Kwa tafakuri yangu binafsi,napata shida kuamini kuwa kwa mifumo yetu na katiba yetu ya sasa upinzani kuchukua nchi ni ndoto za mchana,kuingia kwenye uchaguzi chini ya tume hii ya uchaguzi,na sheria hizi zilizopo ambazo zinatoa fursa ya tume kumtangaza mshindi,(iwe ndiye mshindi au lah),tume hii hii ambayo kama ikionenekana upinzani unaelekea kuchukua dola WANAFUTA MCHAKATO MZIMA WA UCHAGUZI na kuanza upya,Sina imani kama upinzani wanaweza kuchukua dola.
Ushauri wangu,pamoja na kukijenga chama kwa nguvu zote,iende sambamba na kudai katiba mpya itakayojenga misingi imara ya taasisi hizi nyeti,(Tume huru kabisa ya uchaguzi,pamoja na kuvifanya vyombo vya dola kuwa free and neutral figures wakati wa uchaguzi) ili waweze kufanya kazi pasipo kuegemea upande wowote wa wagombea.
Lakini kama tukibaki katika mfumo HUU wa sasa,hata kama upinzani utapata asilimia 80,na CHICHIEM wakapata 20,bado CCM watatangazwa kuwa washindi,na hakuna kitakachotokea zaidi ya raia kulia lia tu,kitu ambacho kimsingi hakisaidii hata kidogo.
Good reference ni ZANZIBAR!!!