STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL:
thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 40
SONGA NAYO............
Vyombo vya habari vilikuwa viko busy sana kuongelea jambo moja hata mtaani watu walikuwa wamejazana kila sehemu wakiwa wanaongelea jambo moja ambalo liliishtua nchi majira hayo ya asubuhi, kilichokuwa kimeleta taharuki yote hiyo ni makaratasi ambayo yalikuwa yamesambazwa na kubandikwa kila sehemu ndani ya jiji la Dar ndicho kitu ambacho kilizua hiyo taharuki kubwa sana ndani ya hili jiji, yalibandikwa kuanzia kwenye nguzo za umeme, maofisi mbali mbali, kwenye mabango ya barabarani, kwenye vituo vya mabasi, treni, airport, viwandani, mpaka kwenye sehemu za biashara na masokoni. Maofisa wa polisi walisambazwa kila sehemu ili kuhakikisha karatasi hizo zinabanduliwa na kuondolewa kwa haraka sana lakini waliacha mara moja baada ya kupokea maagizo kutoka kwa IGP kwamba waache mara moja hicho walichokuwa wanakifanya kwa sababu walikuwa wanaelekea kulichafua jeshi la polisi.
“Mkuu hivi unahisi kuwazuia kuyatoa makaratasi hayo ni maamuzi sahihi sana” UTAPEWA alikuwa yupo karibu sana na IGP siku hiyo kwa sababu ndiye mtu ambaye aliwahi ofisini kwa bosi wake Kwenda kutoa hizo taarifa ambazo zilikuwa zinaonekana kuanza kuongelewa sana kila sehemu.
“Huo ndio uamuzi bora zaidi ambao utatuweka sisi kwenye mikono salama lasivyo tutajichafua sana na jeshi la polisi tutaonekana hatuna maana yoyote ile”
“Kivipi mkuu sijakuelewa”
“Angalia kilicho andikwa kwenye hayo makaratasi kisha pima hali ya wananchi kwenye vichwa vyao kwa sasa, kilicho andikwa ni kitu ambacho wao wanataka kifanyiwe kazi sasa ukianza kuyatoa utaamanisha nini? watajua kwamba huenda kuna mambo tunayaficha ndiyo maana hatutaki kuwaunga mkono watu ambao wamejitokeza kupambana na hiyo hali ambayo ilikuwa ianendelea kwenye nchi yetu. Ukiachana na hilo hizo habari zipo kila sehemu mpaka kwenye vyombo vikubwa vya habari kuanzia mtandaoni, kwenye runinga mpaka kwenye simu unahisi hapa ukizitoa utakuwa umefanya nini zaidi ya kupoteza muda” jibu la IGP lilimfanya kijana huyu ambaye siku ya kwanza wakiwa wameenda kuangalia sehemu ambayo jaji mkuu aliuawa walizinguana sana na ASP Bakari Zalimo ambaye alikuwa mkubwa wake kwa cheo naye ndiye alikuwa msaidizi wake lakini hawakuwa wakiiva sana kwa sababu Utapewa alikuwa anapenda sana kuchukulia mambo mazito kiwepesi mno.
“Nimekuelewa mkuu, kwahiyo kinatakiwa kifanyike nini?”
“Asp atakupa maelezo yote nini cha kufanya, yuko wapi kwanza?” alikunja sura baada ya mtu huyo kutajwa hapo
“Bado hajafika”
“Mpigie simu haraka sana mwambie namhitaji ofisini sasa hivi”
“Sawa mkuu” aliinyanyua simu yake wakati anataka kupiga Asp Bakari Zalimo alitokea kwenye hiyo sehemu na kutoa heshima kwa IGP hivyo hivyo Utapewa naye alitoa salamu kwa Asp ambaye hata hakuhangaika kumjibu chochote kile
“Nifuate ofisini”IGP alitamka akiwa anaanza kuondoka na Asp huyo alianza kumfuata, aligeuka kumwangalia Utapewa alikuwa anamwangalia jicho baya sana
“Ipo siku utaingia kwenye kumi na nane zangu tu” Utapewa alitamka mwenyewe kwa hasira sana akiwa anatoka hiyo sehemu na Kwenda kwenye ofisi yake kusubiri maagizo ambayo angekuja kupewa.
“Umeona kinacho endelea?”
