Asante
FaizaFoxy, mimi siye mwana historia na si mwandishi by profession na muda kusema kweli ni tatizo kubwa kwangu...hata hivyo kabla sijajibu swali lako ningependa ufahamu kuwa wengi wa vijana wasomi wa mwanzoni mwa miaka ya 1920 kuendelea walikuwa ni wahitimu wa shule maarufu iliyoitwa
Kiungani kisiwani Zanzibar. Mwaka
1866 dhehebu la Kikristo,
UMCA, lilinunua sehemu ya ardhi nje kidogo ya mji wa Zanzibar na kujenga hosteli kubwa katika juhudi zao za kuwapa hifadhi wahanga wa Utumwa. Baada ya miaka saba,
1873 walijenga Kanisa lao la kwanza mjini Zanzibar lililojulikana kama
Christ Church Cathedral na kufungua kituo cha afya mwaka
1877 ambacho kiliweza kuwa hospitali kamili mwaka
1893.
UMCA ilianzisha shule Kiungani iliyojulikana kama
St. Andrew's College, U.M.C.A. lakini baadaye kwa sababu mbalimbali ilibidi wahamie bara kama inavyosimuliwa hapa;
Kwa nini nasimulia haya? Ni kwa sababu ukitaka kuwajua watu ambao ungeweza kuwaita "elite" wa mji wa Dar es Salaam kwa nyakati hizo, wasomi wa wakati huo wanachukua daraja la kwanza.
Cecil Matola alikuwa ni moja wa alumni wa Kiungani na Mwalimu Mwandamizi katika shule ya serikali mjini Dar es Salaam. Wahitimu wa Kiungani walijulikana ndani na nje ya nchi na kulingana na simulizi za
John Iliffe ambayo
Mohamed Said anazinukuu kila mara, nanukuu;
Cecil Matola was a senior African Teacher at the Dar es Salaam School which made him almost an ex officio leader of the capital's educated Africans. Nyakati hizo Ualimu ulikuwa ni profession yenye heshima kubwa katika jamii na haikuwa ajabu kwa mtu maarufu kama
Cecil Matola kuchaguliwa kuwa
Raisi wa kwanza African Association mwaka
1929.
African Association ilianzishwa kwa baraka za aliyekuwa Gavana wa Tanganyika
David Cameron na mkutano wake wa kwanza ulifanyika nyumbani kwa Raisi wake muasisi
Cecil Matola. Hii ilifanyika kwa sababu tatu; kwanza hapakuwepo na klabu ama nyumba iliyotosheleza kama ya Cecil Matola, pili hakuwepo mtu aliyeheshimika kama yeye na tatu
Cecil Matola alikuwa
Mtanganyika halisi, Myao. Mpaka anakuwa Raisi wa AA, alishafanya kazi sehemu mbali mbali ndani na nje ya Tanganyika na kukutana na wasomi mbalimbali wenye mawazo mapya. Sababu kuu ya
Mohamed Said kutotaka kujua historia ya
Cecil Matola ni kwamba inawaweka wazee wake mamluki wa Kimanyema, Kizulu na Kinubi pakavu. Watu mamluki waliopigana vita dhidi ya Watanganyika wakiwa upande wa Mkoloni eti ndio waongoze harakati dhidi ya mkoloni, wapi na wapi!
Chama cha kwanza kabisa cha wasomi na kilichowakutanisha Waafrika, wafanyakazi na wafanya biashara, kilianzishwa mjini Tanga na Mtanganyika wa kwanza mhitimu wa Kiungani Zanzibar aliyekuwa na cheo cha juu kabisa serikalini mwaka 1922,
Martin Kayamba. Kwa bahati mbaya sana
Mohamed Said katika kuhangaikia namna ya kuwakweza wazee wake ambao hawakuwa na uwezo wala sifa za kiuongozi amejikita sana katika kuwachafua wengine. Ikumbukwe maraisi wa
AA, TAA na baadaye
TANU walikuwa ndio wenyeviti na watendaji wakuu wa hivyo vyama lakini kwa
Mohamed Said, maraisi hawa hawakuwa chochote na sifa zote anawapa eti makatibu.
Cecil Matola alikuwa ni
Raisi muasisi na Mtendaji Mkuu wa AA hadi anafariki katika mazingira yasiyoeleweka wakati huo tayari
AA wana nyumba ambayo kiwanja chake walipewa na
Gavana David Cameron mtaa wa
New Street.
Kusema kweli kukosekana kwetu wengine kwenye huu mjadala kunatokana na kukosa muda lakini nina hakika tupo wengi wenye historia inayopingana na hizi hadithi za mtaani za
Mohamed Said...a fellow so obsessed with hatred, so bent on distorting facts and so bent on sowing seeds of discord he will stop at nothing till he accomplishes his evil plans but thank God, that chance he wont get,
not on our watch...we wont allow him or his stooges/cronies.
Mohamed Said hawezi hata kusema ni lini
Mzee Kleist Sykes aliuacha
Ukristo na kuingia
Uislaam, hawezi kusema lini
Chief Kidaha Makwaia aliuacha
Uislaam na kuingia
Ukatoliki na hawezi kuacha kuonesha chuki yake kwa msomi
Martin Kayamba mjukuu wa
Chifu Kimweri Zanyumbai Mfalme wa
Wakilindi waliowatawala Wasambaa na makabila mengi ya Tanga hata kabla ya Wajerumani.
