Iran yatoa Onyo kwa nchi yoyote ya Kiarabu itakayoruhusu Israel na Marekani kutumia anga au ardhi yake kushambulia Iran itaadhibiwa vikali

Iran yatoa Onyo kwa nchi yoyote ya Kiarabu itakayoruhusu Israel na Marekani kutumia anga au ardhi yake kushambulia Iran itaadhibiwa vikali

Tatizo ni Iran au Saudia ?

Unataka Saudia awasaidie Palestine kupitia nini ? Kama tu kashindwa kuungana na Sunni wenzake kuwasaidia Wapalestina kitu ambacho hata Shia kamshinda.

Hivi unafahamu kuwa Saudia ipo katika mchakato wa kufanya normalisation na Israel ?
Hakuna ulazima wa Kuisaidia Palestina, hili lazima kila mtu alijue... Kama Wapalestina wanataka Msaada wa mtu lazima wasikilize Masharti ya mtu wanayemuomba msaada.

Hili jambo Watu wengi mnaliruka sana
 
Kituo kinachofuata baada ya Beirut ni Tehran
Nyonzo bin mvule njoo umuone mlokole uliyesema anatokea kanisa la mabati lenye viti vya bar anavyobwabwaja huku.

Yaani nyie watu mmeaminishwa ujinga vibaya sana. Israel huyu huyu aliyetwangwa mara mbili ndani ya ardhi yake ndiyo awe na uwezo wa kuishambulia Iran?

Iran ndiye mbabe wa kweli mashariki ya kati achana na fiksi za wachungaji uchwara. Fungua ubongo.
 
Iran imetoa ONYO kuwa nchi yeyote ya kiarabu itakayosaidia Israel na marekani kuishambulia basi itakumbana na matatizo makubwa.

Iran imechukua msimamo mkali dhidi ya majirani zake baada ya kutoa onyo kali kuhusu ushirikiano wowote na Israel kwa ajili ya operesheni za kijeshi.

Msimamo huu mkali ni sehemu ya mkakati wa Iran kuzuia nchi za kiarabu kushirikiana Israel. Maafisa wa Iran wamesisitiza umuhimu wa "umoja wa kikanda" kukabiliana na kile wanachokiona kama tishio kutoka Israel, huku wakieleza pia umuhimu wa kudumisha utulivu huko Mashariki ya Kati

Soma pia: Israel kuishambulia Iran leo usiku, Marekani yaja juu

Onyo hilo halihusishi tu matumizi ya anga, lakini pia Iran inafuatilia kwa karibu uwezekano wa ushirikiano wa vituo vya kijeshi vya Marekani vilivyoko katika eneo la Gulf

Kwa mujibu wa vyanzo vya kidiplomasia, msimamo wa Iran uliwekwa wazi wakati wa mkutano wa hivi karibuni huko Doha.

Ujumbe ulikuwa wazi: taifa lolote la Gulf States litakaloruhusu anga yake au vituo vyake vya kijeshi kutumika kwa operesheni dhidi ya Iran litakabiliwa na kisasi.

Tehran inachukulia vitendo hivyo kama uamuzi wa pamoja wa mataifa yote ya Gulf, jambo ambalo linaweza kupanua wigo wa majibu yake.

Kazi kwako Saudi Arabia na vibaraka wengine wa marekani hapo Middle East .


naunga mkono hili onyo...haswa hao saudia wakijikoroga tu warudishwe kwenye jangwa km zamani
 
Nyonzo bin mvule njoo umuone mlokole uliyesema anatokea kanisa la mabati lenye viti vya bar anavyobwabwaja huku.

Yaani nyie watu mmeaminishwa ujinga vibaya sana. Israel huyu huyu aliyetwangwa mara mbili ndani ya ardhi yake ndiyo awe na uwezo wa kuishambulia Iran?

Iran ndiye mbabe wa kweli mashariki ya kati achana na fiksi za wachungaji uchwara. Fungua ubongo.

Walishakaririshwa hawa watu, daima wako upande wa wasio waislamu, isipokua baadhi wenye kujitambua, hata Qur'an imeshawazungumzia hawa watu, hawatakua radhi nasi mayahudi na Manaswara mpaka tufuate mila zao
 
Kituo kinachofuata baada ya Beir Tehran
Dah! hao watu noma sana, labda ukiandika watakusoma wakiwa wenyewe majumbani mwao. Iakini ukikutana nao mahala hawasikilizi hoja wala kioja wanaongea wao tu huku wamefumba macho.hawajali kama unawaelewa au la!(wanatumia ile mbinu ya ukitaka kumuua Nyani usimuangalie usoni.
 
Vipi mkuu tukalime viazi? Haya mambo waachie waajemi, wale wanatengeneza nucleur, wewe hata njiti ya kiberiti huwezi halafu unawasema! Are you serious?
Haha,
Ninaowasema ni hawa chawa wa waajemi wa humu jF waliojichimbia huko Buza kwa Mpalange badala ya kwenda front wakalipuliwe
 
Iran anatafuta mtu wa kufanya naye, anajua kilichoko mbele yake siyo kizuri, mbele haoni mwanga anaona giza, ametengeneza mazingira zaidi ya Sadamu Huseni, USA na Israel hawezi kuacha adui atamalaki na kutishia maslahi ya USA na kulifuta taifa la Israel,
 
Kama sikosei Saudia,Jordan,Bahran,Kuwait,Oman,Falme za Kiarabu,baadhi ya hizo zina mikataba ya Ulinzi na US nyingine na Israel(Azerbaijan)
Baadhi ya hizo zina Military Bases za US.
Sijui itakuwaje!
Iran isipoangalia inatafutwa kwa mfano wa sababu zile zile zilizotumika kuipiga Iraq (Saddam)!
 