“Mimi ndiye niliye ifanya hiyo kazi” maneno yake yalimfanya IGP ageuke na kumwangalia sana kijana wake huyo
“Ulikutana naye mara ya mwisho lini na wapi?
“Jana usiku, alinifuata Keko kwenye lile eneo langu”
“Ilikuaje?”
“Alikuja lile eneo nilishangaa sana imekuaje mpaka akajua nipo pale baadae akaja kunambia kwamba simu yangu ndiyo iliyo nifanya nijulikane, ila kilicho nishangaza anaonekana kwamba ananijua zaidi ya pale mpaka nilibaki namshangaa sana, nakumbuka kauli yake ya mwisho aliniambia kwamba nichapishe hizo karatasi kisha nitafute vijana wengi sana wazisambaze sehemu zote za jiji la Dar huku akiwa ameniachia milioni 50 za kitanzania kwa ajili ya kukamilisha kazi hiyo. Nilijiuliza sana huyu mtu ni nani mpaka ananiagiza mimi kazi hiyo ila sikutaka kumuuliza kwa sababu nilikuwa nina uhakika huenda ni wewe umemtuma kufuatia kauli ya mheshimiwa raisi ya mchana wa jana alivyosema kwamba atatoa majibu baada ya miezi sita hivyo bila shaka najua ni wewe ulimtuma ile kazi” Asp Bakari wasiwasi wake haukuwa mkubwa sana kwa sababu alihisi huenda mtu huyo ndiye ambaye alikuwa amemtuma Jason kumpa zile karatasi akabandike.
“Ulisoma kilicho andikwa ndani yake?”
“Hapana, maana nilinunua tu mavazi meusi na mask nikatafuta boda boda ambaye nimezunguka naye kutafuta vijana wenye njaa kali wapo wengi sana nikawa nawapa hiyo kazi na ujira wao nimeimaliza hiyo kazi saa kumi ya usiku nikaenda kulala hivyo sikupata hata nafasi ya kusoma kilicho andikwa nilipiga tu kopi nyingi sana”
“Kwanini hukusoma?”
“Nilijua ni kazi ya kipolisi hivyo sikuwa na shaka nayo” mzee huyo baada ya kuisikia hiyo kauli ya kijana wake, alichukua rimoti kwenye meza yake na kuwasha runinga kubwa ambayo ilikuwa mbele ya macho yao hapo ndipo Asp alijilaumu kuchukulia poa hilo jambo, kila chombo cha habari kilikuwa kinazungumzia kuhusu hiyo barua ikiwa imeambatanishwa pembeni na ilikuwa inasomeka hivi.
KUTOKA KWA RAIA MWEMA
“Kwenu watanzania wote, nawasalimieni kwa jina la nchi yangu pendwa ambayo kila mtu nina uhakika anaijua vizuri sana kwa sababu ni nchi ya kipekee sana ila kwenye hii nchi wametokea watu wachache sana ambao wameamua kujimilikisha hii nchi na kuigeuza kuwa ya kwao, wanafanya kila wanalo litaka wao na muda wanao uhitaji wao bila kujua kwamba hii nchi ina misingi yake na sheria zake”
“Kufuatia kilicho tokea mauaji ya mheshimiwa wangu raisi wa nchi ya Tanzania, mauaji ya kikatili ya jaji mkuu Markvelous Japhary na familia yake yote mkewe mjamzito na mwanae ambaye amemuacha mdogo wake akiwa mkiwa pamoja na tukio la kutekwa kwa mwanasheria ambaye ni kipenzi cha wengi Yasinta kobe basi NATANGAZA HADHARANI KWAMBA NATOA MUDA WA WAHUSIKA WA HILI JAMBO KUJITOKEZA HADHARANI, NAWAPA MIEZI SITA INAWATOSHA SANA INATAKIWA WAWE WAMEJITOKEZA MBELE YA VYOMBO VYA HABARI NA KUJA KUKIRI MAKOSA YAO PAMOJA NA KUOMBA MSAMAHA KWA JAMII NA WATANZANIA WOTE IKIWEMO FAMILIA AMBAZO WAMEZILETEA MATATIZO MAKUBWA YA KUWAONDOA NDUGU ZAO, kama watajitokeza na watanzania wakawasamehe kwa moyo wote basi nami nitawasamehe na wataadhibiwa kwa mujibu wa sheria ya nchi ya Tanzania ila kama wakikaidi badi siku ya kwanza baada ya miezi sita kupita kuanzia leo nitaanza kuwapa adhabu mimi mwenyewe mmoja mmoja kati ya hao watu na kwa huo muda sitakuwa na muwa mwingine tena wa nyongeza kuwasamehe”.
