Iran na Uturuki kuunda meli ya kubebea droni kuzipiku meli za kubebea ndege za kivita za Marekani, Urusi na China

Iran na Uturuki kuunda meli ya kubebea droni kuzipiku meli za kubebea ndege za kivita za Marekani, Urusi na China

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mataifa ya Uturuki na Iran yapo mbioni kutengeneza meli kubwa za kijeshi zitakazobeba droni kushambulia adui badala ya zile meli zilizozoeleka na zinazohofiwa ambazo huwa zinabeba ndege za kijeshi kama vile F-16 na F 35.

Tofauti na meli za kubebea ndege za kivita,meli hizo zao la ubunifu wa Uturuki na Iran zitakuwa zikiongozwa kutoka nchi kavu na kutokea ndani ya meli hizo.Droni kutoka meli hizo zitakuwa zinashambulia adui akiwa majini na nchi kavu na baadae kurudi kwenye kituo chao.

Wachunguzi wa kijeshi kutoka mataifa ya Ulaya na Marekani wamesema athari ya meli hizo kijeshi zinaweza kuwa kubwa kuliko hizi meli za sasa zilizozoeleka.

Marekani iliwahi kuinyima Uturuki vifaa na teknolojia ya kumalizia meli yake ya kivita iliyokusudiwa kubeba ndege za F 35.Hapo Uturuki ikaifanyia mabadiliko meli hiyo kuweza kubeba ndege waliyoibuni wenyewe pamoja na droni zao maarufu za Byraktar.

Iran and Turkey are betting on drone aircraft carriers to project power

1725726521045.png
 
Kuunda ni jambo moja, lakini je, itaweza kuhimili mikimiki iwapo vita vikitokea?
Ndio inaonekana ni rahisi kuitumia kuliko meli za kubebea ndege kwani.tofauti na hizo meli nyengine hizi zitakuwa zikiongozwa kutoka ardhini mbali na ilipo meli.
Droni unaweza ukaziongeza au ukazirudisha ardhini kuzitengeneza kirahisi.Lakini meli za akina Marekani ni lazima uirudishe nyumbani kujaza makombora.Ndio maana zimeshindwa kuhimili vishindo vya Houth pale bahari nyekundu.
 
Waarabu wao wanasubiri nini?
Wao watusubiri kutengenezewa ma usa wataenda kuzinunua kwa mabilion ya dollar. Usa huwa anafurahia sana na ikitokea nchi ya kiaribu ikawa inajitegemea huonekana kama adui na tishio kwa maslahi ya USA na Israeli. Nchi kama saudia ilipaswa kuwa na military industry yeka na si kuitegemea West kwa kila kitu
 
Unasimulia kama upo iran hata source yako haileweki! Hizo si ndizo akili za kibabu kweli…tulikubaliana humu kunahitajika magreater thinker ktk kuchambua mambo tupasayo kuelimishana
 
Ndio inaonekana ni rahisi kuitumia kuliko meli za kubebea ndege kwani.tofauti na hizo meli nyengine hizi zitakuwa zikiongozwa kutoka ardhini mbali na ilipo meli.
Droni unaweza ukaziongeza au ukazirudisha ardhini kuzitengeneza kirahisi.Lakini meli za akina Marekani ni lazima uirudishe nyumbani kujaza makombora.Ndio maana zimeshindwa kuhimili vishindo vya Houth pale bahari nyekundu.

Dah kaka hebu rudi tena kasome hizo warship aircraft carrier uwezo wake inaelekea unaandika kwa hisia kuliko uhalisia.. hv unajua warship aircraft carrier moja ya marekan inabeba jet fighter ngap.. halafu eti zimeshindwa kuhimili houth..

Hebu ingia youtube search top ten za warship aircraft carrier dunia bila kujali zinatokea wapi angalia uwezo wake.. we unadhan warship aircraft carrier ni kwa ajili ya ku lunch jet fighter tu..

By the way US active warship aircraft carrier ziko 47 achana na nchi marafiki wa Europ..
 
Wao watusubiri kutengenezewa ma usa wataenda kuzinunua kwa mabilion ya dollar. Usa huwa anafurahia sana na ikitokea nchi ya kiaribu ikawa inajitegemea huonekana kama adui na tishio kwa maslahi ya USA na Israeli. Nchi kama saudia ilipaswa kuwa na military industry yeka na si kuitegemea West kwa kila kitu
Akili za mwarabu ni kama za mwafrika, Zero creativity, Zero innovation. Kazi kusubiri ready made tu, kutengeneza vya kwao ahahaha
 
Dah kaka hebu rudi tena kasome hizo warship aircraft carrier uwezo wake inaelekea unaandika kwa hisia kuliko uhalisia.. hv unajua warship aircraft carrier moja ya marekan inabeba jet fighter ngap.. halafu eti zimeshindwa kuhimili houth..

Hebu ingia youtube search top ten za warship aircraft carrier dunia bila kujali zinatokea wapi angalia uwezo wake.. we unadhan warship aircraft carrier ni kwa ajili ya ku lunch jet fighter tu..

By the way US active warship aircraft carrier ziko 47 achana na nchi marafiki wa Europ..
Bado una mawazo ya kizamani kuangalia ukubwa wa kitu badala ya ufanisi wake.
Unajua hata ndege za kusafirisha watu na mizigo za masafa marefu sasa zinatumia injini ndogo tu lakini zina ufanisi mkubwa kuliko zile jet engine za zamani.
Sasa ukubwa wa meli za kijeshi za Marekani na wenzake zina umuhimu gani kwa sasa wakati ndege za kivita zinapigwa na droni kabla hazijaruka.
Na sijui una hofu gani ya kukubali kwamba Houth imeshindikana kuwadhibiti wakati makamanda wenyewe wa kijeshi wa wMarekani wameshaliweka wazi hilo baada ya kupata hasara kubwa kuwadondoshea mabomu mazito ya gharama.,Baada ya siku chache wanaonekana kurudia kazi zao za kuzipiga meli zenye uhusiano na Israel
 
Kuunda ni jambo moja, lakini je, itaweza kuhimili mikimiki iwapo vita vikitokea?
Hizi inchi sijui iran , au uturuki huwa nachekaga mmarekani ataendelea kua juu kaaanza kua na meli za kivita toka 1890 huko
 
Hizi inchi sijui iran , au uturuki huwa nachekaga mmarekani ataendelea kua juu kaaanza kua na meli za kivita toka 1890 huko
Muda wa meli za kivita kama hizo umekaribia mwisho.
Karibuni utaona fikra za Uturuki na Iran zinafanyiwa kazi.Ujue kuwa akili sote tumepewa sawa.
 
Kuongea ni jambo moja ila kufanya ulichoongea ni jambo lingine
 
Back
Top Bottom