Itachukua muda mrefu sana kupata jiwe hili wajenzi walilolikataa

Itachukua muda mrefu sana kupata jiwe hili wajenzi walilolikataa

Kibosho1

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2017
Posts
2,621
Reaction score
4,293
Hakuna kitu kinauma kama majuto,majuto yanauma zaidi sababu yanakuja baada ya muda kupita. Hakuna aliewahi kurudisha nyuma muda akafanikiwa. Nyakati za Yesu alipingwa sana japo alisaidia wengi, aliponya wengi lakini bado alionekana si kitu. Baada ya kufa ndio walijua kuwa hakika alikua mwana wa Mungu.

Toka nipate akili sikuwahi kuona kiongozi mwenye uthubutu kama Magufuli, hakuwa muoga, alikua mkali na aliogopeka na kila mtu. Mwaka 2015 kabla ya ufunguzi maoni ya Watanzania wengi walitaka kiongozi mkali, ili asimamie vizuri mali zao na aache kucheka na wezi.

Magufuli alijitahidi sana kutimiza hilo, serikalini kulikuwa na nidhamu ya kweli, mnyonge alipata furaha lakini kama ujuavyo katika dunia hii hutaweza kumridhisha kila mwanadamu. Magufuli hakuwa malaika asiwe na kasoro, pamoja na kasoro yake alimizia mengi kuliko matarajio ya wengi.

Harakati za kumpiga vita mitandao ni kubwa sana kuliko mitaani, hali ya kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja sio powa sana lakini ameimarisha miundombinu. Online Tanzania hatakiwi wakati Wakenya waliomba awe rais wao.

JK akitukanwa sana lakini alikumbukwa baada ya muda mfupi. Magufuli ni jiwe walilolikataa waashi lakini litakuwa jiwe kuu la pembeni muda si mrefu.

Miradi kama SGR, mwendo kasi Mbagala, kujenga mji mkuu Dodoma n.k vinaweza kusimama au kuchukua muda mrefu kama kiongozi anaeingia hatavaa viatu vyake vizuri. Binafsi naamini Magufuli atakumbukwa zaidi ya marais wote Tanzania.
 
Kuna mawe yaliyokataliwa na system na hata baadhi yao kuuawa au kunusurika kifo baada ya marisasi kibao.

Mawe mengine yalikataliwa kwa kufilisiwa ila Magu ndilo jiwe walilolikubali waashi.

Jifunze kuelewa mantiki ya context hasa unapoikopa kutoka maandiko matakatifu
 
Hakuna mtawala anayeweza kupendwa na watu wote, hata aje nani!

Uliyoyaandika hapa hata kwa akina Maalim Seif, Mandela, Nyerere tuliowaanzishia michakato ya uana kheri yanawahusu?

Huyu bwana chini yake wamekufa wengi kwa Corona. Achilia mbali kina Ben na kina Azory.

Huo ndiyo ulio ukweli mchungu.

Tulipo ashukuriwe mola mwanzo mpya barakoa na social distancing ziwe kipaumbele.
 
Uliyoyaandika hapa hata kwa akina Maalim Seif, Mandela, Nyerere tuliowaanzishia muchakato ya uana kheri yanawahusu?....
kwa hyo wewe umeona ben na azory ujaona aliyoyatenda huyu kiongoz acheni unafk aiseeee
 
Uliyoyaandika hapa hata kwa akina Maalim Seif, Mandela, Nyerere tuliowaanzishia muchakato ya uana kheri yanawahusu?..
Hiyo ni kasoro yake, hamuez lingana kwa mapungufu
 
Hakuna kitu kinauma kama majuto,majuto yanauma zaidi sababu yanakuja baada ya muda kupita. Hakuna aliewahi kurudisha nyuma muda akafanikiwa. Nyakati za Yesu alipingwa sana japo alisaidia wengi, aliponya wengi lakini bado alionekana si kitu. Baada ya kufa ndio walijua kuwa hakika alikua mwana wa Mungu...
Kwanini Mkoloni aliondolewa

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna kitu kinauma kama majuto,majuto yanauma zaidi sababu yanakuja baada ya muda kupita. Hakuna aliewahi kurudisha nyuma muda akafanikiwa. Nyakati za Yesu alipingwa sana japo alisaidia wengi, aliponya wengi lakini bado alionekana si kitu. Baada ya kufa ndio walijua kuwa hakika alikua mwana wa Mungu...
Wajenzi wamekataa....unaonaje kama jiwe hili limekataliwa na wenye nyumba
 
Back
Top Bottom