Is It Possible?

Pole sana AD,

Naona hii mioyo imebeba mazagazaga mengi sana,

Mshukuru mungu wako kwa kukuwezesha kumalizana na hilo timbwili...

Babu DC!

DC,

Nishapoa bana thanks...................

Off topic: Kwanini huwa unanichanganya sana na AD????
 
Asprin ndg yangu! Binafsi siwezi achilia mbali kurudiana huo urafiki tu NO! Yaani hii thread imenikumbusha machungu ambayo nilikuwa naanza kuyasahahu, mimi hata salamu sina huo muda kabisa labda kwasababu yeye huwa anaanza kunisalimia


 
Inawezekana kama hamkuachana kwa mbwembwe sana...mnaelewana na kila mmoja amesonga mbele na maisha yake.
Zaidi ya hapo utakua unajitafutia matatizo tu....

Binafsi nadhani ni vizuri kukawa na mipaka ya shughuli gani mnaweza kushirikishana na hata kama mnaelewana ili kuwafanya na wale wanaokuzunguka (ndugu/marafiki/mume/mke mpya/mpenzi) wawe na amani. Kutoka na watoto...lets say on their birthdays isn't a bad idea..alafu kama unataka amani itawale pia kwa wenza wenu wapya mnaweza mkawaalika na wao ili msiwe wenyewe na kuruhusu mambo mengine kuendelea au hata kuhisiwa.
 
Ninakubaliana na wewe kabisa Mkuu.

MJ1 nilichojifunza mimi katika maisha ni kuwa kuachana na mtu does not necessarily mean mmekuwa maadui ,.

1. Nimebakisha hizo za rangi kwa sababu they're my poin tof discussion. Ni kweli namna mlivyoanza uhusiano inaweza kuchangia kama baada ya kutengana muendelee kuwa marafiki, lakini nahisi hutegemea zaidi jinsi mlivyoachana. Inawezekana mlikuwa marafiki wa muda mrefu, inawezekana pia mlikuwa katika katika uhusiano wa miaka mingi, lakini ikiwa wakati wa kuwachana/kutengana mlifanyanya kiadui adui, si rahisi kuendeleza urafiki, ingawaje pia inawezekana. Binadamu tupo wa aina nyingi na wengine wako kama committed kubakia pamoja daima. Nafikiri sote tumewahi kuona mifano ya watu wanaoachana kwa kugombana, kutukanana, kufikishana kwenye vyombo vya sheria... badae hao hao wanarudiana kama hakukutokea chochote. Na nyinyi mliokuwa mnashabikia upande mmoja au mwengine mnabaki na macho ya kichina.

2. Suala la mila na tamaduni linachangia sana. Umetoa mifano ya wazungu kwa sababu kwao urafiki una thamnai kuliko kwetu (au pengine kwa wao ni hypocrisy tu). Sisemi kwa Waafrika haiwezekani, lakini mifano kama ipo ni michache sana.

3. Inahusiana na 1. hapo juu. Mnaweza kutengana kwa sababu tu tabia zenu haziwawezeshi kukaa chini ya paa moja kwa muda mrefu, lakini bado angalau mnatakana, kama sio kupendana. Kwa nini msiendeleze libeneke kwa rythm yenu baada ya kutengana?

4. Kama hitimisho, uhusiano wa baada ya kutengana unategemea zaidi sababu na mazingira ya kutengana kwenu. Wazo binafsi: Kiustaarabu na kwa kufuata kauli ya Bishanga hapo juu, kutengana/kuwachana hakupaswi kufanananishwa na kufungua ukurasa wa chuki bali kuanzisha mpya wa urafiki.
 
hapo ww 2 hisia zako, kwan kuachana ni bifu, labda mkataba wao ulikwisha
RAIM, uko right kabisa mydia, kuachana katu si bifu but sometimes inapokuwa mmoja wenu hakubali muachano, kwa sababu anazozijua yeye na wazi si kwa kuwa anakupenda basi nadhani hapo hunabudi kuigeuza kuwa bifu. Mimi huyu mwanzoni alikuwa ananitake for granted, niliachana naye smoothly (including giving him second chances nyingi tu ili kama anaona bado ananihitaji kama nilivyokuwa namhitaji mimi, aweke wazi na kujirudi. Unfortunately zile second chances akaziabuse, akaendelea na maisha yake aliyoyataka. Mpaka niliposema nimetosheka naomba tukubaliane juu ya hili kwani ni wazi hanihitaji na mimi sioni sababu ya kuendelea kumng'angania. So alipoona nabadili mwelekeo, niko kivyangu na my kid, ndio akaanza visa vya kwapa.
 
