Iran yatoa Onyo kwa nchi yoyote ya Kiarabu itakayoruhusu Israel na Marekani kutumia anga au ardhi yake kushambulia Iran itaadhibiwa vikali

Wakati unaandika huu utumbo kuna nchi za kisunni kama Qatar na Oman zimeikaribisha Iran na zimekubaliana nayo kufanya biashara.
 
Iran anajua kuwa kwenye vita na USA Shah watarudi madarakani
Iran sio nyepesi kama unavyodhani.
Kama ingekua nyepesi ingeshavunjwa utawala wake miaka ile ya 1980s ikiwa bado nchi dhaifu.
Ila sasa ishakita mizizi no way unaweza iangusha Iran.
Hao USA wenyewe wanajua sio rahisi ndio maana kila siku wanaishia kutishia tu.
Unaizungumzia nchi iliyopigana vita miaka nane consecutively.
 
Kwa bahati mbaya sana viongozi wa nchi nyingi za Waarabu ni wale tunaowaita wanafiki na wamewekwa kwenye mamlaka yao na USA ikisapotiwa na Israel. Yani hapo Jordan, Saudi, Misri, UAE etc zote viongozi wao ni vibaraka wa USA na Israel na ndio maana huoni hata wakikemea dhuluma ya Israel dhidi ya Palestina.

Hawa viongozi wao wanachojali ni maslahi yao tu hawajali chochote wala hawapo hapo kuwatetea wanaoonewa, infact wenyewe wanawaonea wananchi wao na katika hizo nchi hakuna demokrasia na hakuna uchaguzi. Lakini kamwe huwezi kusikia USA au UN wanasema hao viongozi kuwa ni madikteta. Kwa dunia ya leo Dikteta ni kiongozi ambaye hataki kufata masharti ya USA mfano Saddam na Gadafi au Mugabe lakini wanaotii kamwe sio madikteta.

Hawa viongozi waliowekwa na USA na Israel wanahakikisha wanalinda maslahi ya waliowaweka vinginevyo wanapinduliwa, na wote wanalindwa na USA na Israel. Na hawataweza kwenda kinyume na makubaliano yao na mabwana zao otherwise watakuwa eliminated. Hawa wameuza ubinadamu wao kwa mali na vyeo

Kwa hivyo ni ngumu sana hawa viongozi kubadilika labda kama yatatokea mageuzi kwenye nchi zao waondolewe madarakani. Na sisi tunaombea hilo na ninaamini ipo siku wataondoka na kupatikana viongozi wema na hapo ndio utakuwa mwisho wa Israhell.
 
Yaani yeye iran ametumia anga la saudia iraq, jordan, misri kuishambulia israel na mabalstic yake halafu israel asitumie anga yeyote huu ni upuuzi?
 
Ameshajiona ndio kiranja wa wavaa kobazi wote ?
 
Wakati unaandika huu utumbo kuna nchi za kisunni kama Qatar na Oman zimeikaribisha Iran na zimekubaliana nayo kufanya biashara.
Yani itanatia aibu sana mkuu kuona jinsi graduates wa Tanzania walivyoweupe upstairs, haswa katika mambo madogo kama haya. The problem is vijana hawana utamaduni wa kujisomea. Wao wakishamaliza shule, ni mpira, umbea, na kubeti. Mtu hata anashindwa kujua simple facts!.
 
Yaani wao Iran watumie anga za wengine kurusha makombora kwenda Israel, ila Israel isitumie hizo hizo anga kulipiza? Upuuzi huo
Habari haisemi Israel kutumia anga bali inasema Marekani kutumia anga.

Tafsiri yake ni kwamba hizo Gulf states kuna kambi nyingi za kijeshi za Marekani.

Alupo Israel na Amerika yupo! Iran asisitiza ikiwa hizo nchi zikaruhusu kambi za kijeshi za Marekani zitumike kumpiginia Israel dhidi yake naye atarudisha mapigo ndani ya hizo nchi.

Ikiwa Marekani inataka kumsaidia Israel imsaidie moja kwa moja kutokea nchini kwake.
 
Sasa mbona anahangaika yeye SI anajidai ni supapawa la kiarabu akae kwa kutulia tu.
 
Yani wanachukulia mambo rahisi rahisi hivyo.
Hao licha ya kutofautiana madhehebu ila ni ndugu ikifika kipindi cha Hijjah wote wanakutana sehemu moja Mecca na Medina.
Sasa haiwezekani wewe wa nje uje uwaletee ugomvi wa kudumu halafu wakuangalie tu na wakutii miaka yote.
 
Hasara to which levels? Iran wali declare kuwa wanahusika na hizo attack?

A perfect attack ni kumuumiza adui asiweze kuendelea na operation zake. But then saudi ndio wana uchumi mkubwa kuliko iran, probably wana jeshi bora sasa kuliko nyuma

Tunarudi pale pale iran hamna kitu atafanya ni biti tu for nothing
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…