Morogoro kaskazini
JF-Expert Member
- Jul 5, 2020
- 2,392
- 9,187
Unatoa pesa kwenda kuangalia wanyama walioletwa na mungu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kumbe siyo garama sanaNItafafanua gharama za kuingia hifadhini kuanzia saa 12 asubuhi Hadi saa 12 Jioni (yaaani day trip) pamoja na Aina za usafiri na gharama zake kama ifuatavyo.
1. Kwa kutumia gari Aina ya LAND CRUISER inayofunguka juu (OPEN ROOF) na inayobeba Hadi WATU WANNE(four passenger seats) gharama ni shilingi 560,000/=. Gharama hizi zinahusisha kukodi gari, mafuta, Kodi ya gari inapoingia hifadhini, chakula Cha asubuhi na mchana, kiingilio Cha watu 4.
Mkiwa kikundi Cha watu 4 hapa Kila mmoja atalipia angalau 140,000/=.
2. Kwa kutumia gari Aina ya LAND CRUISER inayofunguka juu (OPEN ROOF) na inayobeba Hadi WATU SITA (six passenger seats) gharama ni shilingi 700,000/=. Jumla ya watu hapa mtakua 6, endapo mtakua pungufu gharama zitapungua kidogo kwenye chakula na kiingilio hifadhini. Kwa kawaida kiingilio ni shilingi elfu kumi na mbili (12,000/=) Kwa mtu mzima kuanzia miaka 16. Watoto chini ya miaka 5 ni bure. Wastani gharama ya chakula Kwa mtu mmoja ni shilingi elfu kumi (10,000/=) Kwa breakfast na lunch.
Mkiwa kikundi Cha watu 6 hapa Kila mmoja atalipia angalau 120,000/=.
3. Kwa kutumia gari Aina ya HIACE inayobeba Hadi WATU 7 HADI 12 gharama ni shilingi 750,000/=. Hapa mnaweza kuwa kikundi Cha Hadi watu 12, endapo mkiwa pungufu gharama zinaweza kupungua kidogo kama nilivyoelezea hapo juu.
Mkiwa kikundi Cha watu 12, hapa Kila mmoja atalipia angalau 65,000/=.
4. Kwa kutumia gari Aina ya COASTER AU TATA inayobeba wastani wa WATU 13 HADI 30 gharama itakuwa ni shilingi 1,500,000/= (milioni Moja na nusu). Mkiwa pungufu ya idadi hiyo gharama itapunguza kidogo pia.
Mkiwa kikundi cha watu 30 hapa Kila mmoja atalipia angalau 50,000/=.
5. Kwa kutumia gari Aina ya NOAH inayoweza kubeba WATU 2 HADI 6 gharama itakuwa shilingi 450,000/= (laki nne na nusu).
Mkiwa kikundi Cha watu 6 hapa Kila mmoja atalipia angalau 75,000/=.
Kumbuka Gharama hizo ni Kwa jumla na zinabadirikabadirika kutokana na Aina ya gari utakayopenda kutumia. Land Cruisers zinazofunguka juu zinafaa zaidi kwani zinanafasi ya kutosha ndani, madirisha makubwa na zinafika popote ndiyo maana zinagharama kubwa kukodi.
Endapo una gari binafsi utagharamika kununua mafuta ambayo yatatosha kuzungumza angalau 300km. Pia utalipia tozo ya gari kutokana na uzito wake. Gharama nyingine utakazolipa ni za kiingilio kutokana na idadi ya watu utakaokuwa nao na pia utamlipa muongoza watalii (tour guide) Ili akupeleke maeneo wanapopatikana wanyama Kwa urahisi. Gharama za tour guide Kwa siku inategemea a ila Kwa wastani ni shilingi elfu hamsini (50,000/=).
Chakula unaweza andaa chako au ukanunua nje ya HIFADHI kupunguza gharama.
Karibu sana mkuu, unaweza nicheki nikakupeleka wakati wote.
Mnaweza ungana mkawa wengi Ili kupunguza gharama ya mmojammoja.
