Islam’s role in Tanzania’s freedom struggle

Hivi wewe Wickama nimekufuatilia post zako zote Unajifanya muungwana kumbe wapi wewe ni Sawa na panya unang'ata na kupuliza!

Boko Aslaam aleykum,

Za siku nyingi ndugu yangu? Mimi na mzee MS tulikuwa tunarushiana mitego kupitia sigara za Julius. Lakini kama unavyoona huyu bwana mwenyewe kasema huwa anasoma between the LINES. Kagundua issue ya sigara ni kama bait (hahahaha). Sasa pamebaki kitu tena?

Boko suala sio kuuma na kupuliza. Suala ni kuwa siamini kuwa tuko kwenye forum hii ili kumfedhehesha mtu au watu. Bottomline tunatarajia tufurahie ule ushindani na Inshallah siku nakutana na wewe kwamba ndiye Boko basi tucheke na kunywa soda/kahawa sio kujuta.

Honestly, huwa na-admire sana Mzee MS anavyo-respond to challenges hata anapokwepa kama hii ya cigarettes. I normally laugh aloud and enjoy. Why not?. Haina maana sitofautiani naye. No.

Boko, nimekusikia na usisite kunirushia ujumbe au pronto correction kama napotoka. Mimi sio malaika.

Shukran sana.
 

Ni jambo jema kuwa na Sheikh Mohamed Said hapa jamvini

Tumia vema hii fursa japo kiduchu, walau kwa kudadisi na kujifunza jambo toka kwa Bi.Mluguru

Kama vile kwanini wanae Abdul, Ali na Nyerere walikua hawasemezani kwa heri tena ni baada ya uhuru?

Kaa kitako upate kufahamu husoyajua wewe Wickama
 
Last edited by a moderator:

Unajitahidi sana kukwepa uhalisia wako na tabia yako ambayo kuificha hata huwezi. Kumbuka mtu hawezi kuwa na PARANOIA dhidi ya mwingine hivihivi unless umeshawahi kumfanyia kitendo cha kupelekea kukuchukulia hivyo. Ninakusoma sana nguruvi3 katika maandishi yako mengi ambayo unachangia humu jamvini may be ndio kilichonifanya kuwa na Paranoia dhidi yako kwani mawazo yako huwa yamejaa kejeli na dhihaka kwa waislamu na hata maeneo watokayo.
Ok let it go kwani hata utudhihaki na kutukejeli still hauwezi kuzuia mvua ya mabadiliko. Tutaendelea kupaza sauti na kuusema ukweli uliofukiwa miaka mingi kwa makusudi.
 

Wakti ukifika nitafurahi kusikia kisa kingine cha Bibi yetu. Tuseme Inshallah!
 
Wickama,
Haya yote ya baiskeli nk. nk. unataka nikujibu mimi?

Kwa nini nikujibu mimi?
Mie ni chanzo cha taarifa hizo au lipo jingine?

Mzee MS. Nimekuuliza wewe kwa vile huna roho ya mtutu. Basi tuendelee na mengine.
 
Dr. kahtaan

Huu Ulimbo Mubashar!! Nausoma huku nakunywa tende shake...teh teh teh!
 
Last edited by a moderator:
dr kahtaan
Namfahamu sana siku nyingi huyu kaka. Tatizo moja huwa ni mnafiki sana anajifanza kuufahamu uislamu hasa anapoona mambo yanamwia magumu utasikia akihoji uislamu haufundishi hivyo. Hata hapo kaja na kile alichookita ati ni MTAMA na kuwatoa wazee katika uislamu wao kisa walifanya matambiko. Nani kamuambia muislamu akifanya kosa hata la ukafiri anakuwa kafir? Huyu ni mtu wa ajabu sana kwani anasura mbili katika maandishi yake. Ok twende nae hivyo atleast watu tunapata kuufahamu ukweli kupitia kujikongogonga kwake.
 
Last edited by a moderator:

Dr. kahtaan,

Naona unamtia majiti huyo sokwe tehe tehe tehe!

Tena yale ya rohoni!
 
Last edited by a moderator:
Mujitahid CHAMVIGA.

Kumbe umeishamsoma huyu jama siku zote namwambia wapambane na CCM siyo kupambana na Waislam watashindwa vibaya na kudhalilika.

Toka karne ya saba watu wanaukejeli na kuufanyia dhiaka, matusi, lakini leo hii karne ya 21 Waislam wapo bilioni 2.04 duniani sasa wewe ukileta kejeli si unajisumbua bure.

Lakini hawa wametajwa kwenye Qur'an wala hawatupi shida.
 
Last edited by a moderator:

Kuna mengi sana ya kuzungumza dhidi yake mwalimu Nyerere katika makosa yake. Sijaona ubaya kwa mtu uliyemsaidia sehemu ya kulala hata na chakula akaja kukusaliti na kusababisha mauaji yako kuzungumza mema uliyomtendea na asiyajali. Na kama watu wataliona hili la kusema kili ulichokisema kumsaidia mtu ati unamsimanga akashindwa kulaumu kukusababishia uhai wako bila shaka huo ni ukosaji wa fadhila. Nawaashangaa sana kuona Mohamed Said kutaja fadhila nyerere alizozisaliti ni Frustration huku mkiacha kuzungumzia makosa yake. Be fair a little bit my brothers.
 
