Uchaguzi 2020 Inavyoonesha CHADEMA na ACT-Wazalendo hawataungana. Nini kimekwamisha?

Uchaguzi 2020 Inavyoonesha CHADEMA na ACT-Wazalendo hawataungana. Nini kimekwamisha?

Mkuu tuongee uhalisia hivi unaachiwa vipi kitu ambacho tayari una udhibiti nacho?
CDM wanawezaje kusema wana waachia ACT majimbo ya Zanzibar wakati ukweli ni kwamba wanajua hata kama CDM wakiweka mgombea wao hatamshinda wa ACT?

Bara nako CDM wanasema watawaachia ACT mikoa ya pwani ambako tayari kila mtu anajua ACT au CCM watashinda.

Huu muungano ni wa kuifaidisha CDM tu kiuhalisia hasa hapo kwenye kuachiwa majimbo mengi bara na kuachiwa uraisi wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania.
Muungano lazima uoneshe kila mtu anatoa kitu flani siyo yeye anapokea tu na kuongezewa alichonacho na mwenzie haongezewi kitu.

Niwashauri kama wana nia ya dhati ya kuungana basi waachiane hivyo walivyopanga lakini atakaepewa uraisi wa Jamhuri na kushinda basi ateue wabunge wote wa viti maalum vya raisi toka chama kingine kilichokubali kuachia uraisi, pia waziri mkuu atoke chama kilicho achia (kama katiba ina ruhusu) au wagawane nafasi baraza la mawaziri 50/50.

Hii kamari niliyo pendekeza ni kama tu kweli wanajiamini yupo wa kumshinda Magufuli miongoni mwao.
Mimi hiyo Ni proposal yangu binafsi tu, nikimaanisha vyama viachiane sehemu ambazo vina nguvu kuliko kugawana kura na kuipa advantage CCM

Hata kura moja tu inaweza kuleta tofauti Kati ya mshindi na mshindwa, so usije ukasema eti ACT tayari wapo guaranteed kushinda majimbo fulani hivyo hawahitaji ushirikiano, maana Chadema wanaweza kusimamisha mgombea hata akapata kura 2 ambazo zingeenda ACT na ikawa ndio zimemuangusha mgombea wa ACT
 
Isome vizuri katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977
Badala ya kumwambia aisome katiba kwanini usitueleze direct kuna kitu gani.
Unataka aanze kusoma vifungu na vipi kama hajui kuvitafsiri. Ikishindikana kabisa taja kifungu na ibara.
 
Baada ya kumuona Membe amechukua fomu ya Urais meo, nimehitimisha hakuna kuungana Kati ya Chadema na ACT licha ya vyama hivyo kupigia debe suala hili kabla hata ya mchakato wa uchaguzi

Nilitarajia Chadema kuwaachia ACT majimbo yote Zanzibar na Urais na majimbo ya ukanda wa Pwani ambako CUF ilikuwa na nguvu kabla ya kumeguka, na ACT walipe fadhila kwa kuinga mkono Chadema kwenye Urais wa Muungano

Nilimsikia Mbowe na Tundu Lissu wakitamka kuwa japo wamesimamisha wagombea nchi nzima na Zanzibar walikuwa tayari kuwaondoa baadhi ya majimbo kwa Sababu walikuwa kwenye mazungumzo na ACT,

Je, ni nini kimekwamisha Muungano huu?
Uroho wa madaraka na uroho wa Ruzuku
 
Tulieni..... membe hatarudisha form na kumwachia Tundu Lissu
 
Badala ya kumwambia aisome katiba kwanini usitueleze direct kuna kitu gani.
Unataka aanze kusoma vifungu na vipi kama hajui kuvitafsiri. Ikishindikana kabisa taja kifungu na ibara.
Kama huyo jamaa hawlewi hilo takwa la Kikatiba basi hasaidiki hata akiwekewa Ibara husika hapa. Kwamba hajui huwezi kuwa na mgombea Urais na Mgombea mwenza toka sehemu moja ya Muungano?
 