Kumbe siyo garama sana
Kumbe siyo garama sana
Kumbe siyo garama sana
Akati huyo nyani ukienda hapo udsm unawaona bure kabisa.Utalii wa ndani gharama zote hizo...waambie wapunguze ili twende wengi..800k kumuona nyani tu
Asante Kwa kufafanua kiongozi.Baba,mama na watoto wawili ni familia ya watu wanne sio watatu 😇😎
Naunga mkono hoja,Utalii wa ndani gharama zote hizo...waambie wapunguze ili twende wengi..800k kumuona nyani tu
Unadhani kwako wewe binafsi unaweza mudu kiasi GANI bosi?Utalii wa ndani gharama zote hizo...waambie wapunguze ili twende wengi..800k kumuona nyani tu
Kiuhalisia gharama unazolipa ni kwaajili na kuwafanya waendelee kuwepo, yaani gharama za uhifadhi. Hizo gharama nyingine ni kwaajili tu ya kuweka mazingira rafiki ya kufikapo. Karibu sana.Unatoa pesa kwenda kuangalia wanyama walioletwa na mungu
Mimi nikija na familia na gari langu..natakiwa nilipe 50k tu boss....nipewe mtu anizungushe siku nzima...Una
Unadhani kwako wewe binafsi unaweza mudu kiasi GANI bosi?
Inaweza pungua kama nilivyofafanua ila huduma inakua siyo nzuri kiivo. Tatizo ni gharama ya kukodi gari, kuweka mafuta na kuilipia tozo ya kuingilia hifadhini.800,000 parefu mnooo
Akati huyo nyani ukienda hapo udsm unawaona bure kabisa.
Kwa mtanzania kuingia hifadhini gharama ni elfu kumi na Moja na mia nane (11,800/=). Hiyo ni tozo ya kiingilio tu. Tatizo ni kwenye usafiri ndugu. Hapo ndipo zinapojitokeza gharama ambazo wengi hawazimudu.Naunga mkono hoja,
Kwa hizo gharama,
watanzania wengi kuzimudu Ni changamoto.
Wengi wanazeeka mpk wanakufa hawajatembelea vivutio vya ndani.
Hahahah misimu 10 ni mingi sana mkuu, Fanya msimu mmoja tu. Karibu sana!Asante mkuu. Nilikuwa na ndoto za kuja huko nikitokea SONGEA... Sasa bahati mbaya tumepigwa na kitu kizito. Mbolea ni 107000mfuko. Na mahindi ni elf33gunia. . Ngoja nilime kwanza misimu 10 tena ya mvua
Epuka yote hayo kwa kukaa ndani tu.Sasa hizi kodi tunalipa ngap..
Umetoka kigamboni na kagar kako...daraja unalipia...
Umeenda sheli..kodi unalipia..
Umefika serengeti..kodi ya uzito wa gari
Bado uweke mafuta ya 300km..
Kulala unalipia..
Kula unalipia..
Bado swala ajipitishe umfyeke ulipie...
Aaassshh
Hiyo 50k inaweza kuwa tozo ya gari tu mkuu, mtu wa kukuzungusha itabidi uongeze angalau 50k nyingine. Na Chakula uzingatie pia.Mimi nikija na familia na gari langu..natakiwa nilipe 50k tu boss....nipewe mtu anizungushe siku nzima...
BTW, hao watu tunaowalipa si watumishi wa umma?
Gharama ya siku moja laki nane? Hii ndo inasababisha mzungu anaweza kuizungumzia Serengeti au Ngorongoro kuliko mwenyejiMuda wote utaenjoy. Kuanzia mwezi wa sita Hadi wa kumi na Moja ndipo Kun wazungu wengi. Lakini siyo maeneo yote ya HIFADHI kwani Serengeti ni kubwa sana ni vigumu kuitembelea yote Kwa siku moja. Mara nyingi wazungu wqnapenda kufuatilia uhamiaji wa nyumbu, kwahiyo inawezekana kuitembelea maeneo mengine ambapo kunakuwa hakuna nyumbu kwani watu wanakuepo wachache.
Gharama ya kulala hostel ni 5600 Kwa usiku ila inakua kama bweni mnalala watu wengi, lodge gharama zinaanzia 20,000 Hadi 1,000,000 na campsite gharama hazitofautiani sana na za lodge.
Kwa safari ya siku moja Kwa budget ya kawaida andaa angalau kuanzia 800,000.
Karibu sana, unaweza nicheki Kwa namba hii nikupe muongozo zaidi....0625818341.