Ipi ni historia ya kweli kuhusu Israel na wayahudi wa leo?

Ipi ni historia ya kweli kuhusu Israel na wayahudi wa leo?

Kungarochi

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2020
Posts
271
Reaction score
601
Kumekuwa na mkanganyiko mkubwa kuhusu ukweli kuhusu Israel. Wengi wakidai waisrael wa leo siyo OG ni kikundi cha watu tu waliamua kuja kufanya makazi kwenye ardhi ya wa-Palestine kwa lazima.

Mwenye uelewa anieleweshe wa-Israel wa kwl ni wapi na ipi historia yao kabla ya mwaka 1947.
 
Kasome Biblia utajua waisrael kwao ni wapi.
Hivi wale wamasai waliohamishwa kwa mabavu na kupewa waarabu, siku wakirudi kwao watafikia wapi?
Bado hujajibu swali la mtoa mada.Huko unakomwelekeza akosome ndio atazidi kuchanganyikiwa.Dunia hii inaendeshwa Kwa Siri kubwa hasa katika kuwafanya watu kuwa Mental Slave.
 
Kwa mujibu wa biblia:

Babu yao mvamizi Abraham babu kutoka/mzaliwa Iraq , Yakobo kwao Iraq sio hapo wanapo pang'ang'ania na kupaita pao.
 
Kwa mujibu wa biblia:

Babu yao mvamizi na mporaji Abraham babu kutoka/mzaliwa Iraq , Yakobo kwao Iraq sio hapo wanapo pang'ang'ania na kupaita pao.
Lakini kwa mujibu wa Biblia hiyo aliagizwa atoke kwao hadi kule Mungu alikomwagiza akaanzishe makazi mapya na uzao wake.
 
Lakini kwa mujibu wa Biblia hiyo aliagizwa atoke kwao hadi kule Mungu alikomwagiza akaanzishe makazi mapya na uzao wake.
Alitoka kwao si ndio ? Na wewe si unataka historia ya Yakobo ?
 
Jibu swali kaka mbn kama ugomvi
Nimekwisha kujibu toka hapo mwanzo kabisa kuwa

Babu yao mvamizi Abraham babu kutoka/mzaliwa Iraq , Yakobo kwao Iraq sio hapo wanapo pang'ang'ania na kupaita pao.

Au ulitaka nikujibu pale wanapo pang'ang'ania ni pao ndio ujue nimekujibu ?
 
Kumekuwa na mkanganyiko mkubwa kuhusu ukweli kuhusu Israel. Wengi wakidai waisrael wa leo siyo OG ni kikundi cha watu tu waliamua kuja kufanya makazi kwenye ardhi ya wa-Palestine kwa lazima.
Mwenye uelewa anieleweshe wa-Israel wa kwl ni wapi na ipi historia yao kabla ya mwaka 1947.
Changamoto kubwa kuhusu Wayahudi hapo Israel itakubidi kwanza uamue kujadili kwa mujibu wa iman au akili ya kuzaliwa nayo.

Kwanini nimekupa hizo option 2? Sababu iman unakupa kikomo cha kufikiri ila akili ya kuzaliwa nayo haitakupa kikomo cha kung'amua.

Wayahudi wasasa ni wahamiaji walionza kurejea Palestina mwaka 1917 toka Ulaya Mashariki, waliamua kuamza kurejea mara baada kunyanyaswa sana na jamii za wazungu huko Ulaya hasa mashariki.

Uingereza chini ya waziri wa mambo ya nje Sir Joseph Chamberlain aliahidi kuwapatia eneo wayahudi waliobaguliwa huko Urusi na Ulaya, alipendekeza kuwaleta Uganda 1903 ila Wayahudi walikataa na walianzisha harakati za kurudi Palestina.

