Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Naona hapa Kuna mtu/kiongozi anatafutwa Ili kutupiwa lawama (Nyerere). Je, DR Congo nao pia ni misingi mibovu Yao iliyowekwa toka uhuru?
Je, hiyo misingi mibovu haiwezi kurekebishwa?

Note: Nakubaliana na wanasema "akili" ndiyo msingi wa Kila kitu.
Na sababu pekee ni kwa sababu Nyerere ni Mgalatia. Angekuwa mvaa kobazi wala usingeisikia hiyo kauli!

Hili siyo suala la Tanzania pekee. Ni suala la mtu mweusi dunia nzima!
 
Nani ambaye alikuwa ameshafika Ulaya na Afrika kwa wakati huo na kulinganisha viwango vyao vya kimaendeleo?

Na hii inahusianaje na comment yangu uliyoikwoti? 😳
Mkuu, nilichomaanisha hapo ni kuwa ikiwa tulichofundishwa kwenye historia ina ukweli, basi ni kwamba kuna wakati, hasa karne ya 15, ambapo Waafrika na Wazungu walikuwa na maendeleo na changamoto zinazolingana (lakini siamini, ila nilikuwa nikijibu hivyo mitihani kwa kuwa ndivyo nilivyoelekezwa na Mwalimu).

Na kuhusu swali kama kuna aliyefika Ulaya na Afrika kwa wakati huo, inafahamika kuwa kufikia karne ya 15, Wazungu walishaanza kufika barani Afrika, ila sina uhakika kama wao
chanzo cha taarifa inayolinganisha maendeleo ya Afrika na Ulaya kwa kipindi hicho.
 
Nchi Ina miaka 60 ila mnataka maajabu ya kiuchumi?
Singapore ni mdogo wetu🤣.
Ana miaka 58 toka apate uhuru wake ila unamuonaje?
Sisi hata tupewe miaka 1000 kwa akili zetu tutakua hivi hivi
 
Kama ni model za uzalishaji tuliaga za China but why chines wakafanikiwa kuliko sisi,sote tulikuwa hatuna technology na maarifa?
China kwa miaka mingi walikuwa kwenye uchumi duni kabisa.

Maendeleo ya China, kwa kiasi kikubwa yameanza miaka ya 1990 baada ya kubadilisha kabisa mifumo yao ya uchumi. Mifumo yao ile ya kale ambayo tuliiga haikuwafikisha popote.

Ni uwekezaji mkubwa wa makampuni ya Ulaya na America uliofanyika kianzia miaka ya 1990, ndio uliobadilisha hali ya China, japo mpaka leo, kwenye maendeleo ya watu, China ingali chini, ni nchi ya 89, ndiyo maana unaona wamezagaa Dunua nzima kutafuta maisha. Mapato ya nchi ni makubwa sana lakini mapato ya raia bado ni duni.
 
Ugali uongo daa we jamaa [emoji2][emoji75]

Sent from my Pixel 3 using JamiiForums mobile app
 
Sababu za kuufunga Ubalozi.
Kuufunga ubalozi wa Denmark nchini ni process iliyoanza mwishoni mwa mwaka 2020 baada ya Denmark kutoridhishwa na mwenendo wa Tanzania kutoheshimu demokrasia na haki za raia, ambao ndiyo msingi mkuu wa sera za mahusiano ya nje ya nchi zote za Nordic, ikiwemo Denmark.

Mwanzoni mwa 2021, walipunguza majukumu ya ubalozi wa Denmark nchini, na kuhamishia Nairobi, na walisema kuwa wangefunga ubalozi wao moja kwa moja mwaka huu. Kwa hiyo ni utekelezaji wa mambo yaliyokuwa yameamliwa tangu 2020 baada ya uchaguzi.

Ukumbuke kuwa kati 2016 mpaka 2020, mataifa ya Ulaya, ikiwemo Denmark yalipunguza sana misaada yake kwa Tanzania, na kusema misaada pekee ambayo wangeendelea kuitoa ni ile ya huduma ya afya ya mama na mtoto, hasa kwenye masuala ya chanjo. Uporaji wa ushindi wa Maalimu Seif kule Zanzibar, na mambo yaliyoendelea huku bara baada ya uchaguzi wa 2015, vyote kwa pamoja vilichangia kwa kiasi kikubwa kwenye hili. MCC waliamua kufunga ofisi yao Tanzania baada ya notisi ya mwaka mmoja, nao wakielezea sababu hizo hizo.
 
Najaribugu kuwaza watu weusi tulikosea wapi ili tusamehewe sipaoni Kuna watu humu humu saivi wanalaumu uongozi mbovu..
Ndani ya nchi yetu as if wakipewa wao nafasi watanyoosha mstari

Yani hata wapate hizo nafasi Mambo yatakuwa Yale Yale hayatobadikika ukifikiria sana inatia hasira ila unabaki kucheka..
Sijui labda mwenyezi Mungu ashushe malaika ndo aje atuongoze[emoji3]

Sent from my Pixel 3 using JamiiForums mobile app
 
Hata mim naamini tumewekewa li ugali kichwani mkuu.
Honestly ukifanikiwa kuona namna hawa watu wanaendesha maisha yao kwa descpline kuanzia raia mpaka viongozi halafu ulinganishe na sisi daah utaona kabisa sisi kuna nati za kichwa Mungu alisahau kuzikaza vizuri🤣.
 
Hili swali ungelipeleka kwenye muhimili wa bunge.
 
Kwani unadhani ule huwa ni ukarimu? Ile ni rushwa.
 

Hizo ni fikra tu. Hatuna uhakika kama mambo yatabakia vile vile au yatabadilika, kwa sababu hatujawahi kubadili uongozi na mifumo yake hata mara moja. Ila tu tumejazwa na imani kuwa hali itakuwa vile vile.
 
Singapore ilipata uhuru wake toka kwa Mwingereza mwaka 1963. Kwa hiyo kiumri, Tanganyika inaizidi Singapore kwa miaka miwili. Ilikuwa duni sana kiuchumi, lakini leo hii, huwezi kuilinganisha na Tanzania.
 
Labda !!
 
Tatizo letu ni elimu ya kijinga ya kuwa tegemezi kwenye ajira pekee tena za serikali na siyo ujuzi, pia hakuna uzalendo hata kidogo kutoka kwa watawala zaidi ni mafisadi makubwa na majangili yanayofunga tai na kupanda V8
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…