Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Kama sikosei finland bado inaongoza KWA kuwa na watu wenye furaha..africa ni stress tupu hata uwe kiongozi.
 
Duh 🙄 !!
 
Hapo sasa !!
 
Umejiuliza kwanini na we na ukoo wako wote mpaka leo ni maskini na mafukara? Si mna rasilimali ya ardhi nyie? Jiulize kwanza wewe.
 
Ubarikiwe sana. Ni kweli utupu. Muafirka sio mtu heri ya katuni kuliko mtu mweusi
we ni wapumbavu kuliko hata nyani wa porini. sijawahi ona mtu anajitukana na kujidharau mwenyewe, hiki kizazi cha sasa ndiyo sifuri kabisa. Hivi wazee wetu km baba wa Taifa angekuwa na akili za kipumbavu km hizo zenu nchi hii ingepata hata uhuru? Baba wa Taifa alisimamia utu wa mtu mweusi na kusema binadamu wote ni sawa na wazungu wakamheshimu sana. sasa mapoyoyo km nyie mtaisaidia nini nchi hii km mnajitukana wenyewe? Hovyo kabisa nyie.
 
punguza makelele yanaumiza masikio
 
Umejiuliza kwanini na we na ukoo wako wote mpaka leo ni maskini na mafukara? Si mna rasilimali ya ardhi nyie? Jiulize kwanza wewe.
Hizo ndio fikra za Ubinafsi tunazozizungumzia humu ! Mtu akishakwapua aanze kuwatambia wengine !! Halafu anajiona mjanja !!

Watu wa namna hiyo hawazifikirii Nchi zao kabisa ! Na ndio tofauti kati yetu na hao wazungu !!
 
Umemaliza kila kitu, nidhamu yao ya matumizi ipo juu sn Waziri wa Denmark anatumia public transport huku WEO anataka afuatwe na V8 kila siku, tuna viongozi wabovu na wezi wakubwa
Umenikumbusha kitu! Wakati nikiwa mwanafunzi wa Primary, jirani yetu mwajiriwa wa Tanroad, ilikuwa ni kawaida watoto wake kupelekwa shule kwa gari la Serikali, na kurudishwa Jioni. Huyo hakuwa mkubwa saana, lakini hata watoto wake walikuwa wakihidumiwa na gari la Serikali, vipi kwa wale vigogo hasaa?
 
Kama sikosei finland bado inaongoza KWA kuwa na watu wenye furaha..africa ni stress tupu hata uwe kiongozi.
Nayo pia ni kanchi kadoogo, inaingia Tanzania zaidi ya mara mbili, na kana population ya watu milioni tano tu, lakini inaipa Tanzania misaada.

Ila Wazungu nao!!! Kama vile hawawaamini watu weusi.

Mwaka 2009, niliingia ibadani kwenye Kanisa moja mkoani Kilimanjaro. Mchungaji wa hilo Kanisa alikuwa amerejea kutoka Finland alikoenda kuomba msaada. Katika taarifa aliyoitoa Kanisani ya safari yake, alisema Wafinish wamekubali kuufadhili mradi husika ila hawatatuma pesa, watakuja kuusimamia wenyewe. Walikuwa na mashaka kuwa kama wangewapatia pesa taslimu, huenda zingetumika isivyostahiki.

Yaani hawawaamini hata Wachungajui?
 
Hizo ndio fikra za Ubinafsi tunazozizungumzia humu ! Mtu akishakwapua aanze kuwatambia wengine !! Halafu anajiona mjanja !!

Watu wa namna hiyo hawazifikirii Nchi zao kabisa ! Na ndio tofauti kati yetu na hao wazungu !!
Kama isingelikuwa ninawheshimu Watanzania wenzangu, ningethubutu kusema Watanzania ni "wezi" ila kwa sababu nawaheshimu, nimejizuia kusema.

Tulipokuwa Sekondari, tulikuwa tukiulizana kazi tunazozitarajia kufanya baada ya kuhitimu Vyuo, ungesikia TRA, POLISI, n.k.
Kwa nini huko? Mwingine atakuambia, kwa mfano, ukiwa Trafiki, hata kama hakuna unga ndani, unaweza kuagiza maji yainjjikwe jikoni kwa sababu una uhakika ukishafika barabarani lazima utarudi na unga.

TRA ndiyo usiseme kabisaa. Mtu anayefanya kazi huko asipoonekana akiinuka kiuchumi kwa Kasi, huitwa mjinga.

Yaani asiyeiba ni mjinga????
 
Wachungaji pia ni watu. Hata wewe ukikaa na mchungaji, jua kuwa uko na mchungaji lakini pia ni mtu. Zipimeni Kila roho sio ziaminini Kila roho.
 
Tena ni mjinga wa kutolewa mfano kabisa !!
 
Duh !
 
Mwalimu alikuwa na msimamo huo kwa vitendo sio kwa Maneno ya mdomoni !! Ndio maana Mwalimu hawezi kusahaulika vizazi na vizazi vitakavyokuja !! Mwalimu aliyaishi yale aliyokuwa akiyasema. !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…