International Schools zina nini cha zaidi?

International Schools zina nini cha zaidi?

Umeongea nini sasa shule za International huzitaki za kata pia huzitaki kwaiyo watoto wasisome
ANAANDIKA BICHWA KOMWE:-

Hizi shule zinazoitwa "international schools" zinafundisha nini cha ziada sana ambacho hakimo penginepo?

Ni kweli, shule zina mazingira mazuri na yanayofurahisha, lakini je, kile wanachofundishwa wale watoto kina hadhi gani ya kulipiwa mamilioni?

Hapa ieleweke vema kwamba siungi mkono mashule ya kata ambayo kimsingi ni mashule butu yasiyo na sifa wala vigezo vya kuwa shule. Mashule ya kata ni maeneo maalumu ambayo watoto wanaenda kujazwa ujinga na kupoteza wakati.

Hizi international schools pia ni kama mashule ya kata yaliyochangamka tu isipokuwa pale unaenda kununua KIINGEREZA kwa milioni hamsini kwa mwaka.

Zaidi sana mtoto atapewa midoli ya kuchezea na mabembea ya kuning'inia. Of course bila kusahau CHETI CHA KIINGEREZA.

Linapokuja swala la maarifa ni kitu kingine kabisa. Hawa watoto ni makanjanja tu kama watoto wengine wanaosoma kwenye mashule ya kata.

Mpaka sasa sijaona ni kwanini mtoto akanunue Kiingereza kwa shilingi milioni hamsini wakati mtu anaweza kujifunza Kiingereza hata chini ya mti na akabukua vema tu kama makanjanja wengine akina Dayamondi waliojifunza Vingereza magetoni.

Tukiwawezesha hawa walimu wetu uchwara wa shule za Kata wataweza kufundisha kizungu vizuri tu.

Tuanze kudahili walimu ambao wana ufaulu mkubwa badala ya kudahili vilaza wenye MADIVISHENI FOO ati ndio wakawe walimu!

Hili lizingatiwe sana.
 
Kudahili walimu wenye ufaulu wa juu sio tija kwasababu swala la kumfundisha mtu akakuelewa halihitaji ufaulu mzuri ila mbinu madhubuti, mfumo wa kama unaotumiwa na wanafunzi wa Masters na PHD kwa Tanzania ni mzuri ukitumiwa kuanzia kidato cha kwanza.
 
Tungekuwa na waalimu wa kufundisha kizungu for kama Kenya au Uganda, tusingeenda hizo, international, lugha ya kimombo ni Swahili ya dunia, kukijua ni muhimu Sana, Dunia ni, kama kijiji, wanaotoa ajira nzuri, ni Hao wanaoongea kizungu vzr!

Al Jazeera yote hqkuna mtangszaji mbongo! CNN yote hakuna mbongo, ukitaka kujua, umuhimu wa, kizungu muulize, Prof Tibaijuka, Dr Steregomena Tax, Dr Asha migiro, au, Muulize Dr Talimba, na Aden rage kwanini watoto wao waliwapereka Vyuo vya Melbourne austaria,au muulize yule kijana Benjamin Fernandes boss wa, NARA, acha kuuliza watu vilaza ambao umwamba wao, unaishia kupiga picha na hauvuki mipaka, Maulid kitenge, Gerald hando, chombo gani kingine ndani, ya Afrika kinaweza kumpa ajira!
bado mnachanganya kati ya English Medium Schools na Internationa schools. hata huko Uganda na Kenya kuna International schools ila hakuna English Medium Schools maana huko lugha ya kufundishia ni English.
 
Hujanielewa public speaking ni suala la kisaikolojia,tafuta six fears that face human beings. Na ilo la kuongea limo nadhani ni namba mbili Kama sio tatu.
Kujua na kutenda vitu viwili tofauti uelewe
kama ni swala la kisaikolojia huko IS wanafunzwa ndio maana watoto wa IS wanauwezo mkubwa wa kujieleza kwakua wameshajengwa kisaikolojia kwahyo hayo maswala ya sikisi fears tupa kule
 
I really trust desire of someone to reach the highest of his performance at his personal journey.
kama ni swala la kisaikolojia huko IS wanafunzwa ndio maana watoto wa IS wanauwezo mkubwa wa kujieleza kwakua wameshajengwa kisaikolojia kwahyo hayo maswala ya sikisi fears tupa kule
Hebu tuangalie big innovators na suala la shule walizosomea.
Am sure that going outside and buying expensive cigarettes won't make you rich.
Siamini kuwa kuwa shuleni Fulani inampatia mtu akili. Kila mtu ana uwezo wake na ishu kubwa ni desire ya mtu binafsi ku achieve maximum
 
Binafsi naheshimu sana kitu maarifa maana katika dunia ya sasa kinachotafutwa ni wewe una nini cha kutoa utatuzi wa changamoto zinazoikabili dunia.

