Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Ukiwaweka hawa viongozi wa Tanzania Denmark au Korea na Viongozi wa Korea / Denmark kila kitu kitakuwa vice versa.

Uzuri wa wananchi wa nchi hizo hawatachukua muda mrefu viongozi wabovu wataondolewa madarakani na kuishia jela.

Kwa wenzetu kuna uwajibikaji, seriousness, wako serious na maisha.
Umemaliza kila kitu, nidhamu yao ya matumizi ipo juu sn Waziri wa Denmark anatumia public transport huku WEO anataka afuatwe na V8 kila siku, tuna viongozi wabovu na wezi wakubwa
 
Siyo Denmark pekee. Vinchi vyote vidogo huko Ulaya, na baadhi huko Asia, ukilinganisha na Tanzania ni aibu tupu:

Denmark
Norway
Finland
Sweden
Singapore
Switzerland

Utajiri mkubwa hapa Ulimwenguni ni akili, wala siyo idadi kubwa ya fisi na pundamilia, siyo dhahabu na gas, ardhi nzuri ya kilimo, maziwa, bahari au hali nzuri ya hewa.

Hata upewe vyote, ukinyimwa akili, vyote vinakuwa havina maana. Lakini ukibahatika ukapata akili,ni mwanzo wa mafanikio yote. Kwanza utajua ni nini kilicho muhimu, utakuwa na mifumo mizuri ya kuvuna rasilimali, utakuwa na tekinolojia, utakuwa na mifumo mizuri ya utawala, na mifumo mizuri ya kusimamia uchumi kwa ujumla.

Sisi tuna vitu vingi, lakini asilimia kubwa sana ya watu wetu wamenyimwa akili, utashi na maarifa. Ndiyo maana wachache wenye akili, maarifa na utashi, ama wanakuwa frustrated na kukata tamaa au kuishia kwenda kufanya kazi mataifa ya nje kwa sababu nchini mwao ni giza nene.
Sahihi kabisa tena sn
 
Hizo ni fikra tu. Hatuna uhakika kama mambo yatabakia vile vile au yatabadilika, kwa sababu hatujawahi kubadili uongozi na mifumo yake hata mara moja. Ila tu tumejazwa na imani kuwa hali itakuwa vile vile.
Point hapo ni kwamba kwa kuwa bado hatujabadili kisawasawa hatuwezi kuwa na uhalali wa kusema wote ni wale wale tu !!
 
Denmark inatarajia kuufunga ubalozi wake nchini Tanzania ifikapo 2024. Ni kati ya nchi ambazo zimekuwa zikiipa Tanzania misaada, tokea ikiitwa Tanganyika hadi sasa ikiwa inajulikana kwa jina adhimu, Tanzania.

Lakini Denmark ni nchi ya namna gani?

Ukifanya ulinganisho, Tanzania imeizidi kwa mambo mengi isipokuwa ujinga na umaskini. Ina rasilimali nyingi sana kuizidi, na hata idadi ya watu tumeipita mbali sana.

Denmark, ni kanchi kadoogo, kenye ukubwa wa kilomita za mraba 42,920 lakini inaizidi kiuchumi Tanzania, nchi Kuubwa kieneo, yenye kilomita za mraba 945,087.

Denmark, ni kanchi kadoogo kenye watu milioni tano lakini inaipa misaada nchi kuubwa, Tanzania, yenye watu milioni sitini na moja.

Ni nini siri ya kanchi kadogo kuizidi nchi kubwa kama Tanzania? Imekuwa ikiisadia Tanzania tokea 1963, enzi hizo ikiitwa Tanganyika, lakini hakuna taarifa ya Tanzania ambayo ni nchi kubwa kuisaidia Denmark kanchi kadogo.

Imewezekanaje kwao lakini kwetu ikashindikana?

Mwingine anaweza kusema ni kwa sababu ya ukoloni, lakini hilo halina mashiko. Hata Korea Kusini ilishawahi kuwa koloni la Japan, lakini kwa sasa wanatukimbiza kiuchumi.

Ni nini walichogundua hao watu weupe ambao weusi wa Tanganyika na Zanzibar hawajagundua?

Angalia, hata eneo la Korea Kusini ni dogo sana ukililinganisha na ukubwa wa Tanzania. Ina kilomita za mraba 100,210 na watu milioni hamsini na moja.

Inawezekanaje kanchi kadoogo, Denmark, kuipa misaada nchi kuubwa, Tanzania?
Kilo moja ya dhahabu na kilo mia za ugoro kipi kina thamani kubwa?
 
Inaweza kulisha Africa nzima
Hako kanchi kadoogo, ambao unaweza kuingia mkoa wa Tabora mara mbili kanaweza kufanya jambo kubwa kiasi hicho?

Tabora ina kilomita za mraba 76,151, lakini sina uhakika kama imejitosheleza kwa chakula, sembuse kuilisha Tanzania.

Na Denmark ina kilomita za mraba 42,943, lakini mambo yake si ya kitoto.

Ama kweli, ukubwa wa pua si wingi wa kamasi.
 
