Islam’s role in Tanzania’s freedom struggle


Nguruvi,
Usiniwekee maneno yako katika mdomo wangu.

Sijapatapo kusema ''matatizo ya uandishi'' katika mjadala wangu na wewe.
Ikiwa unacho kipande hicho kilete tukijadili.

Tuanze na Cecil Matola.

Ukitaka kujua ushawishi wa Cecil Matola katika siasa za Dar es Salaam ya 1920s
inakubidi kwanza ujue nani walikuwa wakitawala mji.

Kwa hakika si Cecil Matola na taarifa zake ni chache sana katika yale yaliyokuwa
yakitendeka Dar es Salaam.

Huyu Matola hakukaa sana katika uongozi wa AA kwa kuwa alikufa 1933.

Kleist alikuwa na ushawishi mkubwa katika mambo ya Dar es Salaam na ndiyo maana
katika vyama viwili vikubwa vya mjini yeye alikuwa kila siku akichaguliwa kuwa katibu
hata katika chama cha wafanyakazi wa reli alikokuwa akifanya kazi - Tanganyika
Railways.

Kleist alikuwa katiba muanzilishi wa AA (1929) na katibu muanzilishi wa Al Jamiatul Islamiyya
fi Tanganyika (1933). Vilevile katibu kamati ya kujenga shule ya Al Jamiatul Islamiyya Muslim
School.

Lakini kubwa ukimfananisha na wenzake wote Kleist alikuwa akifanya biashara na akatajirika
akiwa na umri mdogo sana...miaka 25.

Hela za Kleist zilisukuma sana harakati mbele na ndiyo kisa cha wanae kuja kutawala siasa za
Dar es Salaam baada ya kifo cha baba yao mwaka 1949.

Hilo wazo la kuanzisha AA alilitoa Dr Aggrey kwa Kleist mwaka 1924.

Taarifa hizi zipo katika mswada alioandika Kleist kabla hajafa na ukitaka zaidi soma maisha ya
Kleist katika Modern Tanzanians kitabu alichohariri John Iliffe na aloandika habari za Kleist ni mjukuu
wake Daisy Aisha Abdulwahid Sykes mwanafunzi wa Ilifee University of Dar Salaam 1968.

Bwana Nguruvi wewe hodari wa kutaja majina lakini tatizo lao kubwa huna taarifa za hao watu
unaowaleta hapa jamvini.

Mimi sijapata kukutana na jina la Ramadhani Ali na mara kadhaa nimekuomba utuwekee hapa
yale alofanya katika siasa za Dar es Salaam lakini hadi leo wewe umekazania kutaja jina lake
tu.

Angalia.
Mabingwa wa AA wanajulikana na taarifa zao wala si siri.

Kuna Erika Fiah ambae akichuana sana na Kleist katika kugombea uongozi wa AA.
Yupo Mzee bin Sudi.

Wapo Hassan Taufik Suleiman, Ali Juma Ponda, Edward Mwangosi na wengineo wengi.

Ramadhani Ali sijapata kumuona si katika majalada ya Sykes wala Tanzania National
Archives (TNA).

Lakini hili si kubwa huenda kanipita pembeni na itakuwa kheri kubwa kwa ukumbi huu
kupata taarifa mpya za mtu huyu.

Ila jua moja.
Hata bingwa wa historia ya Tanganyika John Iliffe hajamtaja Ramadhani Ali popote pale

Mwisho nikuulize Bwana Nguruvi.

Kwa wazee wangu kuondolewa katika historia ya uhuru kulisukumwa na udini hata
unisusulike mimi na udini kwa kuandika kitabu kilichosahihisha historia hiyo?

Mimi ''extremist'' na ndiyo maana napata mialiko...
Mdomo haumkatai bwana wake.

Napata mialiko kwa kuwa yale ninayoandika yana maana.

Tumalize na Nyerere.

Kama una taarifa za Nyerere kufanya makubwa katika siasa za Tanganyika kabla ya
kuja Dar es Salaam na kukutana na Abdulwahid Sykes hebu tupe.

Hiyo kudanadana na Nyerere na siasa za kufikirika haisaidii katika mjadala.

Nyerere ahkuna liyekuwa anamjua katika ulingo wa siasa hadi alipoletwa kwa Abdu na
Joseph Kasella Bantu.

Najua unakereka kusikia habari za baba yangu.
Baba yangu kafahamiana na Nyerere pale nyumbani kwa Abdu Sykes.

Na si yeye tu.

Watu wengi wa Dar es Salaam wamemjulia pale nyumbani kwa Abdu Mtaa wa Aggrey
na kwa Dossa Mtaa wa Mbaruku na wengine pale ofisini kwa Abdu Soko la Kariakoo.

Na katika watu waliomjua kwa karibu sana Nyerere pale Kariakoo Market ni Mzee Abdalla na
Shariff Abdallah Attas.

Kwa watu hawa nimepata mengi sana ya siasa za 1950 nyumbani kwa Abdu na hata pale ofisini
kwake Kariakoo Market.

Hii ndiyo historia ya wazee wangu na Nyerere na hii ndiyo historia ya mji wangu wa Dar es Salaam
nilozaliwa.

