Itanigharimu kiasi gani kutalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti?

Itanigharimu kiasi gani kutalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti?

NItafafanua gharama za kuingia hifadhini kuanzia saa 12 asubuhi Hadi saa 12 Jioni (yaaani day trip) pamoja na Aina za usafiri na gharama zake kama ifuatavyo.

1. Kwa kutumia gari Aina ya LAND CRUISER inayofunguka juu (OPEN ROOF) na inayobeba Hadi WATU WANNE(four passenger seats) gharama ni shilingi 560,000/=. Gharama hizi zinahusisha kukodi gari, mafuta, Kodi ya gari inapoingia hifadhini, chakula Cha asubuhi na mchana, kiingilio Cha watu 4.
Mkiwa kikundi Cha watu 4 hapa Kila mmoja atalipia angalau 140,000/=.

2. Kwa kutumia gari Aina ya LAND CRUISER inayofunguka juu (OPEN ROOF) na inayobeba Hadi WATU SITA (six passenger seats) gharama ni shilingi 700,000/=. Jumla ya watu hapa mtakua 6, endapo mtakua pungufu gharama zitapungua kidogo kwenye chakula na kiingilio hifadhini. Kwa kawaida kiingilio ni shilingi elfu kumi na mbili (12,000/=) Kwa mtu mzima kuanzia miaka 16. Watoto chini ya miaka 5 ni bure. Wastani gharama ya chakula Kwa mtu mmoja ni shilingi elfu kumi (10,000/=) Kwa breakfast na lunch.
Mkiwa kikundi Cha watu 6 hapa Kila mmoja atalipia angalau 120,000/=.

3. Kwa kutumia gari Aina ya HIACE inayobeba Hadi WATU 7 HADI 12 gharama ni shilingi 750,000/=. Hapa mnaweza kuwa kikundi Cha Hadi watu 12, endapo mkiwa pungufu gharama zinaweza kupungua kidogo kama nilivyoelezea hapo juu.
Mkiwa kikundi Cha watu 12, hapa Kila mmoja atalipia angalau 65,000/=.

4. Kwa kutumia gari Aina ya COASTER AU TATA inayobeba wastani wa WATU 13 HADI 30 gharama itakuwa ni shilingi 1,500,000/= (milioni Moja na nusu). Mkiwa pungufu ya idadi hiyo gharama itapunguza kidogo pia.
Mkiwa kikundi cha watu 30 hapa Kila mmoja atalipia angalau 50,000/=.

5. Kwa kutumia gari Aina ya NOAH inayoweza kubeba WATU 2 HADI 6 gharama itakuwa shilingi 450,000/= (laki nne na nusu).
Mkiwa kikundi Cha watu 6 hapa Kila mmoja atalipia angalau 75,000/=.


Kumbuka Gharama hizo ni Kwa jumla na zinabadirikabadirika kutokana na Aina ya gari utakayopenda kutumia. Land Cruisers zinazofunguka juu zinafaa zaidi kwani zinanafasi ya kutosha ndani, madirisha makubwa na zinafika popote ndiyo maana zinagharama kubwa kukodi.

Endapo una gari binafsi utagharamika kununua mafuta ambayo yatatosha kuzungumza angalau 300km. Pia utalipia tozo ya gari kutokana na uzito wake. Gharama nyingine utakazolipa ni za kiingilio kutokana na idadi ya watu utakaokuwa nao na pia utamlipa muongoza watalii (tour guide) Ili akupeleke maeneo wanapopatikana wanyama Kwa urahisi. Gharama za tour guide Kwa siku inategemea a ila Kwa wastani ni shilingi elfu hamsini (50,000/=).
Chakula unaweza andaa chako au ukanunua nje ya HIFADHI kupunguza gharama.