Hako kanchi kadoogo, ambao unaweza kuingia mkoa wa Tabora mara mbili kanaweza kufanya jambo kubwa kiasi hicho?

Tabora ina kilomita za mraba 76,151, lakini sina uhakika kama imejitosheleza kwa chakula, sembuse kuilisha Tanzania.

Na Denmark ina kilomita za mraba 42,943, lakini mambo yake si ya kitoto.

Ama kweli, ukubwa wa pua si wingi wa kamasi.
Kosa mali lakini usikose akili, viongozi aina ya Makamba, Bashe, Ummy, Masauni, Mbarawa, Mwigulu, Nape sijui Aweso ndiyo utegemee watupeleke kwenye matokeo chanya? lazima tuamke
 
Kilo moja ya dhahabu na kilo mia za ugoro kipi kina thamani kubwa?
Sijui mkuu, lakini nakuahidi, ukikubali kuniachia hiyo kilo Moja ya dhahabu halafu wewe ubaki na kilo mia za ugoro, nikitoka tu kuiuza dhahabu, nakupa Asante ya IST mpyaa, zero kilometre.
 
Umemaliza kila kitu, nidhamu yao ya matumizi ipo juu sn Waziri wa Denmark anatumia public transport huku WEO anataka afuatwe na V8 kila siku, tuna viongozi wabovu na wezi wakubwa
Mkuu, waheshimu viongozi. Unataka viongozi wa nchi kuubwa, kama Tanganyika wawaige Mawaziri wa nchi ndoogo, Denmark, watumie usafiri wa umma?

Denmark ni kanchi kadoogo sana, hawana uwezo wa kuwanunulia viongozi wao mav8, ila wanaweza kutupa misaada

Tanzania ni nchi kuubwa, hivyo ni halali kila kiongozi kutumia V8.
 
Ni jambo linaloniuma sana mkuu.
Mungu katuweka kwenye bara zuri lenye kila aina ya utajiri ila akatunyima akili na maarifa ya kuufaidi huo utajiri.

Mim nataman wakoloni wangeendelea kuwepo.
Heee!
 
Singapore ni mdogo wetu🤣.
Ana miaka 58 toka apate uhuru wake ila unamuonaje?
Sisi hata tupewe miaka 1000 kwa akili zetu tutakua hivi hivi
Singapore!!! Mhhh! Singapore!

Unaonaje, ukiondoa nafasi ya Rais pekee, tukilikodi baraza la Mawaziri alau kwa kipindi cha miaka mitano tu?
 
Mkuu, waheshimu viongozi. Unataka viongozi wa nchi kuubwa, kama Tanganyika wawaige Mawaziri wa nchi ndoogo, Denmark, watumie usafiri wa umma?

Denmark ni kanchi kadoogo sana, hawana uwezo wa kuwanunulia viongozi wao mav8, ila wanaweza kutupa misaada

Tanzania ni nchi kuubwa, hivyo ni halali kila kiongozi kutumia V8.
Kwa ujinga huu tuache kulalamika sasa acha wafanye matanuzi
 
Kwa Tanzania Mzee Ruksa akaanza kuibomia misingi mibovu,mkapa akaendelea kuisambaratisha, Kikwete akaanza kuijenga upya, Magufuli akajitahidi kuirudisha baadhi ya misingi mibovu ya Nyerere na kuibomia misingi mizuri iliyosnza kujengwa na Kikwete, Mwenyezi Mungu akamstopisha.

Kwabuwezo wa Mwenyezi Mungu katuwekea Mama Samia kurekebisha palipoanza kubomolewa na bwana yule na kuendeleza kuijenga misingi thabiti iiyoanza kujengwa na Kikwete.

Heko mama Samia.
Nilitegemea jibu kama Hilo Kutoka kwako (lawama Kwa Nyerere).

Tambua: Uimara wa nchi unategemea sana uimara wa wananchi, hapo nazungumzia uimara wa akili.
Kama taifa linakuwa na wananchi wasiojielewa/Vilaza, pia taifa Hilo litazalisha viongozi wasiojielewa/Vilaza, na kinyume chake ni sahihi. Wananchi ndiyo msingi wa Kila kitu.
Nachoona kwako ni wewe kuwa obsessed na personality ya kiongozi mkubwa wa kitaifa kama ndiyo Chachu pekee ya maendeleo Kwa taifa, na ndiyo mtazamo wako ambao agharabu umejikita zaidi kidini. Kwamba kiongozi flani akiwa wa mlengo flani wa kidini huyo ndiye anayefaa, na pia akiwa wa mlengo flani wa kidini huyo hafai, nakataa asilani.
Wananchi ndiyo wazalishaji wa Kila kitu katika nchi, ikiwemo pia na viongozi hodari wanaokuwa na tija Kwa nchi.
 
Ilikuaje wakawa developed na sisi undeveloped?
Sasa apo kuna mabo mengi sana ambayo yametutofautisha mpaka wao wameweza kuwa developed country, hizi zote zinaweza kuwa na sababu nyingi kama internal forec and external force yaan factors ambazo zimechangia
 
Back
Top Bottom