Isuzu Bighorn vs Suzuki Grand Escudo?

Isuzu Bighorn vs Suzuki Grand Escudo?

clasi

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2013
Posts
379
Reaction score
716
Wakuu nataka kuagiza Gari SUV Japan. Katika kuperuzi nimeangukia katika Gari hizo 2 naombeni ushauri wenu Isuzu Bighorn (Diesel 3000cc) vs SUZUKI GRAND ESCUDO (Petrol 2730cc). Nichukue ipi? Ukizingatia barabara off-road na spea Tanzania. Mafuta usihofu nayamudu

BK166329_dec745.jpeg


BK166329_1e897a.jpeg


BH791906_c21ea0.jpg


BH791906_29594f.jpg
 
Kama utaipenda Isuzu Bighorn chukua ya diesel yenye injini ya 4JX1 iwe manual. Nyingi zilizosumbua ni zenye injini ya 4JG2 mafundi na watumiaji walishindwa kuendana nazo.
Basi wabongo hatujui magari hz details unazipatia wapi? Maana hao wavimba macho huko Japan unadhani wajinga wakuwekee details za kukupa wasiwasi usinunue Gari?
 
Basi wabongo hatujui magari hz details unazipatia wapi? Maana hao wavimba macho huko Japan unadhani wajinga wakuwekee details za kukupa wasiwasi usinunue Gari?
Kweli mkuu kila gari watumiaji huwa na platforms ambazo hujadili ubora na mapungufu.

Isuzu Bighorn zenye injini ya 4JG2 hii injini ilitoka haina nguvu na ilikuwa na teknolojia ya kizamani Sana ya indirect injection, mechanical pumps. Hizi gari waliopata nazo tabu ni Wakinga wa Iringa, Njombe, Mbeya,Tunduma walizinunua kwa Fujo kabla ya kuhamia kwenye Toyota Surf na Prado.

Hii injini inatumia heater, na ikiua heater kasheshe kuwasha na inakuwa na uchomaji mbovu wa mafuta.

Kwenye 2nd generation wameweka injini ya 4JX1 hii ni ya kisasa ni direct injection,pampu ya umeme na zina nguvu Sana na fuel consumption nzuri.
 
Ukitaka kulia machozi yasiyokwisha agiza hiyo Isuzu Bighorn.

Ni gari comfortable, fuel consumption nzuri,four-wheel gear ya uhakika unapita popote.

Tatizo kubwa ni injini na mfumo wa umeme, gari hii ilinifanya mimi mwenyewe niwe fundi, mzigo ukiwa mikoa ya barid hata Dar, ikishapoa tuu kuiwasha mtiti yaani mpaka ujufunze kuchoma heater direct (nishaungua sanaaa mikono).

Spea zake ni ghaliii sana,turbo lake bovuuu na haina mwendo hyo ni mdogo mdogo mzee.

Niliinunua mwaka 2011 ikanitesa sanaaa,haiuziki nimeitelekeza mkoani mbeya mpaka leo hii halina mteja.

Narudia tena ni bovu bovu bovu sanaaaa,mimi ni mtunzaji sana wa magari lakini hapo nilikwama.

Ukija kwenye grand vitara,nayo ni nzuri ila tatizo lake kubwa ni kula oil ndio maana wengi wanakaanga injini zake deile,nilipata kuinunua mwaka 2015 ikanifia mwaka huo huo,niliweka oil ya BP kwenye service lakini ngoma ilienda arusha ile kurudi nishakaanga wakati nilipima oil nikaona ipo vizuri,hii nayo vipuri vyake ni ghari sana,nikafanya overhaul ya injin nikaiuza.

Nikaamua kuhamia Toyota ambako sikudumu sana nikahamia magari ya ulaya ndio nimepata pumziko la moyo
 
Ukitaka kulia machozi yasiyokwisha agiza hiyo Isuzu Bighorn.

Ni gari comfortable, fuel consumption nzuri,four-wheel gear ya uhakika unapita popote...
Duuh. Kama nimekuelewa vizuri ni kwamba tujumuike huko kwa Mabeberu (Ulaya) Sasa SUV means ninunue BMW au Land Rover? Labda mpaka nijipange upya chief
 
Back
Top Bottom