Injili: Nyimbo za Papii Clever, Dorcas pamoja na Merci Pianist zinanibariki sana

Injili: Nyimbo za Papii Clever, Dorcas pamoja na Merci Pianist zinanibariki sana

Dr Restart

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
4,949
Reaction score
24,046
Amani iwe juu yenu wana wa Mungu.

Nina miezi kama mitatu sasa, nyimbo za wahusika zimekuwa zikijirudia katika orodha ya nyimbo ninazosikiliza mara nyingi.

Papi Clever na Dorcas ni wanandoa, Merci Pianist ni mtaalam wa kupiga kinanda kwa kiwango kikubwa sana.

Mimi ni muumini wa nyimbo za taratibu kidogo na zenye mapigo ya vinanda vya kufurahisha. Napenda mno upigaji wa guitar na piano inavyochanganya, aaagh sijajaliwa tu uwezo wa kuipiga. Ninaomba Mungu nistaatu mapema, nikajifunze kuipiga na kumuimbia Mungu. Zinanipeleka mawinguni na kuhisi nipo juu, nikiimba na kusifu pamoja na Makerubi.

Hawa waimbaji kutoka Rwanda wana nyimbo nyingi sana. Mwaka huu 2023, walidondosha Collection ya nyimbo za Wokovu yenye jumla ya nyimbo 16 za Kiswahili.

1. Mwokozi Wetu
2. Roho Yangu
3. Yesu ni Furaha Yangu
4. Fanyia Mungu kazi
5. Ee Mungu mwenye kweli
6. Ee Mungu mwenye haki
7. Msifuni msifuni
8. Nilikwenda mbali sana
9. Pendo la Mungu
10. Yesu Ovukiy'i Bethlehemu
11. Uzima ninao
12. Matendo ya Mungu
13.We Mutima urira
14. Yanyonjiyemo
15. Kisima cha Lehi
16. Siku moja ya mavuno..

Nyimbo zote ni nzuri mno. Ila mimi iliyonibamba zaidi ni Mwokozi wetu

Nyimbo zao nyingine ninazozipenda ni Tu Watu huru
Nyingine inayonibamba na kunivuta katika Wokovu ni ameniweka huru kweli

Hakika ninavutiwa sana na nyimbo zao. Sichoki kuzisikiliza, wala haziumizi masikio. Ile midundo na mapigo ya vifaa ndo vinaniacha katika uwepo mkubwa sana.

Je, wewe unawafahamu? Ingia YouTube, watafute kwa jina lao. Papi Clever & Dorcas.

Karibu utuambie, ni wimbo upi umekubamba?
 
Zipo katika kitabu kinaitwa Nyimbo za Wokovu, kinachochapwa na kanisa la Pentecoste, ni kama ilivyo tenzi za Rohoni,kinaizwa elfu 10, kina nyimbo nyingi kuliko tenzi
 
Zipo katika kitabu kinaitwa Nyimbo za Wokovu, kinachochapwa na kanisa la Pentecoste, ni kama ilivyo tenzi za Rohoni,kinaizwa elfu 10, kina nyimbo nyingi kuliko tenzi
Bahati mbaya sana sijawahi kuiona.

Nitajipatia nakala yangu. Ni maduka gani yanauza kwa Arusha ama Dar? Ubarikiwe sana.

Lakini bado hawa nitaendelea kuwasikiliza. Kwa sababu ya namna upigaji maridadi wa vyombo unavyoenda.

Mimi nilidhani ni album yao.
 
Bahati mbaya sana sijawahi kuiona.

Nitajipatia nakala yangu. Ni maduka gani yanauza kwa Arusha ama Dar? Ubarikiwe sana.

Lakini bado hawa nitaendelea kuwasikiliza. Kwa sababu ya namna upigaji maridadi wa vyombo unavyoenda.

Mimi nilidhani ni album yao.
 

Attachments

  • IMG_20230625_111425.jpg
    IMG_20230625_111425.jpg
    439.6 KB · Views: 16
  • IMG_20230625_111529.jpg
    IMG_20230625_111529.jpg
    789.2 KB · Views: 14
Bahati mbaya sana sijawahi kuiona.

Nitajipatia nakala yangu. Ni maduka gani yanauza kwa Arusha ama Dar? Ubarikiwe sana.

Lakini bado hawa nitaendelea kuwasikiliza. Kwa sababu ya namna upigaji maridadi wa vyombo unavyoenda.

Mimi nilidhani ni album yao.
Wameimba vizuri sana,tatizo lipo kwenye beats za nyimbo zote zinafafa(sampling)
 
Wameimba vizuri sana,tatizo lipo kwenye beats za nyimbo zote zinafafa(sampling)
Bahati mbaya mimi si Mtaalam wa muziki. Hivyo wala sijanotice ufanano huo.

Mimi wananibariki mno.
 
Back
Top Bottom