Wakati huu Palestina ilikuwa chini utawala wa Otoman Empire ambapo ilikuwa ni moja ya dola yenye nguvu hapa Duniani. Uingereza alifanikiwa kuyarubuni mataifa kadhaa ya kiarabu kama Misri na Jordan kumpiga Otoman Empire kwenye vita ya 1 ya Dunia na hatimae wakamshinda na rasmi eneo la Palestina akapewa Uingereza kama mwanagalizi chini ya League of Nation's.

Uingereza alikuwa katika harakati pia za kuwatafutia eneo la kuishi Wayahudi na hii ilipata nguvu mara baada ya Uingereza kuitawala Palestina, mwaka 1917 Wayahudi walianza kurejea rasmi Palestina huku Uingereza ikipewa jukumu lasmi la kusimamia uundaji wa Taifa la Kiyahudi.

Hatimae mara baada ya Vita kuu ya pili ya Dunia nchi ya Israel iliundwa yaani 1948.

Nirudi kwenye swali lako mama, Je! Wayahudi hawa ndiyo wale wa kale? Jibu ni Hapana.

Inasemekena Wayahudi walitoka huko Palestina 1517 kukimbia manyanyaso ya utawala wa Otoman, na walianza kurejea mwaka 1917 yaani walikaa Ulaya zaidi ya miaka 400! Kiufupi tunaweza sema vilipita vizazi zaidi ya 5! Hapo katika vizazi 5 pamoja na kujamiina na jamii nyingine za Ulaya na Urusi bas ni wazi kuwa waliorejea kuanzisha nchi hawakuwa Wayahudi wale wa kale.


Hapa sijagusa ya utumwani Misri na ya Utawala wa Rumi.
 
Lakini kwa mujibu wa Biblia hiyo aliagizwa atoke kwao hadi kule Mungu alikomwagiza akaanzishe makazi mapya na uzao wake.
Tunaweza tumia biblia kama kitabu cha rejea ila tusitupe akili zetu kando!

Wakati Mungu wake anamuambia aende huko akaishi ndipo kutakuwa kwake, huko hakukuwa na jamii za watu wengine? Inshort zilikuwepo, je! Hawakuwa na haki ya kumiliki hiyo ardhi kwakuwa hawakujiwa na ndoto kama ya Abraham?

Ikitokea umeota ndoto umetokewa na Yesu usiku anakuambia kesho tembea uchi ila kuwa na iman hakuna ataekae kuona! Utatoka uchi siku ya 2?
 
Kasome Biblia utajua waisrael kwao ni wapi.
Hivi wale wamasai waliohamishwa kwa mabavu na kupewa waarabu, siku wakirudi kwao watafikia wapi?
Umeulizwa kuhusu waisrael wa kweli na sio eneo acha kukurupuka..
 
Changamoto kubwa kuhusu Wayahudi hapo Israel itakubidi kwanza uamue kujadili kwa mujibu wa iman au akili ya kuzaliwa nayo.

Kwanini nimekupa hizo option 2? Sababu iman unakupa kikomo cha kufikiri ila akili ya kuzaliwa nayo haitakupa kikomo cha kung'amua.

Wayahudi wasasa ni wahamiaji walionza kurejea Palestina mwaka 1917 toka Ulaya Mashariki, waliamua kuamza kurejea mara baada kunyanyaswa sana na jamii za wazungu huko Ulaya hasa mashariki.

Uingereza chini ya waziri wa mambo ya nje Sir Joseph Chamberlain aliahidi kuwapatia eneo wayahudi waliobaguliwa huko Urusi na Ulaya, alipendekeza kuwaleta Uganda 1903 ila Wayahudi walikataa na walianzisha harakati za kurudi Palestina.

Wakati huu Palestina ilikuwa chini utawala wa Otoman Empire ambapo ilikuwa ni moja ya dola yenye nguvu hapa Duniani. Uingereza alifanikiwa kuyarubuni mataifa kadhaa ya kiarabu kama Misri na Jordan kumpiga Otoman Empire kwenye vita ya 1 ya Dunia na hatimae wakamshinda na rasmi eneo la Palestina akapewa Uingereza kama mwanagalizi chini ya League of Nation's.