Asprin ndg yangu! Binafsi siwezi achilia mbali kurudiana huo urafiki tu NO! Yaani hii thread imenikumbusha machungu ambayo nilikuwa naanza kuyasahahu, mimi hata salamu sina huo muda kabisa labda kwasababu yeye huwa anaanza kunisalimia
Khaa! Una roho ya kijasiri eh? Au ulikuwa haumpendi?
 
Inawezekana. Its a matter of will, if you have a heart made of stone you can do that, but a heart like mine am not sure, inawezekana lakini.
Duh, ni kamtihani hakoo
April am telling you, hiyo level niliyokuwa nimeiweka I was struggling to death, sasa bado mtu ananiambia niongeze?? Hivi nyie kina baba, umuabuse mwenzi wako, including vipigo vya kila mara na bila kuangalia ni barabarani au la, umfanye atake responsibilities zako simply because anafanya kazi, na bado umdhalilishe but yeye aendelee kukuheshimu kwa kukupa nafasi ya kuja kuwaona wanao, wanao wanaumwa wewe hujui wanatibiwaje (na si kuwa huambiwi, ila ukiambiwa ndo unakata mawasiliano only to wait usikie kuwa wanaendelea vema au wamepona ndio unakuja kuwachukua kwa matembezi na show offs, hujui wanao wanakula nini, wanavaa nini sana sana ukija ukakuta wamevaa nguo ulizowahiziona unakazana kuuliza hivi hawa hawana nguo nyingine??- unatizamwa kimya bila hata kufanyiwa vurugu. Halafu bado unatoka unalalamika kuwa unaonewa ! ah kusema ukweli najiona nimekuwa malaika vya kutosha, now I need that Devil in Me, kwa kweli
 
Pole sana mpenzi ........hawa viumbe wanaweza kukusababisha uwe shetani bila kujijua.

 
naamini kuacha au kutengana huwa kuna sababu ambazo zinaweza kuwa za msingi kwa wahusika na zinaweza kuwa zimechangiwa kutokana na misukumo fulani .. na kabla ya kutengana rasmi kutakuwa na kipindi cha mpito wakati wa tatizo .. kwa vyovyote ni lazima iache majeraha na mara nyingi inapandikiza chuki kwa kutokuelewa au kuwa na ugumu wa kusamehe
 

Mamii hata hivyo una moyo wa kipekee my dia, mimi huwa namwambia unaona nacheka na wewe vizuri kwa sababu unampenda mwanangu lakini ingekua ndivyo sivyo hata huyo mtoto asingekua ana muona angelazimisha ningemlaza hata polisi walahi. Wengine hatuna budi kupiga nao stori kwa ajili ya maslahi ya watoto sasa huyo hata hajui mtoto akiumwa anatibiwaje siku akija sikia ashaaga dunia? na wala hajui anakula nini ningekua mimi hata nikikutana nae no salam akinisalimia namuwasha kibao ili azinduke, wa kazi gani sa mtu wa hivyo?
 

hahahahah...roho ya MJ1 bwana inamtosha mwenyewe, sio ya kuiombea hata kidunchu, kuumia anaumia but anachelewa kuchukua maamuzi tena magumu na yacyo na mazoea, huyu kaka kila cku nasemega alimpata mwanamke(MJ1) hatakaa apate tena......angekuwa ni mie huyu mtoto angeenda kumwona skul 2, kwangu mazoea(hapa nicngetaka kuckia cjui namnyima mtoto haki yake)...
 
Asprin unataka niongee hapa hata ambayo sitakiwi kuyaweka hapa, kifupi ni kwamba yule kaka alinisumbua sana, aliwadharau wazazi, wasimamizi wa ndoa, wachungaji hadi mahakama akaidharau, hivi huyu mtu nimsalimie wa nini au awe rafiki yangu ili iweje? Yaani hata sielewi sijui naanzaanzaje.....

Khaa! Una roho ya kijasiri eh? Au ulikuwa haumpendi?
 
Nilikuwa nampenda lakini si sasa, upendo uliisha siku nyingi sana na ninamchukia, nilishamwambia asiwe ananipigia simu na kunisms lakini hakomi, natafuta dawa ya kumkomesha

Khaa! Una roho ya kijasiri eh? Au ulikuwa haumpendi?
 
Nilikuwa nampenda lakini si sasa, upendo uliisha siku nyingi sana na ninamchukia, nilishamwambia asiwe ananipigia simu na kunisms lakini hakomi, natafuta dawa ya kumkomesha

pole ram...hapo ungekuwa choka mbaya walaaa acngekusumbua kabisa, ndio kwanza angejicfia kwamba alikuwa kila ki2 kwako, sasa mambo poa kinamuuma! hawa viumbe hawa bac 2.
 
Reactions: ram
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…