Kwa leo yatosha
FaizaFoxy, ni muda tu unakosekana...
Mag3,
Ukiwa unataka kumpambanisha
Cecil Matola na babu zangu haitakuwa haki.
Cecil Matola hakujaaliwa umri mrefu alikufa mwaka 1933 kwa hiyo hakufanya
mengi ukilinganisha na babu zangu.
Lakini mbona umemtaja Matola peke yake.
Vipi kuhusu
Mdachi Shariff na
Nichodemus Ubwe?
Lipo bandiko hapa JF katika kirago hiki hiki kuhusu
Kleist Sykes kama nilivyoandika
katika mradi wa Oxford na Harvard.
Angalia mchango wa
Kleist ambao ulikuja kuchukuliwa na wanae pale yeye alipokufa
mwaka 1949.
Kleist wanae wawili ni waasisi wa TANU.
Unataka nikupe habari za
Martin Kayamba?
Kwenye kitabu, ''Modern Tanzanians,'' Iliffe katika kuwajulisha wasomaji wake
Martin
Kayamba ni nani kamueleza kwa njia ya mfano tena katika ufunguzi kama kibaraka wa
Waingereza.
Sasa soma hapo chini usikie wenzake walikuwa wanamuonaje.
Katika kitabu changu hivi ndivyo nilivyomuandika
Martin Kayamba:
''In a cruel and cynical obituary on the death of
Martin Kayamba,
[1] Fiah lamented
that Africans did not benefit from
Kayamba's education nor from his post as a clerk to
Assistant Chief Secretary.''
[2]
Yapo mengi ningependa uyajue kuhusu
Martin Kayamba.
Endela kunisoma hapa nilivyoweleza
Martin Kayamba katika kitabu changu:
''There was a very big difference between the Tanganyika Territory Civil Servants' Association
(TTACA), founded in 1922 by
Martin Kayamba, and the Dockworkers' Union, both in leadership
and in direction.
TTACA was a harmless genuine welfare association, free from any conflict with the colonial
administration.
It was ‘a club for clerks and teachers, with newspapers and a football team, encouraged by
the government.''
[1]
Bado sijamalizana na wewe
Bwana Mag3.
Ukitaka kustarehe na
Martin Kayamba soma kitabu chake, ''The Autobiography of Martin Kayamba,
''The Story of
Martin Kayamba Mdumi, MBE, of the Bondei Tribe,'' katika Margery Perham, (ed)
Ten Africans, pp.175-272 uone jinsi babu yako anavyolamba viatu vya Waingereza.
Ukishasoma kitabu hiki rudi hapa jamvini nakusubiri.
Martin Kayamba mjukuu wa
Chief Kimweri.
Kimweri alikuwa Muislam.
Ludwig Krapf alipofika kwa
Chief Kimweri 1848 kamkuta Kimweri kastaarabika kavaa kanzu na kilemba yuko
katika mahakama yake anahukumu anajua kusoma na kuandika Kiarabu.
Hakuwa peke yake akijua kuandika.
Wanae na Waislam wengine Vuga na katika utawala wake wote walikuwa wameelimika.
Hasad ilimsonga roho
Krapf.
Alikuja kwenye ''dark continent'' kakuta mengine kabisa.
Uislam umeenea na watu wanajua kusoma na kuandika msingi wa kujifunza kusoma ni madras.
Wakoloni walipoichukua Tanganyika kitu cha kwanza ilikuwa kupiga marufuku hati za Kiarabu.
Kingine kilichofuata ni kuwaritadisha akina
Martin Kayamba.
Kayamba akawa Mzungu hata kumshinda Mwingereza mwenyewe.
Mwisho napenda kukufahamisha kuwa
Kleist Abdallah Sykes alizaliwa Muislam na kazikwa Kisutu Makaburi
ya Waislam.
Nitakuongezea kuhusu
Chief Kidaha.
Aliyeritadi kuingia Ukristo si yeye peke yake.
Mdogo wake
Hussein vilevile aliritadi.
Na hawa wote mimi nimeowaona.
Hussein alikuwa rafiki wa mmoja wa baba zangu.
Chief Kidaha aliritadi mwaka 1945.
Ukitaka kisa hiki sema nitakiweka hapa jamvini.
Nakunja jamvi kwa bashraf hii hapo chini.
Kama mwenye chuki na
Martin Kayamba si mimi bali ni John Iliffe aliyemwita Kibaraka.
Mwenye chuki ni
Erika Fiah aliyemwita kibaraka wa Waingereza tena kwenye taazia na kusema kuwa
kazi kubwa aliyoimudu
Martin Kayamba ni kufuga kuku Muheza baada ya kustaafu kazi.
[1] Iliffe, ‘Tanzania Under British Rule' in B.A. Ogot and J. Kieran (Eds)
Zamani:
A Survey of East African History, East African Publishing House, 1968 p. 22 quoted in
African Studies Working Paper No. 8, April, 1979, by G.W. Reeves.
[1] See Iliffe, ‘The Spokesman: Martin Kayamba' in Iliffe (Ed),
Modern Tanzanians,
op. cit. pp. 66-94.
[2]
Kwetu, 29 June, 1940.