“MWANASHERIA Yasinta Kobe NITAMRUDISHA KWAKE SIKU YA JUMATANO SAA SABA KAMILI MCHANA IKIWA NI SIKU MBILI TU KUANZIA HII LEO”.
“Ahsante naipenda sana nchi yangu Tanzania”.
Huo ndio ujumbe ambao ulikuwa umeandikwa kwenye hizo karatasi Asp alijiona yeye ni moja ya watu wazembe sana kuwahi kutokea yaani alikuwa anasambaza yeye mwenyewe na bado hakujua kitu kilichokuwa kimeandikwa humo ndani
“Mimi sina mamlaka ya kumtuma huyo mtu eneo lolote lile wala sina hiyo nguvu ya kumpangia cha kufanya, anafanya anacho jisikia yeye mwenyewe labda raisi pekee ndiye mtu ambaye anaweza akaongea naye vizuri ila sisi wengine anaongea na sisi kikawaida sana na tunaweza kumshauri tu na sio kuanza kumpa amri” hayo maneno yalimshtua Asp kutoka kwenye mwazo mazito ambayo yalikuwa kwenye kichwa chake.
“Mkuu unajua bado sikuelewi unacho kisema hapa naona kama utakuwa umechanganyikiwa sio bure, kumbuka siku ile kule Mbagala ulinipa kazi ya kusafisha ile miili kwa kusema kwamba huyo ndiye aliyekuwa ameua na hakuna sheria yoyote ambayo ilitumika kumkamata wala kuuweka wazi huo ujinga aliokuwa ameufanya, leo tena mimi nimefanya kazi nikijua ni amri yako wewe kumbe ni yule kijana kwa akili zake ndiye aliyekuja kwangu na kunituma kama mtoto wake nitamtafuta na nitamfanya kitu kibaya sana” maneno yake yalimfanya IGP amimine maji kwenye kikombe na kumpatia ili apunguze presha kwanza maana aliona kijana huyo anaropoka vitu ambavyo hata havijui.
“Alivyokuja kwako jana hakuna kauli yoyote yenye utata ambayo alikuachia” Asp aliacha kunywa hayo maji baada ya kuona mkubwa wake amekuwa siriasi sana, alijaribu kukumbuka kwa umakini sana
“Yes,aliniambia kama nikibandika hizi karatasi tutakutana baada ya miezi sita lakini kama nisipo bandika basi leo tungekutana kwangu” alijibu akiwa ana uhakika kwamba kumbukumbu zake hazikumdanganya kabisa.
“Sasa kwanini hayo maswali hukumuuliza yeye unaanza kulalamika hapa?”
“Kwa sababu nilijua huenda ni amri yako wewe”
“Ulishindwa kunipigia simu ili kupata uhakika kama ni mimi? Kwahiyo akija mtu hapo akakwambia fanya mauaji bosi wako kanituma utafanya na baadae uanze kunilaumu mimi? Hivyo ndivyo nilivyo kufundisha kufanya kazi?” maneno hayo yalimgusa ni kweli alifanya uzembe mkubwa sana kuruhusu hicho kitu kitokee, alikaa kimya kwa sababu aliambiwa ukweli
“Unataka kumjua yule ni nani?” IGP aliongea kwa sauti nzito ambayo ilianza kumtisha hata Asp Bakari Zalimo
“Yule ni mkurugenzi wa usalama wa taifa?”
“Whaaaaaaat?”
“Huyo ndiye anaye hakikisha usalama wa hili taifa” Asp alikaa chini yaani kiufupi alichoka sana, yule alikuwa ni kama kijana mwenzake, mara ya kwanza alihisi IGP anampendelea kwa sababu alikuwa ni mdogo wa jaji mkuu lakini haikuwa kweli kilichokuwa kinafanya mpaka wamheshimu sana kilikuwa ni cheo chake kikubwa sana ambacho kilikuwa kwenye vifua vya watu wachache sana
“Mkuu yule bwana mdogo ndiye mkurugenzi wa usalama wa taifa hili?”
