Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Naona hapa Kuna mtu/kiongozi anatafutwa Ili kutupiwa lawama (Nyerere). Je, DR Congo nao pia ni misingi mibovu Yao iliyowekwa toka uhuru?
Je, hiyo misingi mibovu haiwezi kurekebishwa?

Note: Nakubaliana na wanasema "akili" ndiyo msingi wa Kila kitu.

Siyo Denmark pekee. Vinchi vyote vidogo huko Ulaya, na baadhi huko Asia, ukilinganisha na Tanzania ni aibu tupu:

Denmark
Norway
Finland
Sweden
Singapore
Switzerland

Utajiri mkubwa hapa Ulimwenguni ni akili, wala siyo idadi kubwa ya fisi na pundamilia, siyo dhahabu na gas, ardhi nzuri ya kilimo, maziwa, bahari au hali nzuri ya hewa.

Hata upewe vyote, ukinyimwa akili, vyote vinakuwa havina maana. Lakini ukibahatika ukapata akili,ni mwanzo wa mafanikio yote. Kwanza utajua ni nini kilicho muhimu, utakuwa na mifumo mizuri ya kuvuna rasilimali, utakuwa na tekinolojia, utakuwa na mifumo mizuri ya utawala, na mifumo mizuri ya kusimamia uchumi kwa ujumla.

Sisi tuna vitu vingi, lakini asilimia kubwa sana ya watu wetu wamenyimwa akili, utashi na maarifa. Ndiyo maana wachache wenye akili, maarifa na utashi, ama wanakuwa frustrated na kukata tamaa au kuishia kwenda kufanya kazi mataifa ya nje kwa sababu nchini mwao ni giza nene.
 
Ni kanuni ya maisha anaetoa ndie anaebarikiwa.
Wazungu uwasaidia waafrika ili wazidi kuwa masikini zaidi,wanajua pesa zinadakwa juu kwa juu then zitarudi Tena kufichwa bank za ulaya na majizi ya Africa
Mbona na sisi tumetoa hapo Uturuki?
 
Denmark inatarajia kuufunga ubalozi wake nchini Tanzania ifikapo 2024. Ni kati ya nchi ambazo zimekuwa zikiipa Tanzania misaada, tokea ikiitwa Tanganyika hadi sasa ikiwa inajulikana kwa jina adhimu, Tanzania.

Lakini Denmark ni nchi ya namna gani?

Ukifanya ulinganisho, Tanzania imeizidi kwa mambo mengi isipokuwa ujinga na umaskini. Ina rasilimali nyingi sana kuizidi, na hata idadi ya watu tumeipita mbali sana.

Denmark, ni kanchi kadoogo, kenye ukubwa wa kilomita za mraba 42,920 lakini inaizidi kiuchumi Tanzania, nchi Kuubwa kieneo, yenye kilomita za mraba 945,087.

Denmark, ni kanchi kadoogo kenye watu milioni tano lakini inaipa misaada nchi kuubwa, Tanzania, yenye watu milioni sitini na moja.

Ni nini siri ya kanchi kadogo kuizidi nchi kubwa kama Tanzania? Imekuwa ikiisadia Tanzania tokea 1963, enzi hizo ikiitwa Tanganyika, lakini hakuna taarifa ya Tanzania ambayo ni nchi kubwa kuisaidia Denmark kanchi kadogo.

Imewezekanaje kwao lakini kwetu ikashindikana?

Mwingine anaweza kusema ni kwa sababu ya ukoloni, lakini hilo halina mashiko. Hata Korea Kusini ilishawahi kuwa koloni la Japan, lakini kwa sasa wanatukimbiza kiuchumi.

Ni nini walichogundua hao watu weupe ambao weusi wa Tanganyika na Zanzibar hawajagundua?

Angalia, hata eneo la Korea Kusini ni dogo sana ukililinganisha na ukubwa wa Tanzania. Ina kilomita za mraba 100,210 na watu milioni hamsini na moja.

Inawezekanaje kanchi kadoogo, Denmark, kuipa misaada nchi kuubwa, Tanzania?
“Ukubwa wa pua si wingi wa kamasi”
 
Aisee mkuuu una uchungu sana, mwenyewe ninaumia mno kuona ushenzi unaoendelea miongoni mwetu waafrica,

Nasemaje kwa yeyote atakayepata fursa ya kutimukia nje ya bara hili la shida hasa nch yetu hii asichezee hyo fursa.
Kila leo nawambia wanangu kuwa tafuteni fursa za kwenda Ulaya na marekeani lakini hasa Ulaya ya scandinavian countries
 
Magufuli alipotaka kuigeuza Tanzania iwe sawa na nchi za Ulaya mlimfanyaje? Mnataka maendeleo lakini hamtaki namna ya kuyafikia hayo maendeleo. Maendeleo ni malengo, nidhamu, kujitoa mhanga (self sacrifice), bidii ya kazi, uadilifu na kutambua vipaji na ubunifu na kuvitumia ipasavyo. Ulaya wameweza kuviunganisha hivyo vyote kufikia hapo walipo. Sisi hapa bado tunajitafta na akija mwenye mawazo kama hayo bado hatumwelewi. Tutachelewa sana.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Umenikumbusha!