Uingereza alikuwa katika harakati pia za kuwatafutia eneo la kuishi Wayahudi na hii ilipata nguvu mara baada ya Uingereza kuitawala Palestina, mwaka 1917 Wayahudi walianza kurejea rasmi Palestina huku Uingereza ikipewa jukumu lasmi la kusimamia uundaji wa Taifa la Kiyahudi.

Hatimae mara baada ya Vita kuu ya pili ya Dunia nchi ya Israel iliundwa yaani 1948.

Nirudi kwenye swali lako mama, Je! Wayahudi hawa ndiyo wale wa kale? Jibu ni Hapana.

Inasemekena Wayahudi walitoka huko Palestina 1517 kukimbia manyanyaso ya utawala wa Otoman, na walianza kurejea mwaka 1917 yaani walikaa Ulaya zaidi ya miaka 400! Kiufupi tunaweza sema vilipita vizazi zaidi ya 5! Hapo katika vizazi 5 pamoja na kujamiina na jamii nyingine za Ulaya na Urusi bas ni wazi kuwa waliorejea kuanzisha nchi hawakuwa Wayahudi wale wa kale.


Hapa sijagusa ya utumwani Misri na ya Utawala wa Rumi.
Kw hyo hapo waliporejea ndo mababu zao waliishi na nasikia kuwa hata kabla ya 1947 jamii ya wayahudi ilikuwepo japo kwa uchache?
 
Mfalme daudi, mfalme Suleman walikuwa wafalme wa nchi gani?
Hiyo nchi ilikuw eneo gani?
Israel ipo toka zamani kama taifa.
Mkimbizi, huwa anakwao siku zote, ndio maana nchini Tanzania, wakibizi wa Burundi 1972, lakini 2008 walirudi nchi yao ya Burundi na mashamba yao walipewa
 
Kumekuwa na mkanganyiko mkubwa kuhusu ukweli kuhusu Israel. Wengi wakidai waisrael wa leo siyo OG ni kikundi cha watu tu waliamua kuja kufanya makazi kwenye ardhi ya wa-Palestine kwa lazima.
Mwenye uelewa anieleweshe wa-Israel wa kwl ni wapi na ipi historia yao kabla ya mwaka 1947.
Swali dogo kwako Ni ujiulize Kama wapalestina walikuwepo toka zamani kwanini wayaudi wasiwepo toka zamani?. Maana unaposema kuwa wa Leo siyo og. Maana yake hakuna wayaudi duniani kwa Sasa.
 
Swali dogo kwako Ni ujiulize Kama wapalestina walikuwepo toka zamani kwanini wayaudi wasiwepo toka zamani?. Maana unaposema kuwa wa Leo siyo og. Maana yake hakuna wayaudi duniani kwa Sasa.
Uyahudi ni Imani Kama uislam na ukiristo,so mtu yoyote anaweza badili dini na kuwa myahudi, muislam hawezi dai Saudi Arabia ni nchi yake
 
Kw hyo hapo waliporejea ndo mababu zao waliishi na nasikia kuwa hata kabla ya 1947 jamii ya wayahudi ilikuwepo japo kwa uchache?
Umesoma historia iliyoandaliwa na mwarabu lazima ikupotoshe. Hitleraliwaua wayaudi zaidi ya milioni 6. Katika Vita ya pili ya dunia alafu mwarabu anakwambia 47 walikuwa kwa uchache. Hahahahaaaa
 
Mfalme daudi, mfalme Suleman walikuwa wafalme wa nchi gani?
Hiyo nchi ilikuw eneo gani?
Israel ipo toka zamani kama taifa.
Mkimbizi, huwa anakwao siku zote, ndio maana nchini Tanzania, wakibizi wa Burundi 1972, lakini 2008 walirudi nchi yao ya Burundi na mashamba yao walipewa
Wafalme wa 'wayahudi' katika nchi ya watu, ndiyo maana daudi alipigana na wafilisti
 
Back
Top Bottom