Karibu sana mkuu, unaweza nicheki nikakupeleka wakati wote.
Mnaweza ungana mkawa wengi Ili kupunguza gharama ya mmojammoja.
Kwa gari binafsi umesema mafuta ya kuzunguka 300klm

Kilometer 300 ni nyingi sana,huo ni umbali mrefu sana mbona iwapo nitakuja kwa siku moja tu au mbili,wastani angalau nitembee 90kilometer per day
 
Mkuu samahani, urahisi wa kuingia hifadhini ni kutokea Arusha huku au mwanza? Au je wewe unawapokea wateja wako kutokea upande upi?
M nawapokea watu upande wa Ikoma gate iliyoko jirani na mji wa mgm ila kutokea mwanza nikarb maana ukitokea Arusha itakuradhimu kufk mpaka mjin mgm ndipo uludi Tena hifadhini mkuu maelezo zaid 0625818341
 
Kwa gari binafsi umesema mafuta ya kuzunguka 300klm

Kilometer 300 ni nyingi sana,huo ni umbali mrefu sana mbona iwapo nitakuja kwa siku moja tu au mbili,wastani angalau nitembee 90kilometer per day
Nikweli lakin inategemea na wanyama watakuwa umbali gan mkuu
 
Mkuu hongera sema wewe ni wa kampuni binafsi koz naona gharama ziko juu sana. Kwani hao Tanapa hawana guides? Au magari. Na kama hawana magari Ina maana mtu akienda bila gari la kuzungukia ndani wanakubali au wanakataa?
 
Mi naomba kuuliza kwa mfano nikienda mimi mwenyewe binafsi mfano kupanda mlima Kilimanjaro na nikafika nikaanza kuupanda bila kulipia chochote je ni kosa?
 
Mkuu kama sitaki kuzungushwa na gari, gharama zinakuaje? Kuna kitu kinaitwa walking safari, mtalii anatembezwa kwa mguu na tour guide, gharama zake zimekaaje hapo?
 
😂😂😂😂😂😂 aiseee ubahili huu mkuu unatakujaga uliwe tu na simba , kweli mbugani ukazunguke kwa miguu kweli ?
 
Umemaanisha jumla ni watu saba?
Kwa watoto chini ya miaka mitano hawalipii kiingilio hivyo basi gharama zao zitakua chakula na usafiri.
Kama mtapendelea kulala ndani ya HIFADHI gharama zitaanzia shilingi laki nane (800,000).
KAma mtalala nje ya HIFADHI gharama zitakua kati ya laki sita Hadi saba (600,000-700,000).
Kumbuka nje ya HIFADHI gharama za lodge nzuri tu za kawaida ni kuanzia elfu kumi na Tano.
KAribu sana mkuu Serengeti.
Familia ya baba, mama na watoto watatu wa umri wa miaka 9, 5 na 3 tukitaka tours ya kuanzia tarehe 24 hadi 30 ndani ya Hifadhi , minimum budget inaweza ikawa kiasi gani? Ushauri wako kuhusu kulala Lodge, Campsite au Hostel ni muhimu , kumbuka nahitaji minimum cost as much as possible
 
Ukipanda hii mashine kutoka Musoma kwenda Arusha kupitia Mugumu au kutoka Arusha kwenda Musoma kupitia Mugumu utalii utakuwa umemaliza.
20211202_224036.jpg
 
NItafafanua gharama za kuingia hifadhini kuanzia saa 12 asubuhi Hadi saa 12 Jioni (yaaani day trip) pamoja na Aina za usafiri na gharama zake kama ifuatavyo.

1. Kwa kutumia gari Aina ya LAND CRUISER inayofunguka juu (OPEN ROOF) na inayobeba Hadi WATU WANNE(four passenger seats) gharama ni shilingi 560,000/=. Gharama hizi zinahusisha kukodi gari, mafuta, Kodi ya gari inapoingia hifadhini, chakula Cha asubuhi na mchana, kiingilio Cha watu 4.
Mkiwa kikundi Cha watu 4 hapa Kila mmoja atalipia angalau 140,000/=.

2. Kwa kutumia gari Aina ya LAND CRUISER inayofunguka juu (OPEN ROOF) na inayobeba Hadi WATU SITA (six passenger seats) gharama ni shilingi 700,000/=. Jumla ya watu hapa mtakua 6, endapo mtakua pungufu gharama zitapungua kidogo kwenye chakula na kiingilio hifadhini. Kwa kawaida kiingilio ni shilingi elfu kumi na mbili (12,000/=) Kwa mtu mzima kuanzia miaka 16. Watoto chini ya miaka 5 ni bure. Wastani gharama ya chakula Kwa mtu mmoja ni shilingi elfu kumi (10,000/=) Kwa breakfast na lunch.
Mkiwa kikundi Cha watu 6 hapa Kila mmoja atalipia angalau 120,000/=.

