Iringa: Watoto 19 wafanyiwa unyanyasaji wa kulawitiwa na mtoto wa miaka 15

Iringa: Watoto 19 wafanyiwa unyanyasaji wa kulawitiwa na mtoto wa miaka 15

luangalila

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2014
Posts
6,346
Reaction score
6,928
Hii habari niliyo isikia punde toka katika taarifa ya habari ya Ufm

Ni huko Iringa mitaa ya Kiesa ambapo mtoto mmoja wa umri wa miaka 15 anaedaiwa kuwalawiti watoto wenzie zaidi ya 10 kwa kuwahadaa kwa vipipi na kuwawashia luninga nyumban kwao kisha kuwafanyia mchezo huo mbaya wa kikatili, kwa mujibu wa taarifa mtuhumiwa alianza mchezo huo tangia mwaka 2019 alipohamia mtaa huo, taarifa pia inasema mtuhumiwa kwa sasa yupo chin ya jeshi la Polisi

Hii ni wake up call kwa wazazi tuongeze umakini kwa watoto tuangalie ni nani anacheza nae na tabia za hao watoto, sasa imagine kototo cha miaka 15 kinawalawiti wenzake

--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Iringa: Watoto 19 walawitiwa na mtoto mwenzao

Watoto 19 wenye umri wa kati ya miaka minne hadi 14 wa eneo la Kihesa Kilolo Mkoani Iringa wamegundulika kuwa wamefanyiwa vitendo vya ukatili kwa kulawitiwa na mtoto mwenzao mwenye umri wa miaka 15 ambaye alianza kufanya vitendo hivyo kuanzia mwaka 2019 baada ya kuhamia mtaa huo.

Mmoja wa waathirika, mtoto mwenye umri kati ya miaka sita mpaka tisa amekuwa akidanganywa na mtuhumiwa kwa kupewa zawadi ndogondogo na kupelekwa nyumbani kwao kutazama runinga ambapo ndipo vitendo hivyo vimekuwa vikifanyika.

Hata hivyo, mtuhumiwa huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa uchunguzi zaidi.

“Jumamosi tulienda kuwachunguza watoto afya pale Frelimo (hospitali), tukakuta wapo vizuri lakini wa kwangu ndiyo ambaye alikutwa amelawitiwa zaidi na kuharibika, naumia sana kwa hili,” alisema mzazi mmoja.

Naye, Elizabeth Swai ambaye Mkuu wa Dawati ya Watoto na Jinsia Mkoa wa Iringa amewaambia wakazi wa eneo hilo kuwa:

“Idadi ya watoto waliofanyiwa ukatili huo inazidi kuongezeka, tulipokuwa Kituo cha Polisi tuliendelea kumfanyia mahojiano mtuhumiwa akatutajia watoto wengine watatu, nao walipokuja wakataja wenzao wengine.

“Mpaka sasa kesi hii imefikia watoto 19 wameletwa pale kwetu na idadi inaendelea kwa kuwa wanaendelea kutajana.”


Source: UFM
 
Huyo Miaka 15 anajitambua kabisa inawezekana balehe ilikua inamsumbua
 
Dah Mungu atusaidie na hawa watoto wetu wa kiume yaani hizi enzi zimekua ngumu sana..
 
MIAKA 15 INATOSHA KUANZA KUTUMIKIA KIFUNGO, SIKU HIZI WATOTO WANAKUWA HARAKA SANA KIAKILI KULIKO KIMWILI

KWA MAANA NIYINGINE ANAJITAMBUA HUYO ACHA AKAOZEE JELA
 
Ukimfuatilia huyo mtoto wa miaka 15 lazima na yeye alifanyiwa ukatili au ameshuhudia ukatili wa hivyo.

Tatizo wazazi au walezi wanaficha mtoto anapofanyiwa hivi vitendo ili "kuondoa aibu" bila kumtibu mtoto. Matokeo yake victim anakuwa perpetrator.

Tukiendelea na trend hii, Mungu atuepushie, ila tunajenga vizazi hatari sana.
 
Dah Mungu atusaidie na hawa watoto wetu wa kiume yaani hizi enzi zimekua ngumu sana..
We are the people our parents warned us about.
Sasa unaanza kumlinda mtoto dhidi ya watoto wenzake. Nina kitoto cha kike kina miaka 7, watoto wenye umri wake siku moja akiwa ndani nawakuta wanachungulia getini eti wanamwita mchumba na kumrushia mabusu 😳
 
Mmmh ni hatari kwa kweli, Dunia inazidi kuangamia. Ili tendo la ulawiti limeshamiri Sana Kwa wakati huu, asa kwa watoto wetu wa kiume. Inahitaji uangalizi wa juu na kumkagua mtoto Kila wakati. Mungu atulindie vizazi vyetu jamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda kupenda penda Pipi ndio kinachowasumbua [emoji848] ila huyo Dogo lazima haojiwe vizuri inawezekana haka kamchezo alikaona sehemu au alishafanya huu uhuni
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Umakini mkubwa unahitajika katika malezi ya watoto,watoto wasitoke tu majumbani pasipo walezi kujua wako wapi na sehemu walipo je ni sahihi wao kuwa kama ni ya kucheza.
 
MIAKA 15 INATOSHA KUANZA KUTUMIKIA KIFUNGO, SIKU HIZI WATOTO WANAKUWA HARAKA SANA KIAKILI KULIKO KIMWILI

KWA MAANA NIYINGINE ANAJITAMBUA HUYO ACHA AKAOZEE JELA
wew bwege ushawahi kupelekwa japo post acha kubwabwaja sasa kama mtoto wako anapelekwa lupango utsjisikia poa
 
Back
Top Bottom