Hakuna wa kuja kunifundisha historia hii.
Mimi nimeishi ndani ya historia hii.
 
Kwanza naomba usiniwekee maneno mdomoni. Hakuna mahali ambapo nimesema wewe ni extremist. Soma sentensi yangu kwa uangalifu halafu ujiridhishe kuwa nimesema wewe ni extremist. Hii hulka ya spinning ndio ninayoiona kwa vijana wako wakisema nimekuita stupid bila ushahidi. Naomba haya niwaachie huko katika darsa zenu.

Pili, unaposema habari za Cecil Matola hazijulikani si kweli. Hazijulikani kwasababu hukutaka zijulikane. Kifo cha Cecil mwaka 1933 taa ikiwa na miaka 4 hakimfanyi matola asiwe katika historia. Yeye alikuwa rais wa kwanza wa AA hilo linnabaki kuwa ukweli na kulikana si kumtendea haki. Sykes na utajiri wake havimfanyi awe rais wa AA alikuwa katibu mkuu na huuo utabaki ukweli. Utajiri ulikuwa wake na familia yake bila kuondoa au kupunguza intellectual capacity ya mwalimu Cecil Matola.

Tatu, nakumbuka katika mijadala ya nyuma ilizungumziwa makamu wa rais wa AA. Hapa namwalika Mag3 kwasababu katika majibizano hukukanusha kuwepo kwa makamu wa rais tena mtu wa pwani (mndengereko? mzaramo?) kwahiyo subiri tutapata habari. Ima nimekosea jina hilo nalo pia tutalifahamu.

Nne, umewahi kusema kuwa katika maandishi yako huwezi kuandika kila kitu na kusema matatizo mengine yanayotokana na uandishi ni kwa muktadha huo. Nyuzi tulizowahi kujadiliana tangu mwaka 2010 ni nyingi na si rahisi kuvuta. Ninachokuhakikishia ni kuwa hilo limetokea.

Tano, napenda kukuhakikishia kuwa kitabu chako hakijasahihisha makosa ya historia. Kimezidi kujenga ufa mkubwa sana katika jamii kwa kutuondoa katika ukweli. Kitabu kimelenga kumshambulia mtu mmoja na hata kushindwa kuwataja wengine. Mfano, role ya Kyaruzi haiwezi kuwa ndogo kuliko ya Mshume. Watu wote waliokuwa na imani tofauti wameondolewa katika kitabu chako kwa makosa yale yale unayolalamikia.

Zaidi ya hapo unapoona nyuzi na habari za kuhusu waislam huku nukuu zako zikitumika ni ushahidi kuwa kitabu chako kipo katika mahadhi ya kidini.

Hakuna tatizo kuandika kuhusu kundi unalolilenga lakini basi fanya hivyo kwa kusema unaandika historia ya kundi hili ndani ya Tanganyika na si historia ya Tanganyika.
Hadi hapo hutakuwa na mamlaka ya kusema unasahihisha historia utakuwa na mamlaka ya kusema unaandika historia pungufu ukilenga kundi fulani, tutakuelewa.

 
Last edited by a moderator:

Nguruvi,
Kumbe una ''short memory.''
Rudi nyuma soma.

Na mimi nikalisema hilo ingawa sikuchukia.
 

Nguruvi,
Utapata sana shida na mimi.
 
Yani wewe jamaa IQ yako ilivyo ilivyondogo hata mdogo wangu wa mwsho form one maua seminary huwezi ku'argue nae.
Nguchiro kazi yake ni moja tu, kumbe humu tunaweza kuwa tunabishana na watoto wetu humu ukumbini.

Baba yako kumbe mtoto wake wa mwisho anasoma form one maua seminari teh teh teh!! Ndiyo maana hauna cha kuandika masikini zaidi ya kumpa moyo Nguruvi3 asikate tamaa.

Vizuri umetufahamisha kuhusu familia yenu, sawa endelea kutoa kichwa shimoni.
 
Mohamed Said ili kukudhihirishia kuwa historia yako imelenga kuwaondoa watu wengine na haikulenga kusahihisha historia soma kipande chakeo hapa chini
Umeeleza kuhusu K.Sykes bila kueleza hicho chama kilikuwa na katibu mkuu peke yake tu. Ulifahamu kuwa Cecil Matola alikuwepo lakini jitihada zako za kuficha ukweli zikatamalaki kwasababu rahisi ya imani. Hakuna shida ukisema hilo shida ni pale unapotaka ulimwengu uamini historia yako ni ya Tanganyika kumbe ni ya kundi ndani ya Tanganyika tean kukiwa na misleading za kutosha tu.

Ukisoma hiyo utagundua kuwa baada ya miaka mingi ya kusema Sykes ndiye mwanzilishi hatimaye safari hii umeenda Nairobi ukiwa sober ''founded in 1929 by Kleist Sykes as founding secretar
y''
Wale mnaodhani sisi ni 'wendawazimu' oneni nguvu ya hoja inavyoweza kuisadia jamii. Leo jamii inafahamu huyu ni mmoja wa waanzilishi akiwa katibu si mwanzilishi kama ilivyokuwa imefinyangwa siku za nyuma.
 

