Ipo haja ya kumuombea Magufuli msamaha, lawama ni nyingi mno

Superbug

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
13,864
Reaction score
35,079
Ndugu zangu Watanzania mimi ni kati ya watu waliomchukia sana Magufuli kwa sababu ya aina ya uongozi ila nimetafakari sana tumsamehe tumuombee.

Sababu zangu

Viongozi wengi hukosea awamu ya kwanza ila ya pili hujirekebisha pengine Magufuli angejirudi katika awamu ya pili ila Mungu hakumpa nafasi.

Hii nchi kweli kuna mambo tulizingua hivyo tulihitaji angalau mtu wa aina yake ila tulikosa speed governer na regulator.
 
Ninataka matajiri waishi kama mashetani , aisee huyu jamaa kumsafisha inabdi ujitoe ufahamu , alikuwa na chuki za wazi mno ...!!
forget and forgive
 
Too late, alishatangulia mbele ya haki, huko atamalizana na Muumba wake.

Cha kujifunza tuangalie jinsi tunavyoishi duniani na wenzetu hata tukiwa juu sana tusijisahau maana hatujui siku wala saa tutakayorudi kwa Muumba wetu !
 

Mkuu naunga mkono hoja ila tu ungeishia na kichwa cha habari na aya ya kwanza.

Ulipoanza kuweka sababu tu, hoja yako ya msingi ikasambaratika mithili ya gunia tupu lisilioweza kusimama likiwa tupu.

Uhalalishe vipi:

1. Ben, Azory na wa namna hiyo kupotea.
2. Mawazo kuuwawa
3. Kina Lissu kupangiwa kuuwawa
4. Nk nk.

Katika awamu ile kulipita uovu mwingi usiokuwa kifani!
 
Labda nikifa nitaenda kumuombe huko huko tukikutana
 
mungu au Mungu??
 
Watu wa kimara wabomoleeni tu hizo nyumba lkn watu wa Mwanza msiwabomolee hao ndio walionipigia kura nikawa rais.

Jamaa kwa kubagua alikua vzr.
Unaweza kunipa hii qoute ad verbatium..., sababu sidhani kama mtu mwenye ubongo anaweza kupayuka hayo maneno let alone kiongozi...
 
Nchi sasa hivi imepumua maana zile amsha amsha zake kila mahali yupo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…