Itanigharimu kiasi gani kutalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti?

Kumbe siyo garama sana
 
Sasa hizi kodi tunalipa ngap..
Umetoka kigamboni na kagar kako...daraja unalipia...
Umeenda sheli..kodi unalipia..
Umefika serengeti..kodi ya uzito wa gari
Bado uweke mafuta ya 300km..
Kulala unalipia..
Kula unalipia..
Bado swala ajipitishe umfyeke ulipie...
Aaassshh
 
Baba,mama na watoto wawili ni familia ya watu wanne sio watatu 😇😎
Asante Kwa kufafanua kiongozi.
Kwa familia ya watu WANNE (watoto umesema ni chini ya miaka mitano) safari ya siku moja pamoja na kulala(1 day & 1 night) kwa kutumia gari Aina ya Landcruiser itawagharimu jumla shilingi laki saba (700,000/=). Hii inamaanisha kuwa mtakaa ndani ya HIFADHI Kwa masaa 24 pekee. Yaani mkiingia saa 2 asubuhi itabidi mtoke kabla ya saa 2 kesho yake.
Endapo mkitaka kukaa zaidi gharama zitaongezeka kiasi.
 
Unachosema ni ukweli kabisa lakini kutokana na mazingira ya kuwafikia hao nyani ndipo tofauti zinapojitokeza. Pengine inakua bure, pengine unalipia. Kwa mfano, Mimi nilieko Serengeti haiwezi kuwa bure kuja HUKO udsm kuwaona hao nyani. Lazima nigharamike, nilipe nauli, chakula na hata kulala.
Karibu Serengeti Mkuu!
Akati huyo nyani ukienda hapo udsm unawaona bure kabisa.
 
Naunga mkono hoja,

Kwa hizo gharama,
watanzania wengi kuzimudu Ni changamoto.

Wengi wanazeeka mpk wanakufa hawajatembelea vivutio vya ndani.
Kwa mtanzania kuingia hifadhini gharama ni elfu kumi na Moja na mia nane (11,800/=). Hiyo ni tozo ya kiingilio tu. Tatizo ni kwenye usafiri ndugu. Hapo ndipo zinapojitokeza gharama ambazo wengi hawazimudu.
Serikali Haina magari kiivo kusema ndo yatumike kukuzungusha kutalii. Endapo yangekuwepo ya kutosha labda gharama zingepungua zaidi.
 
Asante mkuu. Nilikuwa na ndoto za kuja huko nikitokea SONGEA... Sasa bahati mbaya tumepigwa na kitu kizito. Mbolea ni 107000mfuko. Na mahindi ni elf33gunia. . Ngoja nilime kwanza misimu 10 tena ya mvua
Hahahah misimu 10 ni mingi sana mkuu, Fanya msimu mmoja tu. Karibu sana!
 
Epuka yote hayo kwa kukaa ndani tu.
 
Mimi nikija na familia na gari langu..natakiwa nilipe 50k tu boss....nipewe mtu anizungushe siku nzima...
BTW, hao watu tunaowalipa si watumishi wa umma?
Hiyo 50k inaweza kuwa tozo ya gari tu mkuu, mtu wa kukuzungusha itabidi uongeze angalau 50k nyingine. Na Chakula uzingatie pia.
Wafanyakazi wa serikali hawausiki kukuzungusha, ni watu binafsi kama sisi yaani tour guides.
Karibu tukuhudumie. 0625818341
 
Gharama ya siku moja laki nane? Hii ndo inasababisha mzungu anaweza kuizungumzia Serengeti au Ngorongoro kuliko mwenyeji

Yaani mTanzania anazaliwa mpaka anakufa hajawahi kufika Serengeti au amepita na na Cost line bus la Musoma- Arusha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…