“Ndiye huyo huyo, mpaka akaja kwako na kukupa kazi jua ameamua kukuamini sana tena sana kwa sababu huwa hajitokezi kirahisi sana namna hiyo kwa mtu yeyote yule na kama siku ukitokea ukauvunja huo uaminifu wako kwake basi ndiyo itakuwa habari yako ya mwisho kuendelea kuwa hai kwenye uso wa hii dunia” Asp alinyanyuka kwa kujilazimisha na Kwenda kukaa kwenye kiti, alikuwa na maswali mengi sana mpaka alihisi kama kichwa chake kinamuuma sana, bosi wake alilijua hilo IGP alisogea mpaka kwenye kabati akatoa vidonge na maji na kumpatia kijana wake huyo ili atulize kichwa chake maana alikuwa anaambiwa mambo ya kikubwa mno.
“Kwanini umeniweka wazi jambo ambalo linaonekana kuwa la hatari na siri kubwa snaa namna hii?”
“Yeye ndiye aliyetaka mimi nikwambie wewe ukweli”
“Alitakaje kuniambia ukweli na vipi kama nitatoboa siri hii kwa watu?”
“Utakuwa umejifupishia maisha yako wewe mwenywe, nimekupa hizi taarifa kwa sababu wewe ni kijana wangu ambaye nakujua na nakuamini sana, kuna mambo mengi sana ambayo yanaendelea kwenye nchi hii lakini wewe hapo hauwezi kuyaelewa mpaka siku ambayo baadhi ya watu wataamua kuyaweka hadharani. Yule ni mwanadamu kama wewe kimwonekano tu ila kuna muda hata mimi huwa namuogopa sana japo mimi ndiye pekee mtu ambaye anamsikiliza sana ukimtoa raisi ila havumiliki ipo siku utamuona kwenye macho yako ndipo utakuja kunielewa kwamba yule ni nani”
“Nahisi kama nimechanganyikiwa maana nilikuwa namchukulia poa sana yule, sikuwahi kufikiria kabisa kwamba anaweza kuwa mtu wa hatari kama unavyosema wewe, naweza kujua tafadhali hata historia ya maisha yake japo kwa ufupi na kwanini mtu huyo ni wa siri sana na anaishi nje ya nchi halafu muda huo huo ndiye mkurugenzi wa usalama wa taifa? Na ni kwanini hizi taarifa huwa zinafichwa sana namna hii?” Asp aliuliza swali ambalo lilimfanya IGP asikitike sana.
“Nenda kamwambie Utapewa kwamba aende mtaani akahakikishe usalama wa raia kwa sababu huo ujumbe unaweza ukafanya watu wakaanza kuandamana mitaani huko mwisho wa siku ikaanza kuleta taharuki kubwa ambayo inaweza kutufanya tukawa sehemu mbaya, hizo taarifa ambazo wewe unazihitaji hata mimi sizijui kama una shida ya kuzijua sana basi subiri akirudi huko aliko ukamuulize mwenyewe au kama akiwa na kazi nawewe basi atakutafuta yeye ila kama akirudi huko nchi itakuwa kwenye hali ya kutisha sana namjua vizuri yule kichaa, nakupa likizo ya wiki moja kapumzike na familia yako" Asp alishangazwa sana na maamuzi ya bosi wake hakumjibu swali lake na kingine alimpa likizo ya ghafla sana basi hakuwa na namna alitoka humo ndani kinyonge sana akiwa amejishika kiunoni haamini alichokuwa anaambiwa na kukishuhudia kwa macho yake.
Alitoka mpaka nje ambako alimpa msaidizi wake huyo majukumu yote na kumwambia alitakiwa kusimama kwenye nafasi yake kwani wiki nzima asingeweza kuonekana ndani ya hilo eneo, aliondoka na kupanda piki piki yake ambayo ndiyo alikuja nayo siku hiyo akiwa na mawazo mengi sana, hakuwa anauelewa ulimwengu vizuri alikuwa kila akipita njiani anawaangalia sana watu hakutaka kuendelea kuwaamini wanadamu tena kwenye maisha yake unaweza ukamuona mtu wa kawaida sana kwenye macho yako ila nyuma yake ana mambo mengi sana ya kutisha na huo ndio ulimwengu ambao alikuwa amefunguliwa kwenye macho yake.
Sehemu ya 40 inafika mwisho sina la ziada tena tukutane sehemu inayo fuata.
Wasalaam
Bux the storyteller.