Kiongozi, mimi najua kinachoendelea ME kuliko wewe.

Mimi ni sunni na nina ndugu Yemen ambao ni sunni.

Najua kilichotokea Yemen kwa undani kuliko wewe.

Najua kinachoendelea Syria kuliko wewe. Sheikh Muhammad Al Hudaa Al Yaaqoubi msimamo wa kwanza alidhani kama wewe ambaye ni Sunni. Baadaye alibadilisha msimamo wake.

Sheikh Said Ramadhan Al Bouti ni mwanawazuoni mkubwa sana wa kisunni. Kauliwa na hao hao Isis ambao Saudi Arabia alikuwa aki fund operation zao kisa Sheikh Al Bouti aligundua hila zao na kuwa pamoja na Bashar Al Assad.

Tena aliuliwa ndani ya msikiti na bomu la kutegwa. Alikufa yeye pamoja na mjuu wake na watu wengine 42 na 84 wakiwa maeruhi.

Katika haya uliyoandika huwezi kuniongopea hata nukta.

Saudi Arabia walishaiuza Palestina kitambo na miaka ya nyuma kama siyo 2003 au 2005 mwakilishi wa Saudi Arabia alizomewa na wapelestina na wengine kumtaka aondoke. Mohammad Bin Suleyman alivyokuwa crown prince aliwataka wa Palestina wakubaliana na matakwa ya Israel kabla hata hii vita yao ya oktoba kuanza.

Sijisikii kuandika sana naishia hapa!
Mkuu kwani kwa sasahivi wapalestina wanataka nini na terms zao zipoje
 
Kama sikosei Saudia,Jordan,Bahran,Kuwait,Oman,Falme za Kiarabu,baadhi ya hizo zina mikataba ya Ulinzi na US nyingine na Israel(Azerbaijan)
Baadhi ya hizo zina Military Bases za US.
Sijui itakuwaje!
Iran isipoangalia inatafutwa kwa mfano wa sababu zile zile zilizotumika kuipiga Iraq (Saddam)!
Hii kuna clip moja ya historia nilicheki wanasema saddam walimuongopea ili aingie kingi


View: https://youtu.be/hxW_Oe-76no?si=rgpRD6kk0j3h8TRH
 
Iran na Saudi Arabia kwa sasa wamerudisha uhusiano uliokuwa umelega lega kwa zaidi ya miaka 20 na ubalozi umerejeshwa kwa nchi zote 2
Kwa taarifa yako uelewe kwamba Israel ni muhimu kwa Saudi Arabia kuliko Iran na Saudi Arabia anaelewa kwamba Wairan ni makafiri tu.
 
Kwa taarifa yako uelewe kwamba Israel ni muhimu kwa Saudi Arabia kuliko Iran na Saudi Arabia anaelewa kwamba Wairan ni makafiri tu.
Ki namna gani
 
Wakati unaandika huu utumbo kuna nchi za kisunni kama Qatar na Oman zimeikaribisha Iran na zimekubaliana nayo kufanya biashara.
Hizo ni porojo tu za masjid ubwabwa, hata siku moja wasunni hawawezi kuelewana na washia wanaoamini ni makafiri tu kama makafiri wengine.
 
Hapo ndio mwisho wa Israel na mwenyewe anajua hilo. Si umeona mpaka sasa kimya tangu apigwe kipigo kitakatifu tarehe 1 oktoba.
Soon tutasikia free Iran.

Mwanzo watu walidai Hezbula ni kiboko ya Isarel mwaka 2006 alikimbia, wakadai anawaonea Gaza. Sasa Hezbu wanaomba poo (pause) bila masharti ya kuihusisha Gaza huku mtarajiwa wa mrithi na mtarajiwa wa mrithi wa mrithi wakiungana na mrithiwa.

Yeye Iran anasema akipiga mkwara kwa nguvu zake hajui kimo cha nguvu za wengine.

Kikubwa ameyavulia nguo. Kitajulikana na uwanja wa vita utaamua, na hii inaweza ikawa jumlajumla maana mlengwa hapo ni Ayatollah.

Nakumbuka Iraq alitoa mkwara kama huo, mwisho wa siku ndio hivo tena.

Bila Urusi kuwa bize, ingekuwa ngumu kumpiga Iran, kama ilivyokuwa Syria. Sasa Urusi yupo bize na yake, yafaa sasa kulianzisha na huyu Iran.
 
Hao warabu wajinga sana wanaweza hata kwenda na wao kushambulia Iran wanacho ambiwa na US wanakubali.

Lakini na uhakika 💯 atazipiga kweli hizo nchi tatu vibaya sana wakishiriki kwa njia moja au ingine..
 
Back
Top Bottom