Chadema walikuwa wanalazomisha kuwa mgombea lazima atoke kwao!!! ACt wakagoma
 
Baada ya kumuona Membe amechukua fomu ya Urais meo, nimehitimisha hakuna kuungana Kati ya Chadema na ACT licha ya vyama hivyo kupigia debe suala hili kabla hata ya mchakato wa uchaguzi

Nilitarajia Chadema kuwaachia ACT majimbo yote Zanzibar na Urais na majimbo ya ukanda wa Pwani ambako CUF ilikuwa na nguvu kabla ya kumeguka, na ACT walipe fadhila kwa kuinga mkono Chadema kwenye Urais wa Muungano

Nilimsikia Mbowe na Tundu Lissu wakitamka kuwa japo wamesimamisha wagombea nchi nzima na Zanzibar walikuwa tayari kuwaondoa baadhi ya majimbo kwa Sababu walikuwa kwenye mazungumzo na ACT,

Je, ni nini kimekwamisha Muungano huu?
Huu ni mtego mkali wa panya...CCM kwa sasa hawajui wapange mikakati ipi kupambana na yupi kati ya Membe na Lissu. ...usisahau zenji kuna mzee wa sawa sawa!!

Tume na Police hebu tuachieni hili game tuishangaze dunia.
 
Hawa jamaa walipaswa kumuweka Membe kama mgombea Mwenza na Lissu Rais....Kampeni zisingeshikika
Katiba hairuhusu hilo,mgombea mwenza lazima atoke Zanzibar ndio maana salum mwalimu kuchaguliwa kuwa mgombea mwenza wa Lissu
 
ACT kama NCCR wanataka waachiwe majimbo wayauze kwa ccm, lakini wanataka CHADEMA ikishinda wagawane ruzuku kwasababu eti iliwaachia majimbo.

Kwa msingi huo, Kila chama kipambane kivyake, ili kila mmoja avune alichopanda.
Waungane ili iweje?!

Malalamiko yao ilikuwa kwamba, wakati wa UKAWA Chadema iliwatumia, sasa unadhani hiyo dhana itawaisha?!

Waliionea wivu CHADEMA na kuanza kuihujumu kwa kupeleka uongo huko ccm ,kwasasa kila mtu aende kivyake.

Ukipigwa, ujue ulipigwa kihalali, na ukishinda tembea kifua mbele.

ACT ikishinda Zanzibar haita share madaraka na yeyote, kila mmoja aweke nguvu anapoona anakubalika. Hakuna haja ya kuungana kisha muanze kuoneana wivu na kuanza kusalitiana.

Akishinda sawa, na ukishindwa usilaumu muungano wala nini ukae mbali.

CCM hawataki kuungana na chama chochote, kwanini nyie muungane?!

Walipaswa waungane 5 yeas kabla ya uchaguzi, lakini sio wiki moja kabla ya uchaguzi, hii itawaletea shida.

Kila chama kipige push up zake. Kikapambane kivyake, wengi wanafiki.
Hasa Mbatia na Zitto ni wanafiki sana.

Mbatia anajiona bonge la mwanasiasa, na alijiona kaibeba CHADEMA alipokuwa UKAWA.

Zitto hakutaka UKAWA akiamini angeweza bila UKAWA, leo muungano wa nini?

Lipumba wote mnafahamu alivyo msaliti na kaishiwa hana cha kuchangia kwenye muungano, hivyo aachwe, hata asijadiliwe.
 
Membe keshachukua fomu, NEC watamuweka kwenye karatasi ya kura
Ni hadi arejeshe ndiyo anaingia kwenye list ya wagombea. Kumbuka unaweza kuchukua form ukajaza vibaya ukatupwa nje, hivyo baada ya kurejesha form iliyokamilika ndipo unaingia kwenye orodha. Kuchukua tu siyo hoja.
 
Hawa jamaa walipaswa kumuweka Membe kama mgombea Mwenza na Lissu Rais....Kampeni zisingeshikika
Ili Membe awe mgombea mwenza lazima aache uanachama ACT na kujiunga CDM. Kumbuka Juma Haji Duni wa CUF 2015, aliondoka CUF na kujiunga CDM ndipo akawa mgombea mwenza wa Mzee White hair.
 
Dah...CM yupo kikazi...TL ametumwa... what do you think? [emoji2960]
 
Nafikiri bado mazungumzo yanaendelea na ni vizuri kila mgombea akachukua fomu yake lakini bado yawezekana akajiondoa na kumunga mkono mgombea wa chama mshirika. Na ndivyo itakavyokuwa, msihofu.
Hivi itakuwa vyema kama nguvu ya ACT na Chadema ikawa moja.
 
Back
Top Bottom