#COVID19 Iringa: Mikusanyiko yazuiwa kudhibiti Corona

#COVID19 Iringa: Mikusanyiko yazuiwa kudhibiti Corona

"The creatures outside looked from pig to man ,and from man to pig, and from pig to man again,but already it was impossible to say which was which"
 
Ha ha ha ha .haka kanyimbo Cha korona kazuri sana.safi sana.l! hakuna makongamano kuruhusiwa,Wala sijui mikutano/makongamano ya katiba.cdm kazi mnayo haya Sasa ,si mlisema hatua hazichukuliwi ,Sasa msilie lie Tena.
 
Amejua kuwa cdm kituo kinachofuata baada ya mwanza Ni Iringa. Hongera kwa ushushu
 
Mara Kagera mara Iringa.Bora iwe nchi nzima ili kukabiliana na janga hili la corona.Waziri wa afya usichukulie poa jambo hili. Wewe ndiwe mwenye dhamana na wizara ya afya.Pigeni marufuku mikusanyiko isiyo na ulazima nchi nzima.
 
Mkuu wa mkoa wa Iringa, Queen Sendiga amesitisha kwa muda shughuli zote zisizo za lazima zinazohusisha mikusanyiko pamoja na makongamano yasiyo ya lazima, ikiwa ni moja ya jtihada za mkoa huo katika kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona
Mnasingizia corona 😂
 
Mara Kagera mara Iringa.Bora iwe nchi nzima ili kukabiliana na janga hili la corona.Waziri wa afya usichukulie poa jambo hili. Wewe ndiwe mwenye dhamana na wizara ya afya.Pigeni marufuku mikusanyiko isiyo na ulazima nchi nzima.
Huyo mkuu wa mkoa Kuna watu kawalenga ishu sio korona,(Msigwa na cdm on target)
 
Mkuu wa mkoa wa Iringa, Queen Sendiga amesitisha kwa muda shughuli zote zisizo za lazima zinazohusisha mikusanyiko pamoja na makongamano yasiyo ya lazima, ikiwa ni moja ya jtihada za mkoa huo katika kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona.

Sendiga amesema wamefikia uamuzi huo baada ya kuona maambukizi ya virusi vya corona mkoani Iringa yanaendelea kuongezeka.

Amewataka Wananchi wa mkoa wa Iringa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya corona ikiwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka, na kuvaa barakoa wawapo katika maeneo yenye watu wengi ikiwa ni pamoja na kwenye vyombo vya usafiri.

WhatsApp-Image-2021-07-22-at-11.32.07.jpeg
Mbona mauzauza yanazidi!
Waziri Dr. Nchemba kama sikosei Alitalia wazi kuwa tunahitaji fedha za wahusani tuweze kudhibiti kupambana na Covid-19 kuweka maji tiririka mashuleni! Hivi zilipojengwa hizo shule kwa nini mkondo wa maji haukuwekwa na isitoshe hivi inaingia akilini nchi nzima swala la.maji limeenda kuwa kituko kila awamu! Sasa huyu anasema kunawa maji tiririka akijua wazi watu wanachota maji Ruaha!
Jengeni miundo mbinu ya maji acheni siasa.
Katiba mpya ipo palepale uoga hautasaidia kizazi kijacho!
 
Naona sasa ni mwendo wa Barakoa kwa kwenda mbele
 
Back
Top Bottom