Last edited by a moderator:

Sheikh Tayeb,

Nilinunua kitabu cha mzee MS hapa Tanga many years ago. La maana ni kuwa anayoyasimulia humu JF tulimshauri yawe na ushahidi usio shaka, ambalo sio jambo gumu kwake. MS kanufaika sana na critical outlooks za baadhi yetu ku-shape matoleo yajayo ya kazi zake. Wala sidhani kama sifa kavukavu za wapenzi (za komaa mzee wetu....) zimemsaidia kumjulisha kipi cha kuboresha au kusahihisha kwenye kazi zake.

Tayeb, nakushukuru kwa ushauri wako. Ahsante.
 
Last edited by a moderator:
"Man Sharaaf naf'sahu, fahuwa rasul." ~ Mufti Barubaru.
 
Last edited by a moderator:
Nashukuru kwa ufafanuzi wako ila waliosahaurika ni waislamu pekee Yao? Na Kama sio kwann kusiwe na Uzi mmoja tu? Japokuwa umejaribu kutoa ufafanuzi lakini inaonyesha watu wengi wapo kishabiki/Imani zaidi Kama huyo mheshimiwa anavyodai unanitia majiti!
 
Sokwe,
Waliosahaulika ni Waislam wengi sana na Wakristo wachache.

lakini kwa kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika ilitawaliwa na
Waislam kusahauliwa huko kumewatoa Waislam katika historia
nzima.
 

Chamviga,
Ili mtu aone simulizi ni masimango au vinginevyo ni lazima achambue namna
jambo lenyewe lilivyohadithiwa.

Ikiwa ni lazima naweza nikaweka tena suala la ukarimu wa Abdu Sykes, Dossa
Aziz, Mzee Mshume si kwa Nyerere peke yake bali hata kwa watu wengine
katika TAA na TANU.
 
Wakti ukifika nitafurahi kusikia kisa kingine cha Bibi yetu. Tuseme Inshallah!

Tayeb,
In Sha Allah.

Nitakueleza jinsi mimi na rafiki yangu Ebby Sykes (mtoto wa Abdulwahid Sykes)
tulivyokuwa tukipewa hela na Bi. Mluguru ya kwenda kununua kaukau hoteli na jinsi
tulivyokuwa tukilinywa togwa la Bi. Mluguru biti Mussa.
 

Chamviga; Mchango wako ni mzuri. Awali (Threads ya Yericko...) tulifikia mahali na mzee MS tukakubaliana kila mtu kuwa na msimamo wake katika hili unaloita kusimanga. Binafsi, sina mashaka kabisa ni kusengenya kama utafuata katika sahih hadiths. Na kosa halifanywi ili kusahihisha kosa. Kusita kwangu na analysis yako ni kwa vile sina mahali naposoma ambapo nakuta mwandishi alishawahi kumfanyia fadhila Julius, kisha Julius akamgeuka. Pili, basi tuwekewe angalu wosia au rai ya hao watoa vyakula,malazi,baiskeli wakimpa mwandishi mamlaka ya kuwafichua wao na majina yao na fadhila zao kwa mgeni wao wakati kumbe hatuoni wahusika katika uhai wao wakilalamika kuhusu gharama zao juu ya mgeni huyu.
 
Last edited by a moderator:
Hivi babu yangu aliyepigana vita ya maji maji Mbona sijaona jina lake likitambuliwa Kwenye historia ya nchi hii au Hata inayosimuliwa na MS, au kwa vile babu yangu hakusoma,...? Hata yeye alimbeba Nyerere kwa baiskeli akiieneza TANU,,, Mbona yeye hamumtaji.? Au kwa vile Hana jina la shehe au la ubatizo....?.... Hebu acheni ulalamishi wa kijinga, hivi kila mtanganyika akielezea historia ya ukoo wake ulivyopigania uhuru lakini hawajakumbukwa patatosha kweli hapa,... Kuweni na akili kidogo basi Hata za kuazima zinaruhusiwa ikiwa zako hazitoshi.
 

Wanasema ukitaka kumficha mswahili jambo weka katika maandishi!

Unaweza ukasoma kitabu chake lakini husifahamu maana!

Na ndio maana anaendelea kutusimulia simulizi nyengine ambazo mimi na wewe hatujapata kuzifahamu hapo kabla!

Au wewe hutaki kupata faida kwanini Abdu, Ali na Nyerere walikua hawasemezani kwa heri tena baada ya kupatikana kwa uhuru?

Hapo hapahitaji hayo makhanatha yako ya "koma mzee"
 
Tayeb,
In Sha Allah.

Nitakueleza jinsi mimi na rafiki yangu Ebby Sykes (mtoto wa Abdulwahid Sykes)
tulivyokuwa tukipewa hela na Bi. Mluguru ya kwenda kununua kaukau hoteli na jinsi
tulivyokuwa tukilinywa togwa la Bi. Mluguru biti Mussa.

Inshallah!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…