Walianza kumtukana eti anataka tunyimwe misaada.
 
Huyo Magufuli nae ni mwehu mwingine wala sio wa kumention humu.Bora hata ungemtaja JK NYERERE ila huyo mwehu anatawala badala ya kuongoza ni kielelezo cha mfalme juha ambae alishawahi pita hapa nchini.
Kwa namna ambavyo Magufuli alikuwa anaipeleka nchi, yaani ndiyo tungezidi kuwa duni zaidi, kwa sababu alikuwa anatumia sana nguvu zaidi kuliko akili.

Wazungu wamefika mahali walipo kwa sababu ya akili, siyo nguvu.
 
Viongozi wanatokana na wanananchi. Walivyo viongozi ndo walivyo wananchi maana wanachaguliwa na wananchi, Viongozi hawashuki kutoka sehenu nyingine itoshe kusema tatizo ni wananchi wenyewe wa Afrika. Kama unabisha kwanini kama shida ni viongozi wananchi mmechukua hatua gani kuwawajibisha Viongozi??

Tatizo ni WANANCHI wa nchi husika ndo msingi maana viongozi wanatokea miongoni mwetu ata ww ukiwa kiongozi leo utapita mule mule.
Wananchi hawawajibishi viongozi wanategemea miujiza na kudra za Mungu 😀!
.... "Basi tunawaomba waheshimu katiba tu" ....
 
Naona hapa Kuna mtu/kiongozi anatafutwa Ili kutupiwa lawama (Nyerere). Je, DR Congo nao pia ni misingi mibovu Yao iliyowekwa toka uhuru?
Je, hiyo misingi mibovu haiwezi kurekebishwa?

Note: Nakubaliana na wanasema "akili" ndiyo msingi wa Kila kitu.
Kwa Tanzania Mzee Ruksa akaanza kuibomia misingi mibovu,mkapa akaendelea kuisambaratisha, Kikwete akaanza kuijenga upya, Magufuli akajitahidi kuirudisha baadhi ya misingi mibovu ya Nyerere na kuibomia misingi mizuri iliyosnza kujengwa na Kikwete, Mwenyezi Mungu akamstopisha.

Kwabuwezo wa Mwenyezi Mungu katuwekea Mama Samia kurekebisha palipoanza kubomolewa na bwana yule na kuendeleza kuijenga misingi thabiti iiyoanza kujengwa na Kikwete.

Heko mama Samia.
 
Naungana na wewe

Nyerere ndo aliipoteza nchi

Akiweka katiba inayomlinda yeye na chama chake

Hakuwekeza katika tafiti kuhusu ukuaji wa nchi miaka 50 ijayo.

Hakuwekeza katika elimu bora na miundombinu bora

Matatizo yote ya Tanzania yameanza baada ya Yeye kuwa Rais
Nakataa!

Je, Kenya kuna Nyerere
Congo je
Uganda
Zimbabwe?

Wanachi ndio tatizo! Hatuna akili.
 
Viongozi huwekwa na watu na watu wenyewe ndio sisi so why tusiwabadilishe?
Utawabadilisha vipi wakati wananchi wenyewe waliostahili kuwabadilisha viongozi, hawajitambui na wala hawajui wanatakiwa kuwa na viongozi wa namna gani?

Wananchi wanaosubiria teuzi bila ya kujali anateuliwa na nani, anaenda kufanya nini, au wale wanaosubiria rushwa za wakati wa uchaguzi ili wapate t-shirt au kiongozi wa CCM anayesubiria rushwa toka kwa wagombea ili apate pesa ya kununulia bati za kuezekea kibanda chake, huyo unategemea atakuwa na wazo lolote la kubadilisha viongozi ili kuwapata viongozi wazuri zaidi? Huyu kwake, kiongozi mzuri zaidi ni yule anayempa hongo kubwa zaidi.
 
Msilinganishe mataifa ya Ulaya na Nchi za Africa...

Mataifa ya Ulaya yapo miaka 1000 kabla ya nchi yoyote ya Africa kuanza kuwa nchi, Denmark ndio nchi ambayo bendera yake haijabadilika zaidi ya miaka 500
Nikisema hoja yako ya kipuuzi, unaweza kusema nimekuonea, labda niseme kuwa huelewi chochote.

Ebu nipime uelewa wako kidogo:

Singapore, Malaysia, Thailand, hizi nchi zina umri gani? Unajua kuwa haya mataifa yote tulikuwa kwenye kiwango sawa cha umaskini 1961? Imekuwaje leo UNDP wanasema pale walipofikia Malaysia, wakabakia hapo hapo, wasuendelee zaidi, sisi kwa speed tunayoenda nayo itatuchukua miaka 250?

Vipi kuhusu mataifa kama Misri na India, yameendelea sana kwa sababu nibya zamani sana?

Fuatilia, kuna scientific study kubwa ilikwishafanyika ili kujua kwa nini baadhi ya mataifa ni maskini sana na mengine ni matajiri sana.
 
Back
Top Bottom