Mazembe kuwepo kombe la shirikisho ni Vipers ambaye amefungwa na simba anayo iita mbovu nje ndani.

Ndugu mchambuzi hakuishia hapo akaongeza kwa kusema kuwa Simba pia imebahatisha kumfunga Horoya goli 7 kwa sifuri, anazungumza haya sio katika hali ya kiuchambuzi tena, anabisha bila hoja misuli ya shingo ime msimama [emoji23][emoji23].

Aanachosema yeye ni Simba mbovu na kusema kuwa Yanga itafika mbali kuliko Simba bila kujali ugumu wa mashindano aliyopo Simba, wapinzani wagumu anaocheza nao Simba ukilinganisha na Kombe la Shirikisho.

Hili lilizidi kuwa chekesha aliokuwa nao kwenye kipindi na kumuona kituko, waka muuliza inamaana Simba haikustahili kushinda hata kwenye mechi ya kwanza kule Guinea, maana Simba aliukamata mchezo kama isingekuwa kukosa umakini kwa straika John bocco, simba ingetoka na sio chini ya mabao matatu, majibu hana anajikanyaga kanyaga tu.

Sio yeye tu wapo wachambuzi wengi tu wa kaliba yake, Simba mbovu umekuwa ndio wimbo halafu Simba hiyo hiyo mbovu ndIo inawakilisha nchi kwenye mashindano makubwa zaidi kwa ngazi ya vilabu barani Afrika CAFCL, ndio timu pekee ukanda wa CECAFA na ni miongoni mwa timu mbili kutokea Kusini mwa Jangwa la Sahara yani Simba na Mamelodi Sundowns kufuzu hatua ya nane bora.

Wanacho kifanya ni sawa sawa na kusema, kwakuwa Al Ahly ame-struggle kupita makundi ya CAFCL basi Future FC ambayo ipo shirikisho ni bora kuliko Al Ahly, wakuu ina tumika nguvu kubwa sana kuishusha Simba ili Yanga ionekane bora. Kuna mchambuzi pia aliandika Twitter akidai kuwa kwa ilichofanya Yanga msimu huu kwenye Kombe la Waliofeli ndio klabu bora zaidi ukanda wa CECAFA na kudai kuwa TUJIVUNIE [emoji23][emoji23].

Kwa miaka 5+ ya hivi karibuni Simba imepambana sana kuijenga brand yake Afrika na Duniani kiujumla na kupata mafanikio chungu nzima, tunavyozungumza sasa, Simba ni miongoni mwa timu 10 bora zaidi barani Afrika na kwa kuthibitisha hilo, baadaye mwaka huu Simba ita shiriki kwenye CAF Super League ambayo itafanyika kwa mara ya kwanza kabisa barani Afrika.

ni dhahiri watu hawa pendezwi na hili, na ndio maana baada ya Yanga kufanya vizuri kidogo kwenye kombe la mbuzi msimu huu, tayari anaveshwa ukubwa ambao hana, tena wana kwenda mbali zaidi wakisema ndio timu bora zaidi ukanda wa CECAFA.

Nguvu moja [emoji881]
Taja huyo mtangazaji tumjue kwani unaogopa nini
 
Back
Top Bottom