Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Nilikuwa naangalia taarifa ya habari ITV wakawa wanahabarisha kuhusu Benki kuu(BoT) kuondoa zile noti za zamani katika mzungu, cha ajabu katika kupata watu wa kutoa maoni kuhusu hilo jambo badala ya kuwatafuta wataalamu wa biashara, fedha, au uchumi kutoka taasisi mbalimbali za hadhi ya juu kama vyuo vikuu au benki wao wakaenda mtaani kuokoteza watu wasiojua chochote kuhusu mfumo wa fedha.
Wameenda kutafuta sijui ni watembeza maji au wamachinga wakaanza kuwauliza maswali wafanye uchambuzi! Mwingine anaitwa mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Dar yeye akasema hili suala litachangia ku "stabilize" shilingi yetu, nilipoons huu upupu hapo nikazima na TV na kuendelea na mambo mengine kabisa.
Wameenda kutafuta sijui ni watembeza maji au wamachinga wakaanza kuwauliza maswali wafanye uchambuzi! Mwingine anaitwa mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Dar yeye akasema hili suala litachangia ku "stabilize" shilingi yetu, nilipoons huu upupu hapo nikazima na TV na kuendelea na mambo mengine kabisa.