3. Kwa kutumia gari Aina ya HIACE inayobeba Hadi WATU 7 HADI 12 gharama ni shilingi 750,000/=. Hapa mnaweza kuwa kikundi Cha Hadi watu 12, endapo mkiwa pungufu gharama zinaweza kupungua kidogo kama nilivyoelezea hapo juu.
Mkiwa kikundi Cha watu 12, hapa Kila mmoja atalipia angalau 65,000/=.

4. Kwa kutumia gari Aina ya COASTER AU TATA inayobeba wastani wa WATU 13 HADI 30 gharama itakuwa ni shilingi 1,500,000/= (milioni Moja na nusu). Mkiwa pungufu ya idadi hiyo gharama itapunguza kidogo pia.
Mkiwa kikundi cha watu 30 hapa Kila mmoja atalipia angalau 50,000/=.

5. Kwa kutumia gari Aina ya NOAH inayoweza kubeba WATU 2 HADI 6 gharama itakuwa shilingi 450,000/= (laki nne na nusu).
Mkiwa kikundi Cha watu 6 hapa Kila mmoja atalipia angalau 75,000/=.


Kumbuka Gharama hizo ni Kwa jumla na zinabadirikabadirika kutokana na Aina ya gari utakayopenda kutumia. Land Cruisers zinazofunguka juu zinafaa zaidi kwani zinanafasi ya kutosha ndani, madirisha makubwa na zinafika popote ndiyo maana zinagharama kubwa kukodi.

Endapo una gari binafsi utagharamika kununua mafuta ambayo yatatosha kuzungumza angalau 300km. Pia utalipia tozo ya gari kutokana na uzito wake. Gharama nyingine utakazolipa ni za kiingilio kutokana na idadi ya watu utakaokuwa nao na pia utamlipa muongoza watalii (tour guide) Ili akupeleke maeneo wanapopatikana wanyama Kwa urahisi. Gharama za tour guide Kwa siku inategemea a ila Kwa wastani ni shilingi elfu hamsini (50,000/=).
Chakula unaweza andaa chako au ukanunua nje ya HIFADHI kupunguza gharama.

Karibu sana mkuu, unaweza nicheki nikakupeleka wakati wote.
Mnaweza ungana mkawa wengi Ili kupunguza gharama ya mmojammoja.
Ah bora Nile zangu bata
 
ITANIGHARIMU KIASI GANI KUTALII KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI?
Napenda kuchukua nafasi hii kutoa ufafanuzi kwa wale wanaotamani kwenda kutalii lakini hawajui itawagharimu shilingi ngapi.

Gharama ya kutalii mara nyingi inabadirika kutegemeana na sababu mbalimbali kama vile...

Kampuni utakayotaka kutumia, upatikanaji wa gari(kama ni gari binafsi au ya kukodi), chakula, na malazi endapo utapenda kulala hifadhini.

Kwa ufupi tu makadirio ya upesi kwa kundi la watu 2 hadi 5 itagharimu kuanzia laki 5 kuendelea kwa safari ya siku moja (Day Trip). Na kwa kundi la watu 6 hadi 12 itagharimu kuanzia laki 6 na kuendelea. Kama safari itahusisha kulala hifadhini gharama zinaweza ongezeka kutegemea na endapo utachagua kulala lodge, campsite au hostel.

Endapo pia utatumia gari binafsi gharama zinaweza kupungua Hadi kufikia shilingi laki 2-3 kwa kundi la watu 2 hadi 5.
Kumbuka: Gharama zinahusisha kiingilio Cha HIFADHI, chakula, muongoza watalii na tozo ya gari.