Nguruvi3.

Angalia paragraph yako ya mwisho neno "STUPID"
 
Last edited by a moderator:
THE BIG SHOW na wengine kwa nyakati tofauti wamehoji kuwa madai yangu ya majina ya barabara kwa waislam ninayapata wapi. Hii ni paper mbichi kabisa kutoka Nairobi (Mohamed Said) akilalama kuhusu kutajwa kwa mitaa. Tafadhalini pateni 'darsa'
 
Last edited by a moderator:
Usitake kupotosha hiyo quote uliyokuja nayo inaeleza habari zingine kabisa wala haipo kwenye kitabu cha Mohamed Said.

Kumbe haujasoma kitabu umeamua kubisha tu.

Kitabu cha Mohamed Said. Kimemtaja Cecil Matola, Rawson Watts, Ibrahim Hamis, Zibe Kidasi. Ali Said Mpima, Kleist, hawa ndiyo waasisi wa TAA.
 
Last edited by a moderator:
THE BIG SHOW na wengine kwa nyakati tofauti wamehoji kuwa madai yangu ya majina ya barabara kwa waislam ninayapata wapi. Hii ni paper mbichi kabisa kutoka Nairobi (Mohamed Said) akilalama kuhusu kutajwa kwa mitaa. Tafadhalini pateni 'darsa'
Haya ndiyo madai ya Waislam wa Tanzania kama ulivyokuwa unavyoeleza?
 
Last edited by a moderator:
Huwezi kujadili nyuzi nzima kuhusu stupid and trivial thing halafu uka depict positive image ya society.

Hiyo sentensi ikisomeka kuanzia hitimisho pale juu halafu zikafuatwa nukta kwa kila sentensi ni kituko kusema ilimtukana Mohamed Said.

neno 'nyuzi nzima' linasema kila kitu. Nyuzi ipi.
halafu kuna maneno depict positive image ya society nayo pia inaonyesha kuwa kilichiokuwa kinaongelea ni nyuzi na society ni katika sehemu ya maongezi ya nyuzi na si mtu.

Yale yanayomhusu Mohamed Said yapo clear.
Nakushukuru sana umeileta hii, kila mtu atasoma na kuelewa iwe kwa mantiki au spinning.

Mwisho wa kuliongelea hili suala, mna hiari ya kuendelea ku-promote hiyo kauli kwa gharama zenu.

Kwa hii sentensi sina hatia asilani. Inajieleza yenyewe.
Kama hamna hoja kunjeni jamvi, mimi kwa upande wangu sikunji.

Teh teh teh !
 
Unajua quote imetoka wapi?
Nimemsoma Mohamed kuanzia siku ya kitabu cha kwanza, nikamsoma katika magazeti mingi mingi FYI.

Hiyo quote inatoka katika paper ya juzi Nairobi. Kumbe hata ile paper mliokuwa mnarushiana matusi hujaisoma!
Kasome vizuri halafu urudi tujadili. Hujasoma paper
!
 
Haya ndiyo madai ya Waislam wa Tanzania kama ulivyokuwa unavyoeleza?
Nimeshajibu hoja kwasababu swali liliuliza wapi nimepata hoja ya majina ya barabara. Nikawa muungwana na kushari majina zaidi.
Kama ushauri wangu si mzuri basi uacheni. Ushahidi wa kuwa moja ya malalamiko ya kuwaenzi wazee ni majina huo hapo. Ni kutoka paper ya Mohamed Said ya Nairobi. Paper mbichi kabisa na bado moto kutoka jikoni, Mzee analalama kuhusu barabara! Hili nimeshalijibu kwa ufasaha nimefunga.
 
Teh teh teh! "STUPID" ni nini?
 
Wewe ndiyo rudi kajisome upya umendika baada ya miaka mingi Kleist kuandikwa muasisi wa AA, mie nimekujibu mbona kwenye kitabu chake toka 1997 Cecil Matola kaandikwa kama mmoja wa waasisi wa AA. Hiyo miaka mingi ni ipi unayoisema?
 
Teh teh teh! "STUPID" ni nini?

Al shariff Ritz waswahili wansema "ukitaka kuwa muongo basi usisahau neno"
Huyu kijana Nguruvi3 akitoa kashfa na matusi, kwake yeye ni kama kunywa togwa! Akirudishiwa bakora za makalio, anapayuka kama kaona jinni!
Teh teh teh teh!
Tunasubiri hoja zake! Manake kaishaanza kutoa hitimisho alfajiri.!!
 
Last edited by a moderator:
Dr. kahtaan.

Nimecheka sasa eti anatuambia tukunje jamvi hatuna hoja wakati yeye mwenye alisema atamwga mtama.

"STUPID" kwako siyo tusi teh teh teh teh! analalamika eti tunafanya spinning tumemletea neno aliloandika hataki kujibu ngoja nimuulize tena.

Nguruvi3. "STUPID" ni nini au ulilitumia kama salamu, halafu anasema tunamchafua teh teh teh!
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…