Inawezekana vipi Taifa linampata Rais kama huyu?

Behaviourist

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2016
Posts
39,926
Reaction score
95,626
Katika kipande kifupi cha video hapo chini Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika Mkutano na wadau wa Demokrasia hivi leo ametoa hotuba inayoshangaza sana.

Anasema kuwa Rais akitoa kibali cha mikutano ya hadhara, Chadema wanaenda kuvunja vunja Magari pamoja na mali nyingine za uma ndiyo maana hatoi vibali vya MikutanoπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Nimejiuliza maswali mengi sana.Tokea lini Rais akawa na haki au wajibu wa kutoa vibali vya Mikutano kwa vyama vya siasa?Hata kama ni kweli kuwa vyama vya siasa vikipewa vibali vya mikutano ya hadhara vinafanya fujo na kuharibu mali za uma,sheria za kuwadhibiti si zipo?

Mikutano ya vyama vya siasa ipo kwa mujibu wa Katiba na sheria zetu na wala siyo kwa mujibu wa Rais.Sasa leo Rais anadai kuwa yeye ndiye mtoa vibali.WTF!!!πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Ameenda mbali zaidi na kudai kuwa vyama vya siasa vikipewa vibali vya Mikutano vinaenda kuvunja vunja Magari pamoja na mali nyingine za ummaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Kuna mtu yeyote hapa ambae ana ushahidi wa Chadema au chama chochote cha upinzani kuharibu mali za uma katika mikutano yake ya kisiasa kama anavyodai Rais?

Haya mambo yamenishangaza sana.Ni maajabu makubwa kwangu mimi.Yanafikirisha pia, lakini cha zaidi ni kwamba yanachekesha sana.
Your browser is not able to display this video.
Your browser is not able to display this video.
 
Huyu Rais asijitie kiburi cha kupitiliza, akumbuke yaliyompata mtangulizi wake!

Kutokana na kiburi cha Mwendazake, hivi sasa anamuangukia Mola, ili awe kiongozi wa malaika!
 
Utawala wa huyu Mzanzibar utasababisha hata ccm wenyewe waone umuhimu wa katiba mpya. Wasipofanya hivyo Zanzibar wana njia rahisi sana ya kutawala Tanzania. Wataacha Mtanganyika ashinde uchaguzi then akifa wao wanamalizia awamu
 
Kwani uongo ? Wapinzani wa Tanzania Wana vurugu hatari na matusi Yaani dizaini ya mdude nyangali . Jazba kibao hawana ustaarabu.

Alafu mbona kaongea kawaida tu kuelezea hali inavyokuwa 🀣 . Yaani ulivyoongea kwa jazba sipati picha ndio upo barabarani kwenye maandamano yenu yale si utatuvunjia magari wewe ? πŸ˜ƒ

Mimi Sina chama.
 
Mh. Rais wetu Samia hana shida tatizo ni Sisi kujaribu kumpima kwa kumlinganisha na Hayati Magufuli.Isitoshe ni muda mfupi sana kusema kitu kwani pia ni nafasi aliyoshtukiziwa sana, tuwe na subira angalau baada ya miaka miwili tunaweza kuongea kitu. TUMPE MUDA SAMIA SULUHU HASSAN, MHE. RAIS WA JMT
 
Nadhani hujamsikiliza uzuri Mhe. Rais mama yetu. Hakuna sehemu amesema Rais akitoa kibari. Tusimlishe maneno. Kauli nayo isikia hapo katika clip uloweka kasema "Unatoa kibari kafanyeni Mikutano..." Turudi darasani neno Unatoa... ni nafsi ya ngapi? Inawakilisha nini? Angetumia neno..."ninatoa kibari"....hapo sawa ni nafsi ya kwanza.
Hivyo Rais ametumia neno "Unatoa kibari..." kama nafsi ya pili, ambayo inawakilisha mtoa kibari!
Sikiliza kwa umakini, utaelewa.
 
kama hawezi aachie ngazi
 
Kwanini upoteze kuangalia hotuba za marais wa Tz!, fanya kama mimi nunua bando tafuta pornstar mmoja umuangalie kuliko kusikiliza hizo hotuba zao.
 
Hatuwezi kumpa muda zaidi Rais ambae anavunja sheria za nchi yetu pendwa kila kukicha.

Leo anatamba mbele ya uma kuwa ni mtoa vibali vya mikutano ya vyama vya siasa. Pia anadanganya uma kuwa vyama vya siasa vikipewa vibali vya mikutano ya hadhari vinaenda kuvunja vunja magari pamoja na mali nyingine za uma badala ya kufanya mikutano na ndiyo maana hatoi vibali hivyo.

Hii maana yake ni kwamba tukiendelea kumchekea chekea kesho ataamka na kubwa zaidi la kuiangamiza nchi yetu pendwa.

Kama CCM mmebadilika kuwa matahira pisheni wenye uwezo wa kuongoza waongoze nchi yetu pendwa.
 

Kwani Nani aliwaambia muivamie Zanzibar? Haya ndiyo matunda ya Uvamizi , mumelikoroga sasa mtalinywa
 
Rais awe makini na wanaomzunguka, hii ngoma ya Mh. Mbowe aicheze kwa akili vinginevyo itamlipukia..iwe balaa kwake.

Hii nchi ni kubwa mno, ikitokea jambo ni kazi sana kulizuia..watu wamejaa vifua wanagonja tu wapate pa kupumulia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…