KAMA UNA SWALI LOLOTE TAFADHARI ULIZA NA NITAKUJIBU HAPAHAPA!
Kwa wakazi wa mikoa ya kaskazini, pwani na kati kama vile Arusha, Kilimanjaro, Dodoma, Tanga, Pwani n.k wanaweza kwenda Hadi Arusha au Moshi na kuzungumza na kampuni za watalii zinazopatikana maeneo hayo.

Kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa inapendeza zaidi kuanzia safari yao katika mji wa Mugumu kupitia geti la Tabora-B au Ikoma na kumalizia katika geti la Ndabaka.
Binafsi napatikana katika mji wa Mugumu, Wilayani Serengeti.
Asante!


View attachment 2037071
Million 30 mkuu

Nimesoma mimi

Nisiusishe na lolote mkuuu
 
Tanapa hawana guides, ikitokea ukaenda bila gari hautaruhusiwa kuzunguka hifadhini. Sanasana watakuunganisha na kampuni binafsi Ili upate gari. Gharama zinaweza kuwa kubwa zaidi kulinganisha na endapo utapanga safari mapema na kupat gari.
Karibu.

Mkuu hongera sema wewe ni wa kampuni binafsi koz naona gharama ziko juu sana. Kwani hao Tanapa hawana guides? Au magari. Na kama hawana magari Ina maana mtu akienda bila gari la kuzungukia ndani wanakubali au wanakataa?
 
Familia ya baba, mama na watoto watatu wa umri wa miaka 9, 5 na 3 tukitaka tours ya kuanzia tarehe 24 hadi 30 ndani ya Hifadhi , minimum budget inaweza ikawa kiasi gani? Ushauri wako kuhusu kulala Lodge, Campsite au Hostel ni muhimu , kumbuka nahitaji minimum cost as much as possible
Samahani Kwa kuchelewa kukujibu mkuu.
Kwa ufupi safari hii itakuwa ya 7 days na 6 nights. Kwa mtazamo wangu naona itakuwa vizuri kama ukilala lodges za bei nafuu. Kwa siku hizo sita ndani ya Serengeti pekee itapendeza kama ukilala kwenye lodges/hotel angalau tatu tofauti katika maeneo tofauti yaani siku mbili utalala Kaskazini mwa Serengeti mpakani mwa Tanzania na Kenya katika maeneo ya Kogatende. Siku mbili utalala katikati ya Serengeti yaani Seronera na Siku mbili za mwisho utalala Kusini Magharibi mwa HIFADHI karibu za Ziwa Victoria.

Chaguo lingine ambalo linaweza kupendeza ni kuunganisha safari Yako katika HIFADHI ya Ngorongoro yaani unakaa siku nne Serengeti na siku tatu Ngorongoro. Gharama hazitofautiani sana na endapo utatumia siku zote ndani ya Serengeti.
Gharama nimekutumia inbox. Karibu sana mkuu.
0625818341
 
Kwa gari binafsi umesema mafuta ya kuzunguka 300klm

Kilometer 300 ni nyingi sana,huo ni umbali mrefu sana mbona iwapo nitakuja kwa siku moja tu au mbili,wastani angalau nitembee 90kilometer per day
Mkuu 90km Kwa Serengeti ni chache sana. Kumbuka Ina ukubwa wa zaidi kilomita za mraba elfu 14. Eneo kubwa ni tambarare tu yenye nyasi ndefu na wanyama wachache. Hivyo basi Ili uifaidi vizuri inakubidi utembee eneo kubwa zaidi.
Karibu sana tukuhudumie msimu huu wa Krismasi na Mwaka Mpya.
 
Ukipanda hii mashine kutoka Musoma kwenda Arusha kupitia Mugumu au kutoka Arusha kwenda Musoma kupitia Mugumu utalii utakuwa umemaliza. View attachment 2046152
Hii pia ni chaguo zuri Kwa wale wenye budget ndogo ambapo itakugharimu angalau shilingi elfu 45 ya nauli kutoka Arusha Hadi Mugumu, Musoma au Tarime kupitia Ngorongoro na Serengeti. Tatizo la kutumia njia hii ni kwamba utawaona wanyama wale tu walioko pembeni ya barabara. Kwa vivutio vingine vilivyo mbali na barabara ni vigumu kuviona.
Karibuni Serengeti!
 
Back
Top Bottom