Katika elimu yetu hii ya kidumu na mfagio inayomkaririsha mtoto majibu ya maswali ya mtihani badala ya kumfundisha kuwa na fikira tunduizi(critical thinking) na mdadisi huwezi kulinganisha na wenzetu wa mitaala ya kimataifa au hata baadhi ya English Medium kuanzia mazingira ya kujifunzia, nyenzo/vifaa hadi mfumo wa ufundishaji.

Tukubali tu kuwa ni umasikini ndio kikwazo lakini hakuna urithi bora kama elimu bora kwa mwanao.
 
Zama zimebadirika sana....
Sasa hivi baba, mama wote watafutaji. Na malezi ya watoto yameachwa kwa mtu wa tatu, msichana wa kazi, ndugu wa karibu, wa mbali jirani nk nk.
Yale masaa nane mtoto anayotumia akiwa shule, ni vyema mazingira ya shule yakawa salama kwao kiafya, kiakili, kimwili na imani pia.

Hapa ndipo umuhimu wa hizi shule unapo kuja, zina viwango vya kimataifa:
Yale matoto yenu yanayoshinda kwenye vibanda umiza kuangali video, chafu.
Yale matoto yenye kushinda kwenye ngoma na mikesha ya singeli,
Yale yale matoto yenye kushinda kwenye ku-bett,
yenye kujifunza misamiati na matusi mapya kila leo.

vyema yakasomea huukoo KATA

HATUTAKI HIYO MITOTO IJE IHARIBU WATOTO WETU!
ACHA WAO WASOME HUKO HUKO KATA, KWENYE SHULE ZA HADHI YAO.
 
Zama zimebadirika sana....
Sasa hivi baba, mama wote watafutaji. Na malezi ya watoto yameachwa kwa mtu wa tatu, msichana wa kazi, ndugu wa karibu, wa mbali jirani nk nk.
Yale masaa nane mtoto anayotumia akiwa shule, ni vyema mazingira ya shule yakawa salama kwao kiafya, kiakili, kimwili na imani pia.

Hapa ndipo umuhimu wa hizi shule unapo kuja, zina viwango vya kimataifa:
Yale matoto yenu yanayoshinda kwenye vibanda umiza kuangali video, chafu.
Yale matoto yenye kushinda kwenye ngoma na mikesha ya singeli,
Yale yale matoto yenye kushinda kwenye ku-bett,
yenye kujifunza misamiati na matusi mapya kila leo.

vyema yakasomea huukoo KATA

HATUTAKI HIYO MITOTO IJE IHARIBU WATOTO WETU!
ACHA WAO WASOME HUKO HUKO KATA, KWENYE SHULE ZA HADHI YAO.
Tuliosoma shule za kata ndio leo tunafanya mambo makubwa kwenye nchi
 
Hivi unazijua international schools kweli.Unaongelea English medium schools.International schools zinafundisha watoto toka mataifa mbalimbali na hutumia mitaala ya kimataifa kama Cambridge.Hizo shule wanazimudu watanzania wachache.Kwa Dar kuna IST iko Upanga,Heaven of peace iko Mbuyuni Salasala,kuna Aghakan nk.hizi za st Marys,Anne Marie ,Tusiime ni local tu ila hutumia kiingereza kuanzia chekechea.
Watu wamekariri kwamba shule zote za magari ya njano ni international jambo ambao si kweli international school means mtaala wa elimu ni wa first nje hata baadhi ya waalimu ni wa nchi za nje ,let's say UK ,USA, na wana exposure na mambo mbalimbali unakuta eti mwalimu anajiita mwalimu wa international kisha tu sababu anafundisha watoto wa magari ya njano , huyo huyo mwalimu akiwa anatazama CNN news anatoka kapa hajui nini kinazungumzwa. International means international that's is not child play ,that's where children are taught how to interact with the world.
 
St.Jude hiyo,bonge la shule kuzidi hata baadhi ya vyuo vikukuu hapa Bongoland.
Kumbe wewe ni wa "kule"😀


Nilikwepa kuitaja jina lakini kumbe umeshainyaka.

Nilikuwepo siku mkurugenzi wa hiyo shule alipotangaza kusitihwa kwa mchakato wa St. Jude kutumia mitaala ya Cambridge kwa sababu walimu wake hawajui Kizungu cha Kimataifa😢😢😢
 
Back
Top Bottom