Intelijensia ya simba imchunguze Henock Inonga

Huu ni upumbavu.
Unadhani Simba ndiyo timu ya kufungwa kila siku na kinye fc?
 
Mnavyo msema hiyo Inonga, utafikiri timu nzima ilikuwa na mchezaji mmoja tu!

Ila binafsi sishangai. Maana malalamiko ni jadi yenu. Hasa pale timu yenu inapofungwa. Baadhi yenu hamjawahi kuwa na uvumilivu kama mashabiki wa Yanga.
Mbona akicheza vizuri tunamsifia humu

Tukiona kasoro tutamsema pia humu humu

Sisi mashabiki hatuna platform nyingine ya kusifia ama kukosoa zaidi ya hapa mtandaoni
 
Itoshe kusema kuwa kwenye pesa hakuna ujamaa..licha ya mwamuzi elly sasii kuwa na mahaba na mnyama ila jana alichukua mpunga mrefu kuhakikisha kuwa maamuzi yake yanaelekea upande wa home shopping center. Soka letu linanuka milungula.
Sure
 
Haya mambo ya mpira wa kibongo huyajui

Ndio maana azam wanauita mpira wetu kivyetuvyetu
 
Ukisikia ramli chonganishi ndiyo hii sasa! Kunatafutwa kila aina ya visingizio ili kukamatana uchawi, na pia kuangushiana jumba bovu.

Timu imefungwa, Yanga amechukua Ngao kwa mara ya pili mfululizo! Watu wajipange kwa mechi zijazo.
Always kolo's uwa wanajiona wako mbele zaidi ya Yanga,sio kosa lao wameaminishwa hivyo wakati si kweli,waache waendelee kujiona hivyo ndio nzuri sana kwetu,hawa hawatakiwi kujua shida yao ipo wapi
 
Hii habari inanikumbusha fainali ya FA kule kigoma pale mukoko kaitafuta kadi nyekundu na akaipata kweli na kutolewa nje ya uwanja.kilichokuja kutokea ni kuichungulia Yanga ya Nabi kwenye instagram.
Haya mambo yapo hivyo mara zote mpira wetu hauchezwi uwanjani ule tunaoucheki ulishachezwa jana
 
Ata manura achunguzwe mechi za derby anajitia pancha ili asicheze,miswahili mijitu ya hovyo sana
 
Itoshe kusema kuwa kwenye pesa hakuna ujamaa..licha ya mwamuzi elly sasii kuwa na mahaba na mnyama ila jana alichukua mpunga mrefu kuhakikisha kuwa maamuzi yake yanaelekea upande wa home shopping center. Soka letu linanuka milungula.
Alichukua hela mpaka akamnyima Inonga redcard
 
Ulichowaza nani niliwaza hicho hicho,kuna dot dot ukiziunganisha ukweli unakuja.
 
labda kama kakugongea mkeo ila jana alizidiwa akili... Kwa uwezo gani ahongwe..?
 
Tanzania hakuna siri hata kidogo na ukibainika ktk uhuni huu uwezekano wa kuumia ni mkubwa mno.
 
Tatizo viongozi wabahili. Wanasajili cheap players. Pamoja na msiba wa ushambuliaji butu last season tumesajili striker gani tishio? Kila mtu ameonya Simba haina DM wa maana bado hatusajili!

Pale ondoa mzungu, Victor Ikpar na leta DM na mashambuliaji katili level za Manzoki au zaidi! Kama Phiri ameshindwa kuonesha kitu kwenye training piga chini hata kwa kuvunja mkataba tafuta mtu wa maana! Huu si muda wa majaribio.

Timu imevuna mikataba mizuri wasajili vizuri badala ya ubahili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…